Friday, December 28, 2012

BPL: NI MOTO KUAGA 2012 WIKIENDI!!!

BPL_LOGOKLABU ZOTE 20 zitaingia dimbani Jumamosi na Jumapili kucheza Mechi zao za mwisho za Mwaka 2012 kwenye BPL, Barclays Premier League, kwa akina sie tunaiita Ligi Kuu England, na zipo Mechi kadhaa ambazo, bila shaka, zitakuwa tamu na mvuto, na baadhi ya hizo ni zile za Arsenal v Newcastle, Everton v Chelsea.

Zifuatazo ni Dondoo muhimu kuhusu mitanange hiyo ikiwa pamoja na Hali za Wachezaji wa kila Timu na Marefa:
+++++++++++++++++++++++

RATIBA:  

Jumamosi 29 Desemba 2012
[SAA 9 Dak 45 Mchana]
Sunderland v Tottenham

[SAA 12 Jioni]
Aston Villa v Wigan
Fulham v Swansea
Man United v West Brom
Norwich v Man City
Reading v West Ham
Stoke v Southampton

[SAA 2 na Nusu Usiku]
Arsenal v Newcastle

+++++++++++++++++++++++
SUNDERLAND V TOTTENHAM HOTSPUR 
Sunderland wataivaa Spurs bila Beki wa kushoto Danny Rose ambae haruhusiwi kucheza dhidi ya Klabu yake Tottenham kwa vile yupo hapo Sunderland kwa Mkopo.
Badala ya Danny Rose, huenda Sunderland wakamchezesha Phil Bardsley kwenye nafasi hiyo.
Tottenham wanaweza kuwa nao tena majeruhi wao waliopona Clint Dempsey na Tom Huddlestone na pia upo uwezekano wa Wachezaji wao walioumia kwa muda mrefu na sasa kuwa fiti kuanza Mechi yao ya kwanza na hao ni Benoit Assou-Ekotto na Scott Parker.

MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Sunderland 1 Man City 0
Aston Villa 0 Tottenham 4
Refa: Martin Atkinson
[Gemu; 15 Kadi za Njano 59 Kadi Nyekundu: 0]
Wasaidizi: P Kirkup & S Burt
Refa wa Akiba: Mike Dean

ARSENAL V NEWCASTLE UNITED 
Wachezaji wawili wa Arsenal, Olivier Giroud na Tomas Rosicky, wameshapona na wanaweza kucheza kwenye Mechi kama watapangwa lakini Andre Santos na Abou Diaby bado ni majeruhi na wanatarajiwa kurudi Wiki ijayo.
Newcastle wana majeruhi kwa Wachezaji wao wanane na hivi karibuni Listi hiyo imeongezeka na Vurnon Anita (enka) na Jonas Gutierrez (goti).
Kiungo wa Newcastle Cheick Tiote amemaliza Kifungo chake cha Mechi moja lakini Mike Williamson atatumikia Kifungo cha Mechi moja baada ya kufikisha Kadi za Njano 5.
MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Man United 4 Newcastle 3
Wigan 0 Arsenal 1
Refa: Chris Foy
[Gemu: 13 Kadi za Njano: 21 Kadi Nyekundu: 0]
Wasaidizi: S Child & H Lennard Refa wa Akiba: Anthony Taylor
 
NORWICH CITY V MANCHESTER CITY 
Norwich watacheza bila ya Beki wao Steven Whittaker ambae ni majeruhi na nafasi yake itachukuliwa na Russell Martin.
Manchester City wanaweza kuwa nao tena Samir Nasri na Gael Clichy ambao wamepona maumivu yao lakini watamkosa Mchezaji wao machachari Mario Balotelli ambae ni mgonjwa.

MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Norwich 0 Chelsea 1
Sunderland 1 Man City 0
Refa: Mike Jones
[Gemu: 12 Kadi za Njano: 44 Kadi Nyekundu: 1]
Wasaidizi: S Ledger & M McDonough
Refa wa Akiba: Craig Pawson

MANCHESTER UNITED V WEST BROMWICH ALBION
Manchester United watakuwa nao tena Danny Welbeck, ambae amepona ugonjwa, na majeruhi Ashley Young na Phil Jones waliopona maumivu.
Nae Shinji Kagawa ameshapona Goti lake na anatarajiwa kuanzia Benchi kwa mujibu wa Meneja wao Sir Alex Ferguson.
Majeruhi wa West Brom ni Beki Jonas Olsson, Goran Popov na Kiungo Youssouf Mulumbu.

MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Man United 4 Newcastle 3
QPR 1 West Brom 2
Refa: Jon Moss
[Gemu: 10 Kadi za Njano: 27 Kadi Nyekundu: 1]
Wasaidizi: A Garratt & C Breakspear
Refa wa Akiba: Phil Dowd  

READING V WEST HAM UNITED
Meneja wa Reading Brian McDermott amethibitisha hawana majeruhi na pia upo uwezekano wa Straika wao Jason Roberts kucheza baada ya kupona maumivu.
Straika wa West Ham Carlton Cole anaweza kucheza baada ya FA kuifuta Kadi Nyekundu aliyopewa Wiki iliyopita walipocheza na Everton.

MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Reading 0 Swansea 0
West Ham 1 Everton 2
Refa: Michael Oliver
[Gemu:: 11 Kadi za Njano: 26 Kadi Nyekundu: 1]
Wasaidizi: S Bennett & M Scholes
Refa wa Akiba: Paul Tierney

ASTON VILLA V WIGAN ATHLETIC 
Timu hizi zote hazina Listi za majeruhi lakini zinatoka kwenye vipigo vizito mfululizo.
MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Aston Villa 0 Tottenham 4
Everton 2 Wigan 1
Refa: Kevin Friend
[Gemu: 11 Kadi za Njano: 42 Kadi Nyekundu: 2]
Wasaidizi: J Flynn & D England
Refa wa Akiba: Howard Webb

FULHAM V SWANSEA CITY  
Fulham hawana majeruhi lakini Swansea kuna hatihati kuhusu Wachezaji wao Mahamadou Diarra, Mladen Petric na Straika wao hatari Muchu ambao wana maumivu.
MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Fulham 1 Southampton 1
Reading 0 Swansea 0
Refa: Andre Marriner
[Gemu: 10 Kadi za Njano: 38 Kadi Nyekundu: 0]
Wasaidizi: R West & S Massey
Refa wa Akiba: Neil Swarbrick

STOKE CITY V SOUTHAMPTON 
Bosi wa Stoke City Tony Pulis atalazimika kutafuta Mabeki wengine kwa vile Nahodha wao Ryan Shawcross na Geoff Cameron wote wapo kwenye Kifungo cha Mechi moja baada kulimbikiza Kadi za Njano 5 kila mmoja.
Southampton watamkosa Nahodha Adam Lallana ambae ameumia goti.
MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Stoke 3 Liverpool 1 
Fulham 1 Southampton 1
Refa: Mark Clattenburg
[Gemu: 10 Kadi za Njano: 35 Kadi Nyekundu: 4]
Wasaidizi: S Beck & S Long
Refa wa Akiba: Lee Mason

+++++++++++++++++++++++

MECHI ZIJAZO:  
Jumapili 30 Desemba 2012 

[SAA 10 na Nusu Jioni]
Everton v Chelsea
[SAA 1 Usiku]
QPR v Liverpool

Jumanne 1 Januari 2013
SAA 9 Dak 45 Mchana]
West Brom v Fulham

[SAA 12 Jioni]
Man City v Stoke
Swansea v Aston Villa
Tottenham v Reading
West Ham v Norwich
Wigan v Man United

[SAA 2 na Nusu Usiku]
Southampton v Arsenal

Jumatano 2 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Chelsea v QPR
Liverpool v Sunderland

[SAA 5 Usiku]
Newcastle v Everton

1 comment:

  1. oya timu zote zinamaliza ligi zikiwa na idadi sawa ya michezo zilizocheza? Amna ambaye ana mchezo mkononi?

    ReplyDelete