Saturday, December 22, 2012

LEO TAIFA STARS V CHIPOLOPOLO

KATONGOTimu za Taifa za Tanzania, Taifa Stars, na Zambia, Chipolopolo, ambao ndio Mabingwa wa Afrika, leo kuanzia Saa 10 Jioni zitashuka Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kucheza Mechi ya Kimataifa ya Kirafiki.
Mara ya mwisho Timu hizi kukutana ilikuwa ni Mwaka 2010 kwenye Mechi ya ufunguzi ya Chalenji Cup na Chipolopolo kushinda Bao 1-0.
Leo, Chipolopolo, wataongozwa na Nahodha wao Christopher Katongo, ambae juzi alitunukiwa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Afrika na BBC, Shirika la Utangazaji la Uingereza.
Stars, ambao wako chini ya Kocha toka Denmark, Kim Poulsen, wataingia kwenye Mechi hii bila ya Wachezaji wao wawili wanaocheza huko TP Mazembe, Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu ambao wameripotiwa kuwepo Dar es Salaam lakini ni majeruhi.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
AFCON 2013
MAKUNDI:
KUNDI A: South Africa, Cape Verde, Morocco, Angola
KUNDI B: Ghana, DR Congo, Niger, Mali
KUNDI C: Zambia, Ethiopia, Nigeria, Burkina Faso
KUNDI D: Ivory Coast, Togo, Tunisia, Algeria
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Chipolopolo leo wataongezewa nguvu baada ya kuwasili kwa Kocha wao Mkuu Herve Renard ambae alikuwa Accra, Ghana akipokea TuzoTAIFA_STARS-small toka CAF ya kuwa Kocha Bora wa Afrika ambako pia Zambia ilitajwa kuwa ndio Timu Bora Afrika kwa 2012 baada ya kutwaa Ubingwa wa Afrka, AFCON 2012, huko Gabon Mwezi Februari Mwaka huu.
Mwezi Januari, Chipolopolo watakuwa huko Afrika Kusini kuanza utetezi wa Ubingwa wao wa Afrika kwenye michuano ya Kombe la Mataifa Afrika, AFCON 2013, itakayochezwa kuanzia Januari 19 HADI Februari 10.
Taifa Stars wao wapo kwenye vinyang’anyiro vya Mechi za Mchujo za CHAN, Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa ndani wa Afrika, na Kombe la Dunia la 2014, na Mechi hizo watazicheza Mwakani.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa Sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, Sh. 7,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, Sh. 10,000 kwa VIP C, Sh. 20,000 kwa VIP B wakati VIP A itakuwa Sh. 30,000.
Tiketi zilianza kuuzwa tangu jana kwenye vituo vya Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Uwanja wa Uhuru, Mgahawa wa Steers ulioko Mtaa wa Ohio na Samora, Sokoni Kariakoo, kituo cha mafuta cha Ubungo OilCom na Dar Live Mbagala.

No comments:

Post a Comment