Saturday, December 22, 2012

Real yaaga Mwaka kwa kichapo, Barca yapaa, Inter yanasa!

BARCA_v_REALLIGI za Spain na Italy hapo jana ziliaga Mwaka 2012 kwa Mechi zao za mwisho na kwenda Vakesheni hadi Januari 6 huku Mabingwa wa Spain, Real Madrid, wakitandikwa kwenye La Liga na kutupwa Pointi 17 nyuma ya vinara Barcelona wakati huko Serie A Inter Milan walijikuta wakishushwa hadi nafasi ya 4 na Mabingwa Juventus kubaki kileleni Pointi 8 mbele.

Wakati Barcelona ikishinda ugenini kwa kuichapa Real Valladolidi Bao 3-1 kwa Bao za Xavi, Lionel Messi na Tello, Real Madrid walichapwa 3-2 ugenini na Malaga ambao walifunga Bao zao kupitia Isco na Santa, bao mbili, na Real kufunga kwa Bao za Sanchez, kujifunga mwenyewe, na Karim Benzema.

Barcelona wamefunga Mwaka wakiwa kileleni na wana Pointi 40, wakifuatiwa na Atletico Madrid wenye Pointi 40, Real Madrid 33 na Malaga 31.

Huko Italy kwenye Serie A, Inter Milan walikosa nafasi ya kupunguza pengo lao na Mabingwa Juventus walio kileleni wakiwa na Pointi 44 baada ya kutoka sare 1-1 na Genoa na kujikuta wakiporomoka hadi nafasi ya 4.

Nafasi ya 2 imekamatwa na Lazio ambao waliwafunga Sampdoria 1-0 na Fiorentina kushika nafasi ya 3 baada ya kuifunga Palermo 3-0.
MATOKEO:

LA LIGA
Alhamisi Desemba 20
RCD Espanyol 2 Deportivo La Coruna 0
Real Sociedad 2 Sevilla 1
Rayo Vallecano 3 Levante 0
Ijumaa Desemba 21
Valencia 4 Getafe 2
Atletico Madrid 1 Celta Vigo 0
Jumamosi Desemba 22
Real Betis 1 Real Mallorca 2
Real Valladolid 1 FC Barcelona 3
Malaga 3 Real Madrid 2
Osasuna 1 Granada 2
Jumapili Desemba 23
Athletic Bilbao 0 Real Zaragoza 2 [IMECHEZWA JANA USIKU BAADA SAA 6]
**LIGI MAPUMZIKONI HADI JANUARI 6

MSIMAMO-Timu za Juu:
[Kila Timu imecheza Mechi 17]
1 Barcelona Pointi 49
2 Atletico Madrid 40
3 Real Madrid 33
4 Malaga 31
5 Real Betis 28
6 Levante 27
7 Real Sociedad 25

SERIE A
Ijumaa Desemba 21
Pescara 2 Catania 1
Cagliari 1 Juventus 3
Jumamosi Desemba 22
Inter Milan 1 Genoa 1
Atalanta 1 Udinese 1
Bologna 1 Parma 2
Torino FC 2 Chievo Verona 0
Sampdoria 0 SS Lazio 1
Siena 0 Napoli 2
Palermo 0 Fiorentina 3
AS Roma 4 AC Milan 2
**LIGI MAPUMZIKONI HADI JANUARI 6

MSIMAMO-Timu za Juu:
[Kila Timu imecheza Mechi 18]
1 Juventus Pointi 44
2 Lazio 36
3 Fiorentina 35
4 Inter Milan 35
5 Napoli 34
6 AS Roma 32
7 AC Milan 27
8 Parma 26

City yaikaribia United Pointi 3, Arsenal ni ya 3, Liverpool ipo 8!!

BPL_LOGOCHELSEA YASHUKA HADI 7, USHINDI JUMAPILI KUWARUDISHA 3!
MATOKEO:
Jumamosi 22 Desemba 2012
Wigan 0 Arsenal 1
Man City 1 Reading 0
Newcastle 1 QPR 0
Southampton 0 Sunderland 1
Tottenham 0 Stoke 0
West Brom 2 Norwich 1
West Ham 1 Everton 2
Liverpool 4 Fulham 0
+++++++++++++++++++++++
MSIMAMO:
=Tofauti ya Magoli inatajwa kwa Timu zilizofungana Pointi
1 Man United Mechi 17 Pointi 42
2 Man City Mechi 18 Pointi 39
3 Arsenal Mechi 18 Pointi 30 [Tofauti ya Magoli 14]
4 Everton Mechi 18 Pointi 30 [Tofauti ya Magoli 8]
5 Tottenham Mechi 18 Pointi 30 [Tofauti ya Magoli 5]
6 WBA Mechi 18 Pointi 30 [Tofauti ya Magoli 4]
7 Chelsea Mechi 16 Pointi 29 [Tofauti ya Magoli 11]
8 Liverpool Mechi 18 Pointi 25 [Tofauti ya Magoli 4]
9 Stoke Mechi 18 Pointi 25 [Tofauti ya Magoli 2]
10 Norwich Mechi 18 Pointi 25 [Tofauti ya Magoli -7]
11 Swansea Mechi 17 Pointi 23 [Tofauti ya Magoli 4]
12 West Ham Mechi 18 Pointi 23 [Tofauti ya Magoli 0]
13 Fulham Mechi 18 Pointi 20 [Tofauti ya Magoli -5]
14 Newcastle Mechi 18 Pointi 20 [Tofauti ya Magoli -6]
15 Sunderland Mechi 18 Pointi 19
16 Aston Villa Mechi 17 Pointi 18
17 Southampton 15 [Tofauti ya Magoli -10]
===============
18 Wigan Mechi 18 Pointi 15 [Tofauti ya Magoli -15]
19 QPR Mechi 18 Pointi 10
20 Reading Mechi 18 Pointi 9
+++++++++++++++++++++++

LIVERPOOL 4 FULHAM 0
Bao za Skrtel, Gerrard, Downing na Suarez, zimewapaisha Liverpool wakiwa kwao Anfield hadi nafasi ya 8 baada ya kuichapa Fulham Bao 4-0.
VIKOSI:
Liverpool: Reina, Johnson, Skrtel, Agger, Jose Enrique, Gerrard, Lucas, Shelvey, Fernandez Saez, Suarez, Downing
Akiba: Jones, Sahin, Henderson, Carragher, Allen, Sterling, Wisdom.
Fulham: Schwarzer, Riether, Hangeland, Hughes, Riise, Kacaniklic, Karagounis, Baird, Richardson, Dejagah, Berbatov
Akiba: Stockdale, Senderos, Kasami, Briggs, Rodallega, Frei, Tavares.
Refa: Mark Clattenburg

WEST BROM 2 NORWICH 1 
West Brom walimaliza wimbi la Norwich la kutofungwa katika Mechi 10 na wao wenyewe kutofunga Bao katika Masaa 6 ya Soka baada ya kutoka nyuma kwa Bao la Robert Snodgrass na kusawazisha kwa frikiki ya Zoltan Gera na kisha Romelu Lukaku kuwapa Bao la ushindi.
VIKOSI:
West Brom: Foster, Jones, McAuley, Olsson, Popov, Morrison, Brunt, Odemwingie, Gera, Dorrans, Lukaku
Akiba: Myhill, Ridgewell, Rosenberg, Long, Jara Reyes, Tamas, Fortune.
Norwich: Bunn, Whittaker, Bassong, Turner, Garrido, Snodgrass, Tettey, Hoolahan, Johnson, Pilkington, Morison
Akiba: Steer, Martin, Howson, Jackson, Elliott Bennett, Barnett, Kane.
Refa: Martin Atkinson

TOTTENHAM 0 STOKE 0
Tottenham wameipoteza nafasi ya kukamata nafasi ya 3 baada ya kubanwa na Stoke na kutoka sare 0-0 Uwanjani White Hart Lane.
Stoke sasa hawajafungwa katika Mechi 8.
VIKOSI:
Tottenham: Lloris, Walker, Dawson, Caulker, Vertonghen, Lennon, Sandro, Dembele, Bale, Defoe, Adebayor
Akiba: Friedel, Parker, Gallas, Naughton, Sigurdsson, Livermore, Townsend.
Stoke: Begovic, Wilkinson, Shawcross, Huth, Cameron, Shotton, Nzonzi, Whelan, Etherington, Jones, Walters
Akiba: Sorensen, Palacios, Whitehead, Upson, Kightly, Crouch, Jerome.
Refa: Lee Mason

NEWCASTLE 1 QPR 0
Shola Ameobi leo katika Dakika ya 81 amefunga Bao lake la 3 Msimu huu na kuwapa ushindi Newcastle wa Bao 1-0 dhidi ya QPR na kumfanya Meneja wa QPR, Harry Redknapp, apate kipigo chake cha kwanza katika himaya yake ya Mechi 4 Klabuni hapo.
VIKOSI:
Newcastle: Krul, Simpson, Coloccini, Williamson, Santon, Anita, Tiote, Perch, Gutierrez, Ba, Cisse
Akiba: Harper, Bigirimana, Marveaux, Shola Ameobi, Obertan, Sammy Ameobi, Ferguson.
QPR: Green, Da Silva, Ferdinand, Nelsen, Hill, Mackie, Mbia, Granero, Faurlin, Taarabt, Cisse
Akiba: Murphy, Diakite, Traore, Derry, Wright-Phillips, Onuoha, Hoilett.
Refa: Kevin Friend

SOUTHAMPTON 0 SUNDERLAND 1
Bao la 8 la Steven Fletcher kwenye Ligi leo limewapa ushindi Sunderland wa Bao 1-0 ugenini walipocheza na Southampton.
VIKOSI:
Southampton: Kelvin Davis, Clyne, Yoshida, Fonte, Shaw, Puncheon, Cork, Schneiderlin, Mayuka, Lambert, Ramirez
Akiba: Boruc, Hooiveld, Steven Davis, Rodriguez, Do Prado, Richardson, De Ridder.
Sunderland: Mignolet, Gardner, Cuellar, O'Shea, Rose, Johnson, Colback, Larsson, McClean, Sessegnon, Fletcher
Akiba: Westwood, Bardsley, Campbell, Wickham, McFadden, Vaughan, Bramble.
Refa: Howard Webb

WEST HAM 1 EVERTON 2
Leo Everton walitoka nyuma kwa Bao 1-0 Uwanjani Upton Park na kuwafunga West Ham Bao 2-1 lakini shukrani ziende kwa Refa Mark Anthony ambapo alimpa Kadi Nyekundu Shola Ameobi, Mfungaji wa Bao la West Ham, kwa rafu ambayo haikustahili na kufungua njia kwa Everton kusawazsha kupitia Victor Anichebe na kupiga Bao la pili la ushindi kupitia Steven Pienaar.
Baada ya Bao hizo Darron Gibson wa Everton alitolewa nje kwa Kadi Nyekundu na Refa Anthony Taylor baada ya kugongana na Mark Noble.
VIKOSI:
West Ham: Jaaskelainen, Tomkins, Collins, Reid, O'Brien, Noble, O'Neil, Taylor, Nolan, Jarvis, Cole
Akiba: Spiegel, Collison, Maiga, Diarra, Spence, Moncur, Lletget.
Everton: Howard, Heitinga, Jagielka, Distin, Baines, Osman, Gibson, Neville, Pienaar, Jelavic, Anichebe
Akiba: Mucha, Oviedo, Naismith, Hitzlsperger, Barkley, Vellios, Duffy.
Refa: Anthony Taylor

MAN CITY 1 READING 0
Bao la faulo la Gareth Barry la Dakika ya 92 limeipa Manchester City ushindi Manchester City wa 1-0 dhidi ya Klabu ya mkiani Reading na kuwafanya wawe Pointi 3 tu nyuma ya vinara Manchester United.
Mbali ya Bao hilo la utata, Reading pia walipigia kelele Penati mbili walizonyimwa na Refa Mike Dean na matukio hayo yalimkera sana Meneja wa Reading Brian McDermott ambae alilalamika sana kuhusu Refa huyo na maamuzi yake.
VIKOSI:
Man City: Hart, Zabaleta, Toure, Nastasic, Rekik, Barry, Javi Garcia, Toure, Silva, Aguero, Tevez
Akiba: Wright, Kompany, Lescott, Milner, Dzeko, Sinclair, Razak.
Reading: Federici, Gunter, Pearce, Mariappa, Harte, McAnuff, Leigertwood, Karacan, Tabb, Kebe, Pogrebnyak.
Akiba: Taylor, Shorey, Le Fondre, Hunt, Gorkss, Robson-Kanu, Guthrie.
Refa: Mike Dean

WIGAN 0 ARSENAL 1
Penati ya Dakika ya 60 ya Mikel Arteta leo imewapa Arsenal ushindi wao wa 3 mfululizo kwenye Ligi na kuwapaisha hadi nafasi ya 3.
Kipigo hiki kimewafanya Wigan wawe wamepoteza Mechi 6 kati ya 8 za Ligi walizocheza mwisho na pia kuwafanya kwa Misimu mitatu mfululizo wawe mkiani, nafasi 3 za chini, wakati wa Krismasi.
VIKOSI:
Wigan: Al Habsi; Stam, Boyce, Figueroa, Beausejour; McCarthy, McArthur, Jones; Di Santo, Kone, Maloney
Akiba: Pollitt, Caldwell, Gomez, McManaman, Boselli, Fyvie, Golobart

Arsenal: Szczesny, Sagna, Mertesacker, Vermaelen, Gibbs, Arteta, Wilshere, Oxlade-Chamberlain, 
Cazorla, Podolski, Walcott
Akiba: Mannone, Jenkinson, Koscielny, Coquelin, Ramsey, Arshavin, Gervinho.
Refa: Jon Moss
+++++++++++++++++++++++++++

RATIBA:
Jumapili 23 Desemba 2012
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Swansea v Man United
[SAA 1 Usiku]
Chelsea v Aston Villa

Jumatano 26 Desemba 2012
[SAA 12 Jioni]
Arsenal v West Ham
Everton v Wigan
Fulham v Southampton
Man United v Newcastle
Norwich v Chelsea
QPR v West Brom
Reading v Swansea
Sunderland v Man City
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Aston Villa v Tottenham
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Stoke v Liverpool

DIEGO MARADONA AKANWA NA CHAMA CHA SOKA CHA IRAQ - WASEMA HAWANA MPANGO WA KUMUAJIRI




 

Kufuatia ripoti zilizotoka kwamba Diego Maradona alikuwa akikaribia kuwa kocha wa timu ya taifa ya Iraq, chama cha soka cha nchi hiyo kimesema jambo hilo halitotokea kabisa.
Kutoka The National:

"Hakuna mazungumzo yoyote kati ya chama cha soka cha Iraq na Diego Maradona na hakuna nia ya kumuajiri kocha huyo," makamu wa mwenyekiti wa IFA Abdul-Khaliq Masoud alisema jana.
Kukataliwa huku kumekuja siku baada ya afisa mmoja wa shirikisho la soka la Argentina kukaririwa akisema kwamba Maradona ndio anayeoongoza katika mbio za kumrithi Zico, kocha wa zamani wa Iraq, ambao wapo katika nafasi nzuri ya kufika katika fainali za kombe la dunia 2014.

HIVI NDIVYO STARS ILIVYOMUADHIRI BINGWA WA AFRIKA ZAMBIA




Mchezaji wa Taifa Stars Mrisho Ngasa akishangilia na kupongezwa na wenzake mara baada ya kufunga goli la mkwanza katika mchezo huo.

 Wachezaji wa Taifa Stars wakitoka nje ya uwanja kwa mapumziko baada ya kipindi cha kwanza kuisha kwenye uwanja wa Taifa.

 Mashabiki wa timu ya Taifa Stars wakishagilia mara baada ya Mrisho Ngasa kufungo goli la kwanza dhidi ya Chipolopolo katika mchezo huo

 Kikosi cha timu ya Zambia kikiwa katika picha ya pamoja.

 Kulia ni Rais wa Chama cha Mpira wa Miguu nchini Zambia Kalusha Bwalya na mabalozi wa Zambia nchini Judith Kangoma-Kapijimpanga na Balozi Tanzania nchini Zambia Bi. Grace Mujumi ambaye alikuwa mgeni rasmi katika mchezo huo.

 Mashabiki wa timu ya taifa ya Zambia wakishangilia timu yao katika mchezo huo.

  Mashabiki wa Stars wakishangilia timu yao dhidi ya Zambia














Makocha wa Zambia wakitoka uwanjani baada ya mechi kuisha
 
Mcha akiwapeleka puta mabeki wa Zambia





 

TAIFA STARS YAIPOPOA CHIPOLOPOLO 1-0!!

MABINGWA AFRIKA ZAMBIA HOI UWANJA wa TAIFA!!
NGASSA ni ‘KISIRANI’ BALAA!

MRISHO_NGASATimu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, leo imetoa burudani safi na zawadi safi ya Krismasi na Mwaka mpya kwa Watanzania kwa kuwalaza Mabingwa wa Afrika Zambia, maarufu kama Chipolopolo, kwa Bao 1-0 kwenye Mechi ya Kirafiki ya Kimataifa iliyochezwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.

Bao la ushindi lilifungwa na Mrisho Ngassa katika Dakika ya 44 baada ya kupokea krosi safi kutoka kwa Mwinyi Kazimoto.

Kwa ujumla, Taifa Stars, wanaofundishwa na Kim Poulsen, walicheza vizuri sana na uwezo wa kuongeza Mabao mengine ulikuwepo.

Zambia, chini ya Kocha Bora Afrika Herve Renard, Kipindi cha Pili, waliongeza kasi na Mashambulizi lakini Stars walisimama imara na kusafisha hatari zote huku Kipa Juma Kaseja akiwa nguzo imara.

VIKOSI VILIVYOANZA:

TAIFA STARS: Juma Kaseja, Erasto Nyoni, Shomari Kapombe, Aggrey Morris, Kevin Yondan, Frank Domayo, Salum Abubakar, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba, Mrisho Ngassa, Khamis Mcha

ZAMBIA: Danny Munyao, Chintu Kampamba, Hichani Himonde, Chisamba Lungu, James Chamanga, Moses Phiri, Christopher Katongo, Felix Katongo, Nathan Sinkala, Rodrick Kabwe, Isaac Chansa.

COASTAL UNION WAIGONGA SIMBA - KUCHEZA FAINALI YA UHAI CUP NA AZAM FC



Azam ya Dar es Salaam na Coastal Union ya Tanga ndizo zitakazoumana kwenye fainali ya michuano ya Kombe la Uhai 2012 itakayochezwa kesho jioni (Desemba 23 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam.
Timu hizo zimepata fursa hiyo baada ya kushinda mechi zao za nusu fainali ya michuano hiyo inayoshirikisha timu za vijana wenye umri chini ya miaka 20 za klabu za Ligi Kuu ya Vodacom. Michuano hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya Said Salim Bakhresa kupitia maji Uhai.
Azam ndiyo iliyokuwa ya kwanza kupata tiketi ya fainali baada ya kuitoa Mtibwa Sugar ya Morogoro kwa mikwaju ya penalti 3-2. Matokeo ya dakika 90 yalikuwa bao 1-1. Nayo Coastal Union iliivua ubingwa Simba kwa kuifunga mabao 2-1.
Mechi ya fainali itaanza saa 10 kamili jioni, na itatanguliwa na ile ya kutafuta mshindi wa tatu kati ya Mtibwa Sugar na Simba ambayo itachezwa saa 2 kamili asubuhi kwenye uwanja huo huo.
Mbali ya kombe, bingwa wa michuano hiyo atapata sh. milioni 1.5, makamu bingwa sh. milioni 1 wakati mshindi wa tatu atajinyakulia sh. 500,000. Timu iliyoonesha zaidi mchezo wa kiungwana (fair play) itapata sh. 400,000, mchezaji bora wa mashindano sh. 350,000, mfungaji bora sh. 300,000 na kipa bora sh. 300,000.
Naye kocha bora katika mashindano hayo atazawadiwa sh. 300,000 kama itakavyokuwa kwa refa bora.

MKE WA SNEIJDER ASEMA "TUNAONDOKA MILAN MWEZI JANUARY"

Mke wa Wesley Sneijder amesema kwamba mumewe ataondoka Inter wakati dirisha la usajili la mwezi January.

"Tunakaribia kuondoka Milan," Yolanthe Cabau aliviambia vyombo vya habari vya Uholanzi. "Kila kitakuwa kimewekwa vizuri katika siku za mwanzo za mwezi January.

"Tutakapohamia? Tunaangalia mahala pazuri kwa ajili ya familia yetu. Kwa sasa hivi sijali sana kuhsu kazi yangu."

Sneijder amekuwa kwenye kutokuelewana na Inter katika siku za hivi karibuni baada ya kukataa ombi lao kwa mchezaji apunguze kiasi cha €2m kutoka kwenye mshahara wake.

Hajaichezea timu hiyo ya Serie A tangu alipocheza dhidi Chievo, kwanza kwa sababu ya majeruhi na baadae kwa sababu za kiufundi za boss Andrea Stramaccioni.

Sneijder aliruhusiwa kuanza mapumziko yake ya Christmas mapema wiki hii pamoja na kwamba Inter bado wana mechi mbili  za kucheza.

ROONEY KAMA BECKHAM: MKEWE ATANGAZA JINSIA YA MTOTO WAO ANAYETARAJIWA KUZALIWA MAY 2013

Tayari wameshafanikiwa kuwa na mtoto wa kiume katika familia yao, lakini kama vile haitoshi Collen na Wayne Rooney wanategemea kumkaribisha dume lingine katika familia yao hvi karibuni.

Coolen, 27, ambaye ni mjamzito wa mtoto wake wa pili, alitangaza jinsia ya mtoto wake aliye tumboni kwenye mtandao wa kijamii wa Twiter na akasema mshambuliaji wa United, Rooney amezipokea taarifa hizo kwa furaha kubwa.

Aliandika hivi kwenye akaunti yake ya Twiiter
 
Coleen na Wayne tayari ni wazazi wa Kai, na sasa wanategemea kuongeza kidume kingine ndani ya nyumba mnamo mwezi wa tano mwakani.  

RONALDO "SITOSHANGILIA GOLI ENDAPO NITAFUNGA DHIDI YA UNITED"

Mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo amesisitiza kwamba hatoweza kushangilia ikiwa atafunga katika hatua ya 16 ya UEFA Champions league dhidi ya Manchester United.

 Nahodha huyo wa Ureno ambaye alicheza kwa mafanikio makubwa akiwa na United katika kipindi cha miaka 6 kabla ya kuondoka na kujiunga Los Blancos katika kipindi cha kiangazi mwaka 2009 kwa ada iliyovunja rekodi ya dunia ya £80 million.

"Sitoshangilia goli nikiweza kufunga dhidi ya Man United," Ronaldo alikaririwa akisema siku ya alhamisi na mtandao wa AS.


Ronaldo, 27, hivi karibuni alielezea hisia zake juu ya kocha wa Manchester United na kusema kocha huyo raia wa Scotland amecheza part kubwa katika kumfanya mchezaji ambaye alivyo sasa.

"Ferguson ni mtu mzuri sana. Mwanadamu mwema. Amenifundisha vitu vingi," Ronaldo aliiambia The Sun.


"Kama nilivyosema huko nyuma, Fergie ni kama baba yangu kwenye soka. Nammisi sana yeye na mahusiano tuliyokuwa nayo."

LEO TAIFA STARS V CHIPOLOPOLO

KATONGOTimu za Taifa za Tanzania, Taifa Stars, na Zambia, Chipolopolo, ambao ndio Mabingwa wa Afrika, leo kuanzia Saa 10 Jioni zitashuka Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam kucheza Mechi ya Kimataifa ya Kirafiki.
Mara ya mwisho Timu hizi kukutana ilikuwa ni Mwaka 2010 kwenye Mechi ya ufunguzi ya Chalenji Cup na Chipolopolo kushinda Bao 1-0.
Leo, Chipolopolo, wataongozwa na Nahodha wao Christopher Katongo, ambae juzi alitunukiwa Tuzo ya Mchezaji Bora wa Afrika na BBC, Shirika la Utangazaji la Uingereza.
Stars, ambao wako chini ya Kocha toka Denmark, Kim Poulsen, wataingia kwenye Mechi hii bila ya Wachezaji wao wawili wanaocheza huko TP Mazembe, Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu ambao wameripotiwa kuwepo Dar es Salaam lakini ni majeruhi.
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
AFCON 2013
MAKUNDI:
KUNDI A: South Africa, Cape Verde, Morocco, Angola
KUNDI B: Ghana, DR Congo, Niger, Mali
KUNDI C: Zambia, Ethiopia, Nigeria, Burkina Faso
KUNDI D: Ivory Coast, Togo, Tunisia, Algeria
+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
Chipolopolo leo wataongezewa nguvu baada ya kuwasili kwa Kocha wao Mkuu Herve Renard ambae alikuwa Accra, Ghana akipokea TuzoTAIFA_STARS-small toka CAF ya kuwa Kocha Bora wa Afrika ambako pia Zambia ilitajwa kuwa ndio Timu Bora Afrika kwa 2012 baada ya kutwaa Ubingwa wa Afrka, AFCON 2012, huko Gabon Mwezi Februari Mwaka huu.
Mwezi Januari, Chipolopolo watakuwa huko Afrika Kusini kuanza utetezi wa Ubingwa wao wa Afrika kwenye michuano ya Kombe la Mataifa Afrika, AFCON 2013, itakayochezwa kuanzia Januari 19 HADI Februari 10.
Taifa Stars wao wapo kwenye vinyang’anyiro vya Mechi za Mchujo za CHAN, Kombe la Mataifa ya Afrika kwa Wachezaji wa ndani wa Afrika, na Kombe la Dunia la 2014, na Mechi hizo watazicheza Mwakani.
Viingilio katika mechi hiyo vitakuwa Sh. 5,000 kwa viti vya rangi ya bluu na kijani, Sh. 7,000 kwa viti vya rangi ya chungwa, Sh. 10,000 kwa VIP C, Sh. 20,000 kwa VIP B wakati VIP A itakuwa Sh. 30,000.
Tiketi zilianza kuuzwa tangu jana kwenye vituo vya Shule ya Sekondari Benjamin Mkapa, Uwanja wa Uhuru, Mgahawa wa Steers ulioko Mtaa wa Ohio na Samora, Sokoni Kariakoo, kituo cha mafuta cha Ubungo OilCom na Dar Live Mbagala.

Friday, December 21, 2012

EUROPA LIGI: DROO RAUNDI YA TIMU 32 HIYOOO!

EUROPA_LIGI_CUP>>MABINGWA wa ULAYA Chelsea v SPARTA PRAGUE!!
>> ZENIT V LIVERPOOL, NEWCASTLE V METALIST KHARKIV, SPURS V LYON
DROO ya Mechi za EUROPA LIGI kwa Raundi ya Mtoano ya Timu 32 imefanyika leo huko Nyon, Uswisi na sambamba na hiyo kila Timu inajua ikifuzu Raundi hiyo na kuingia Raundi ya Mtoano ya Timu 16 nani watakuwa Wapinzani.
DROO KAMILI:
RAUNDI ya MTOANO TIMU 32:
BATE Borisov v Fenerbache
Inter Milan v Cluj
Levante v Olympiakos
Zenit St Petersburg v Liverpool
Dynamo Kiev v Bordeaux
Bayer Leverkusen v Benfica
Newcastle v Metalist Kharkiv
Stuttgart v Genk
Atletico Madrid v Rubin Kazan
Ajax v Steaua Bucharest
Basel v Dnipro
Anzhi Makhachkala v Hannover
Sparta Prague v Chelsea
Borussia Monchengladbach v Lazio
Tottenham v Lyon
Napoli v Viktoria Plzen
RATIBA ya MECHI:
Mechi ya 1=14 Februari 2013
Mechi ya 1=21 Februari 2013
RAUNDI ya MTOANO TIMU 16:
Napoli au Viktoria Plzen v BATE Borisov au Fenerbache
Leverkusen au Benfica v Dynamo Kiev au Bordeaux
Anzhi Makhachkala au Hannover v Newcastle au Metalist
Stuttgart au Genk v Monchengladbach au Lazio
Tottenham au Lyon v Inter Milan au Cluj
Levante au Olympiakos v Atletico Madrid au Rubin Kazan
Basel au Dnipro v Zenit St Petersburg au Liverpool
Ajax au Steaua Bucharest v Sparta Prague au Chelsea
RATIBA ya MECHI:
Mechi ya 1=7 Machi 2013
Mechi ya 2=14 Machi 2013
+++++++++++++++++++
RATIBA HATUA YA MTOANO
RAUNDI YA TIMU 32:
Mechi ya 1=14 Februari 2013
Mechi ya 1=21 Februari 2013
RAUNDI YA TIMU 16:
Mechi ya 1=7 Machi 2013
Mechi ya 2=14 Machi 2013
ROBO FAINALI:
Mechi ya 1=4 Aprili 2013
Mechi ya 2=11 Aprili 2013
NUSU FAINALI
Mechi ya 1=25 Aprili 2013
Mechi ya 2=2 Mei 2013
FAINALI
15 Mei 2013
UWANJA wa AMSTERDAM ARENA

UEFA CHAMPIONZ LIGI: BAADA ya DROO, NINI WAMESEMA!!

>>RATIBA KAMILI YATOKA!!
>>REAL v MAN UNITED ni FEBRUARI 13
>> FERGIE: ‘NDIO BIGI MECHI RAUNDI YA TIMU 16!!’
+++++++++++++++++++
RATIBA:
[Mechi zote kuanza Saa 4 Dak 45 Usiku]
Jumanne 12  Februari 2013
Celtic v Juventus
Valencia v Paris St Germain
Jumatano 13  Februari 2013
Real Madrid v Manchester United
Shakhtar Donetsk v Borussia Dortmund
Jumanne 19  Februari 2013
Arsenal v Bayern Munich
FC Porto v Malaga
Jumatano 20  Februari 2013
Galatasaray v FC Schalke
AC Milan v Barcelona
Jumanne 5 Machi 2013
Borussia Dortmund v Shakhtar Donetsk
Man United v Real Madrid
Jumatano 6 Machi 2013
Juventus v Celtic
Paris St George v Valencia
Jumanne 12 Machi 2013
Barcelona v AC Milan
Schalke v Galatasaray
Jumatano 13 Machi 2013
Bayern Munich v Arsenal
Malaga v FC Porto
+++++++++++++++++++
FERGIE_n_MOURINHOMara baada ya kumalizika kwa Droo ya kupanga Mechi za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya UEFA CHAMPIONZ LIGI hapo jana huko Nyon, Uswisi, Wadau mbalimbali waliibuka kutoa maoni yao kuhusu Ratiba hiyo na Meneja wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, alisema pambano la Real Madrid na Manchester United ndio ‘mpambano’ wa Raundi hiyo.
Real Madrid na Manchester United hawajakutana kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI tangu Robo Fainali ya Mwaka 2003 ambayo Real walishinda kwa jumla ya Mabao 6-5 baada ya kushinda Mechi ya kwanza 3-1 huko Santiago Bernabeu na kufungwa 4-3 Uwanjani Old Trafford huku Ronaldo de Lima akipiga Hetitriki.
Mbali ya pambano kuwa zito, Mechi hii itakuwa na mvuto kwani Cristiano Ronaldo atarudi Old Trafford kwa mara ya kwanza tangu aihame Man United na kwenda Real Madrid Juni 2009 kwa Dau la Pauni Milioni 80.
Mara ya mwisho kwa Sir Alex Ferguson kumvaa Jose Mourinho ilikuwa kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI Mwaka 2009 wakati Man United ilipoibwaga Inter Milan kwenye Robo Fainali baada ya kutoka 0-0 na kuifunga 2-0 Old Trafford kwa Bao za Vidic na Ronaldo.
Ferguson amesema: “Ni nafasi nzuri kwa Mashabiki wetu kumuona Ronaldo tena na mimi kukutana na Jose-itabidi niagize Mvinyo safi!”
+++++++++++++++++++
Man United v Real Madrid
-1957: European Cup-Nusu Fainali: Real washinda 3-1Madrid, sare 2-2 na Real kushinda Jumla ya Bao 5-3
-1968: European Cup-Nusu Fainali: Man United washinda 1-0 Old Trafford, sare 3-3 ugenini na Man United washindi Jumla ya Bao 4-3
-2000: European Cup-Robo Fainali: Sare 0-0 huko Bernabeu, Man United wafungwa 3-2 nyumbani
-2003: European Cup-Robo Fainali: Real washinda 3-1 nyumbani, Man United washinda 4-3 nyumbani, Real wapita Jumla ya Mabao 6-5.
+++++++++++++++++++
YAFUATAYO ni NINI KILISEMWA KUTOKA KWA WADAU MBALIMBALI:
Real Madrid
Mkurugenzi wa Real Madrid, Emilio Butragueno, aliewahi kuwa Straika wao zamani:  "Tungependa kucheza na Man United baadae lakini hata wao hawakufurahia!"
Barcelona
Makamu wa Rais wa Barcelona, Josep Maria Bartomeu "AC Milan ni Klabu kubwa Ulaya, inaheshimika. Kwa sasa hawachezi vizuri lakini mpira hubadilika Siku hadi Siku."
Bayern Munich
Mwenyekiti wa Bayern Karl-Heinz Rummenigge "Tunaijua Arsenal vizuril. Tunaridhika na Droo hii lakini hatuwadharau!"
Paris St Germain
Mkurugenzi wa Soka, Leonardo: "Siku zote ni ngumu kusema ni Droo nzuri au siyo!"
Valencia
Mkurgenzi wa Valencia, Fernando Giner: "Kama tumefika hapa basi sisi ni moja ya Timu Bora 16 Ulaya!"

BPL: KURINDIMA WIKIENDI, ARSENAL KUANZISHA DW STADIUM!

TIMU ZASAKA USHINDI KABLA MECHI MFULULIZO X-MASI, MWAKA MPYA!
+++++++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumamosi 22 Desemba 2012
[SAA 9 Dak 45 Mchana]
Wigan v Arsenal
[SAA 12 Jioni]
Man City v Reading
Newcastle v QPR
Southampton v Sunderland
Tottenham v Stoke
West Brom v Norwich
West Ham v Everton
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Liverpool v Fulham
Jumapili 23 Desemba 2012
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Swansea v Man United
[SAA 1 Usiku]
Chelsea v Aston Villa
+++++++++++++++++++++++
AMESHATAMKA kuwa zawadi yake bora kwa Krismasi ni kubakia Pointi 6 mbele kileleni mwa Ligi Kuu England wakielekea kwenye Mechi mfululizo za wakati wa Krismasi na Mwaka mpya na Sir Alex Ferguson ataisafirisha Timu yake Manchester United kwenda huko Wales kucheza na Swansea City hapo Jumapili kulinda pengo hilo.
Lakini Ratiba ya Mechi za Ligi itaanza Jumamosi kwa Arsenal kucheza ugenini DW Stadium na Wigan na baadae Siku hiyo zitafuata Mechi 7 ikiwemo ya Mabingwa watetezi Man City kucheza kwao Etihad na Timu ya mkiani Readimg
+++++++++++++++++++++++++++
MSIMAMO:
=Tofauti ya Magoli inatajwa kwa Timu zilizofungana Pointi
1 Man United Mechi 17 Pointi 42
2 Man City Mechi 17 Pointi 36
3 Chelsea 29 [Tofauti ya Magoli 11]
4 Tottenham Mechi 17 Pointi 29 [Tofauti ya Magoli 5]
===============
5 Arsenal Mechi 17 Pointi 27 [Tofauti ya Magoli 13]
6 Everton Mechi 17 Pointi 27 [Tofauti ya Magoli 7]
7 WBA Mechi 17 Pointi 27 [Tofauti ya Magoli 3]
8 Norwich Mechi 17 Pointi 25
9 Stoke Mechi 17 Pointi 24 [Tofauti ya Magoli 2]
10 Swansea Mechi 17 Pointi 23 [Tofauti ya Magoli 4]
11 West Ham Mechi 17 Pointi 23 [Tofauti ya Magoli 1]
12 Liverpool Mechi 17 Pointi 22
13 Fulham Mechi 17 Pointi 20
14 Aston Villa Mechi 17 Pointi 18
15 Newcastle Mechi 17 Pointi 17
16 Sunderland Mechi 17 Pointi 16
17 Southampton 15 [Tofauti ya Magoli -10]
===============
18 Wigan Mechi 17 Pointi 15 [Tofauti ya Magoli -14]
19 QPR Mechi 17 Pointi 10
20 Reading Mechi 17 Pointi 9
+++++++++++++++++++++++
BPL_LOGOMechi ya mwisho Jumamosi ni ile ya Anfield kati ya Liverpool na Fulham.
Jumapili zipo Mechi mbili kati ya Swansea na Man United na Chelsea v Aston Villa.
Vinara Man United wapo kileleni Pointi 6 mbele baada ya kushinda Mechi zao 10 kati ya 11 walizocheza mwisho lakini Man City, kwa vile wanacheza Jumamosi Uwanjani kwao Etihad kabla ya Man United wanaocheza Jumapili, wakishinda wanaweza kukata pengo hilo na kuwa Pointi 3.
Man City watakuwa nyumbani kwao kwa mara ya kwanza tangu wafungwe hapo na Man United Desemba 9 Bao 3-2 na kupoteza Rekodi yao ya kutofungwa nyumbani kwa Miaka miwili na pia kutofungwa kwenye Ligi Msimu huu lakini huenda safari hii wakapata ubwete maana Reading wako mkiani na wamefungwa Mechi 6 mfululizo.
Arsenal, baada ya kuishindilia Reading, wamepaa na kukamata nafasi ya 5 na wako ugenini kucheza na Wigan ambayo imevutwa chini na kuwa moja ya Timu 3 za mkiani baada ya kufungwa Mechi 3 na sare moja katika Mechi zao 4 za mwisho.
Baada ya kuchapwa kwao Anfield na Aston Villa katika Mechi yao ya mwisho, bila shaka Meneja wa Liverpool, Brendan Rodgers, atawashikia bakora Wachezaji wake wasifungwe na Fulham, ambao hata hivyo, hawana rekodi nzuri Uwanjani Anfield, na wameshinda Mechi moja tu kati ya 9 walizocheza mwisho.
Newcastle wapo nyumbani St James Park lakini, baada ya kuanza vyema, wameporomoka hadi nafasi ya 15 wakiwa na Pointi 17 kwa Mechi 17 na wanacheza na QPR ambayo juzi ndio iliambua ushindi wao wa kwanza Msimu huu chini ya Meneja wao mpya Harry Redknapp ambae itakuwa Mechi yake ya 5 baada ya kwenda sare 3 na kushinda hiyo moja majuzi walipoifunga Fulham 2-1.
Tottenham wapo nafasi ya 4 baada ya kushinda Mechi zao 4 kati ya 5 walizocheza mwisho na safari hii wapo nyumbani White Hart Lane kucheza na Stoke City ambao hawajafungwa kati Mechi zao 7 za mwisho.
Sare 8 kati ya Mechi 11 zimewafanya Everton waporomoke toka nusu ya juu ya Msimamo wa Ligi lakini, hata hivyo, wapo Pointi mbili tu nyuma ya Tottenham ambao wamekamata nafasi ya 4 lakini watakuwa Upton Park kucheza na West Ham ambayo haina masihara wakiwa Uwanjani kwao.
WBA wanacheza na Norwich na Timu zote hizi zimeonyesha Soka safi sana.
Mechi nyingine ya msisimko ni ile kati ya Timu zinazosuasua Southampton na Sunderland na ushindi ni muhimu kwa kila Timu.
+++++++++++++++++++++++++++
RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumatano 26 Desemba 2012
[SAA 12 Jioni]
Arsenal v West Ham
Everton v Wigan
Fulham v Southampton
Man United v Newcastle
Norwich v Chelsea
QPR v West Brom
Reading v Swansea
Sunderland v Man City
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Aston Villa v Tottenham
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Stoke v Liverpool

MAKOCHA STARS, POULSEN, NA RENARD, CHIPOLOPOLO, KUONGEA!!

 TFF_LOGO12
MKUTANO MKUU TFF FEBRUARI 23 & 24, 2013
UHAI CUP-NUSU FAINALI KUPIGWA KARUME
TAARIFA KAMILI:
Release No. 199
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Desemba 20, 2012
KIM, RENARD KUWAKABILI WAANDISHI KESHO
Makocha wa Tanzania (Taifa Stars), Kim Poulsen na Zambia (Chipolopolo) watakuwa na mkutano na waandishi wa habari utakaofanyika kesho (Desemba 21 mwaka huu) kuzungumzia pambano lao litakalochezwa Jumamosi (Desemba 22 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mkutano huo utafanyika saa 5 asubuhi kwenye ukumbi wa mikutano wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF). Makocha hao watazungumzia maandalizi yao ya mwisho kabla ya pambano hilo litakalochezeshwa na mwamuzi Sylvester Kirwa kuanzia saa 10 kamili jioni.
Pia makocha hao watajibu maswali kutoka kwa waandishi wa habari kuhusu pambano hilo litakalokutanisha timu hizo ambazo zimefanya vizuri kwenye orodha ya viwango vya ubora vya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) vilivyotolewa jana (Desemba 19 mwaka huu).
Wakati Zambia ambao ni mabingwa wa Afrika wamepanda juu kwa viwango vya ubora kwa nafasi nne, Taifa Stars ambayo katika mchezo uliopita iliifunga Kenya (Harambee Stars) bao 1-0 imepanda kwa nafasi nne.
Taifa Stars ambayo inadhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iko kambini tangu Desemba 12 mwaka huu kujiandaa kwa mechi hiyo kubwa ya kirafiki inayotarajiwa kuwa ya kuvutia.
TENGA ATOA NOTISI YA MKUTANO MKUU TFF
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Leodegar Tenga ambaye ndiye Mwenyekiti wa Mkutano Mkuu wa Shirikisho hilo tayari ametoa notisi ya mkutano huo utakaofanyika Februari 23 na 24 mwakani jijini Dar es Salaam.
Mkutano huo utafanyika Februari 23 mwakani na kufuatiwa na ajenda ya uchaguzi siku inayofuata. Ajenda ya uchaguzi iko chini ya Kamati ya Uchaguzi ya TFF.
Notisi hiyo imetumwa kwa wajumbe wa Mkutano Mkuu ambao ni kutoka vyama vya mpira wa miguu vya mikoa, vyama shiriki, klabu za Ligi Kuu ya Vodacom na wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF.
Ajenda za Mkutano Mkuu zitatumwa kwa wajumbe siku 15 kabla ya mkutano huo wenye wajumbe zaidi ya 100.
NUSU FAINALI UHAI CUP KUPIGWA KARUME
Mechi za nusu fainali ya michuano ya Kombe la Uhai 2012 inayoshirikisha timu za vijana wenye umri chini ya miaka 20 za klabu za Ligi Kuu ya Vodacom zitachezwa kesho (Desemba 21 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam.
Nusu fainali ya kwanza ya michuano hiyo inayodhaminiwa na kampuni ya Said Salim Bakhresa kupitia maji Uhai itazikutanisha timu za Mtibwa Sugar ya Morogoro na Azam na itafanyika kuanzia saa 2 kamili asubuhi.
Simba na Coastal Union zitacheza nusu fainali ya pili kuanzia saa 10 kamili jioni kwenye uwanja huo huo. Mtibwa Sugar imepata tiketi ya nusu fainali baada ya kuichapa African Lyon mabao 3-1 wakati Simba iliilaza Oljoro JKT mabao 2-0.
Nayo Azam iliindoa JKT Ruvu kwenye robo fainali kwa bao 1-0 huku Coastal Union ikipata ushindi wa penalti 4-3 dhidi ya Ruvu Shooting kwenye mechi ya mwisho ya robo fainali.
Mechi ya fainali na ile ya kutafuta mshindi wa tatu zitachezwa Jumapili (Desemba 23 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam. Mechi ya mshindi wa tatu itaanza saa 2 kamili asubuhi wakati ya fainali itakuwa saa 10 kamili jioni.
PONGEZI KWA UONGOZI MPYA TWFA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linaupongeza uongozi mpya wa Chama cha Mpira wa Miguu wa Wanawake Tanzania (TWFA) uliochaguliwa katika uchaguzi uliofanyika jana (Desemba 19 mwaka huu) hoteli ya Midlands mjini Morogoro.
Ushindi aliopata Lina Kessy aliyechaguliwa tena kuwa Mwenyekiti pamoja na wajumbe wengine wa Kamati ya Utendaji unaonesha jinsi ambavyo wajumbe wa Mkutano Mkuu wa TWFA walivyo na imani kwao.
TFF inaahidi kuendeleza ushirikiano wake kwa Kamati ya Utendaji ya TWFA, na kwamba ina changamoto kubwa ya kuhakikisha inaendesha shughuli za chama hicho kwa kuzingatia katiba na kanuni.
Pia tunatoa pongezi kwa Kamati ya Uchaguzi ya TWFA chini ya Mama Ombeni Zavala na Kamati ya Uchaguzi ya TFF inayoongozwa na Deogratias Lyatto kwa kuhakikisha uchaguzi huo unafanyika kwa utulivu na kwa kuzingatia Katiba ya TWFA na Kanuni za Uchaguzi za Wanachama wa TFF.
Safu mpya ya uongozi wa DRFA inaundwa na Lina Kessy (Mwenyekiti), Rose Kissiwa (Makamu Mwenyekiti), Amina Karuma (Katibu), Zena Chande (Mwakilishi wa Mkutano Mkuu wa TFF) wakati mjumbe wa Kamati ya Utendaji ni Triphonia Temba.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)