Thursday, May 9, 2013

RIO FERDINAND, CARRICK WAMKARIBISHA DAVID MOYES MAN UNITED. . .

MWENYEKITI EVERTON KENWRIGHT AHUZUNIKA: “NI MENEJA BORA! MAN UNITED WANA BAHATI!

DAVID_MOYES WAKATI Wachezaji wa Manchester United, Rio Ferdinand na Michael Carrick, wakichekelea na uteuzi wa Meneja mpya David Moyes na kumkaribisha kwa furaha, Mwenyekiti wa Everton, Bill Kenwright, amesikitishwa na kuondoka kwake na kusema Man United wamebahatika sana kumpata.
Jumatano, Sir Alex Ferguson alitangaza kustaafu kuwa Meneja na leo Man United imemtangaza Mrithi wake kuwa ni David Moyes, Mtu ambae alipendekezwa na Sir Alex Ferguson mwenyewe.MOYES_n_FERGIE-POA
David Moyes amepewa Mkataba wa Miaka 6 na Man United ambao utaanza rasmi Julai 1.
Moyes, ambae Mkataba wake na Everton unamalizika Juni 30, ataisimamia Everton katika Mechi zake 2 zilizobakia za BPL, Barclays Premier League, ambazo watacheza na West Ham na kumaliza na Chelsea hapo Mei 19 Uwanjani Stamford Bridge.
Rio Ferdinand, ambae amecheza chini ya Ferguson kwa Miaka 10 huko Old Trafford, amesema: "Ilikuwa ni muhimu kwa Klabu kufanya uamuzi wa haraka kabla Watu hawajaanza kuleta uvumi. Hatujawahi kuwa na tatizo nae na Watu wanaomjua wanasema ni Mtu mwema aliefanya kazi nzuri huko Everton.”
Nae Michael Carrick amesema anachojua yeye ni kuwa Moyes ni mkweli kwa Wachezaji wake na Mchapa kazi aliefanya kazi njema Everton.

Mwenyekiti Everton- Bill Kenwright
Mwenyekiti wa Everton Bill Kenwright amemsifia Meneja wake David Moyes ambae anaondoka na kuanza kazi ya Umeneja huko Man United kuanzia Julai 1.
Kenwright, ambae ndie alimwingiza Moyes Goodison Park kutoka Preston North End Mwezi Machi 2002, amesema amehuzunishwa na kuondoka kwake.
Ametamka: “Huyu ni Meneja Bora na Man United wana bahati sana kumpata! Everton yote itahuzunika kuagana nae, ni Meneja Bora! Hatukuweza kumzuia Mkataba wake unakwisha na yeye kaamua kwenda Man United! Huwezi kumzuia!”
Licha ya kutofanikiwa kuchukua Kombe lolote akiwa na Everton kwa Miaka yake 11 aliyokuwa hapo kitu pekee na kikubwa kilichompa umaarufu ni kuiongoza Klabu masikini, isiyokuwa na Fedha kununua Wachezaji wakubwa, kubakia BPL na kuweza kushindana kiume na Klabu kubwa na Tajiri.


-ALIANZA kucheza Soka na  Celtic na kumalizia Preston ambako alicheza na Chipukizi David Beckham aliepelekwa hapo kwa mkopo na Man United kati ya Februari na Machi 1995
-BAADA ya kuifikisha Preston kwenye Fainali ya Mechi za Mchujo wa Daraja la Kwanza, Moyes akahamia Everton kama Meneja kumrithi Walter Smith hapo Machi 2002
-ALIMPA Wayne Rooney nafasi ya kucheza Mechi ya kwanza kwenye Ligi Agosti 2002 na kumuuza Man United Miaka miwili baadae kwa Pauni Milioni 20.
-ALIIFIKISHA Everton nafasi ya 4 kwenye Ligi Kuu Mwaka 2005 na kucheza UEFA CHAMPIONZ LIGI
-ALIIPELEKA Everton Fainali ya FA CUP Mwaka 2009 walipofungwa 2-1 na Chelsea baada ya kuitoa Man United kwenye Nusu Fainali

No comments:

Post a Comment