JUMAMOSI JUNI 8, MOROCCO v TAIFA STARS [SAA 5 USIKU]
SAMATTA & ULIMWENGU KUJIUNGA NA KIKOSI LEO!!
PATA HABARI KAMILI:
Taifa Stars imewasili hapa Marrakech,
Morocco leo- Juni 3 mwaka huu tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe la
Dunia dhidi ya wenyeji Morocco itakayochezwa Jumamosi- Juni 8 mwaka huu.
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro
Premium Lager imefikia hoteli ya Pullman ambayo pia Ivory Coast ilifikia
ilipokuja kucheza hapa dhidi ya Morocco. Stars imetua na wachezaji 21
huku Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu waliokuwa Maputo, Msumbiji kwenye
mechi ya Kombe la Shirikisho na timu yao ya TP Mazembe watawasili
kesho- Juni 4 mwaka huu saa 8 mchana.
Mechi kati ya Stars na Morocco itachezwa kuanzia saa 3 usiku kwa saa za hapa wakati nyumbani itakuwa ni saa 5 usiku.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
Marrakech, Morocco
No comments:
Post a Comment