Saturday, September 21, 2013

DABI YA MANCHESTER: CITY v MAN UNITED, NI DABI YA 166!

UWANJA: Etihad SIKU: Jumapili Septemba 22 SAA 12 Jioni
 
DERBY_OF_MANCHESTER-2JUMAPILI, Jiji la Manchester litarindima kwa pande zake mbili, ile ya Kibuluu na ile Nyekundu, kukutana Uwanja wa Etihad kwa ajili ya Dabi ya 166 wakati Manchester City itakapowakaribisha Mahasimu wao Mabingwa Manchester United kwenye Mechi ya Ligi Kuu England huku Timu zote zikiwa na Mameneja wapya kwa Msimu huu.

Man City wanae Manuel Pellegrini na Man United wanae David Moyes.

Hali za Wachezaji

Manchester City wanaweza kuwachezesha Kiungo David Silva na Beki Micah Richards ambao wamepona maumivu yao lakini Beki Gael Clichy hatarajiwi kucheza kwa sababu hajapona vyema tatizo la Musuli za Pajani.

Manchester United wanaweza kumtumia Danny Welbeck ambae inasemekana amepata afueni tatizo la Goti lakini Phil Jones na Rafael bado hawajetengemaa maumivu yao.

++++++++++++++++++++++++++

REKODI:

MASHINDANO
MAN CITY-USHINDI
SARE
MAN UNITED-USHINDI
LIGI
40

49

59

FA CUP
3

0

6

LIGI CUP
3

1

2

NGAO YA
 JAMII
0

0

2

JUMLA

46


50


69



++++++++++++++++++++++++++

MATOKEO MECHI ZA MWISHONI:

27 Jan 2010 Manchester United 3 Manchester City 1 [Carling Cup]

17 Apr 2010 Manchester City 0 Manchester United 1 [BPL]

10 Nov 2010          Manchester City 0 Manchester United 0 [BPL]

12 Feb 2011 Manchester United 2 Manchester City 1 [BPL]

16 Apr 2011 Manchester City 1 Manchester United 0 [FA Cup]

07 Aug 2011           Manchester City 2 Manchester United 3 [NGAO YA JAMII]

23 Oct 2011 Manchester United 1 Manchester City 6 [BPL]

08 Jan 2012 Manchester City 2 Manchester United 3 [FA Cup]

30 Apr 2012 Manchester City 1 Manchester United 0 [BPL]

09 Dec 2012           Manchester City 2 Manchester United 3 [BPL]

08 Apr 2013 Manchester United 1 Manchester City 2 [BPL]

++++++++++++++++++++++++++

Tathmini

Timu zote hizi mbili, baada Mechi 4, zimefungana kwa Pointi zikiwa na Pointi 7 kila mmoja ikiwa ni Pointi 3 nyuma ya Vinara Liverpool.

Msimu huu, Man United walianza kwa kuifunga Swansea City Bao 4-1, Sare 0-0 na Chelsea, kufungwa 1-0 na Liverpool na kuichapa Crystal Palace Bao 2-0.

++++++++++++++++++++++++++

NINI WAMESEMA:

-PELLEGRINI: ‘Sijui nini kilitokea huko nyuma lakini kwa sasa najua tuna fikra zenye nguvu sawa na Man United au zaidi!’

-MOYES: ‘’Nina uzoefu wa Dabi nyingi-huko Glasgow na Merseyside. Ni muhimu sana kwa Mashabiki. Ni muhimu kwa Wachezaji lakini muhimu zaidi ni nini kitatokea mwishoni mwa Msimu na nani yuko kileleni!’

++++++++++++++++++++++++++

Man City walianza kwa kuifunga Newcastle 4-0, kufungwa 3-2 na Cardiff City, kuifunga Hull CityMAN_CITY_v_MAN_UNITED-TEAM_PITCH 2-0 na Sare ya 0-0 na Stoke City.

Nguzo muhimu kwa Man City ni Kiungo wao Yaya Toure ambae Msimu huu ameanza kwa kutawala vizuri katikati ikiwa pamoja na kufunga Bao pia likiwemo Bao kwenye Mechi ya Juzi ya UEFA CHAMPIONZ LIGI, UCL, ambayo walishinda Ugenini kwa kuichapa Viktoria Plzen Bao 3-0.

Nao Man United wamaimarisha Kiungo chao walipomsaini Marouane Fellaini Septemba 2 na bila shaka ataongeza nguvu kazi kuwakabili kina Yaya na Fernandinho.

Lakini, bila shaka, Man United nguzo zao kubwa ni Washambuliaji wao, Robin van Persie na Wayne Rooney huku Rooney akiwa juu kwa hivi sasa baada kung’ara mno kwenye Mechi ya UCL Jumanne iliyopita Man United walipoicharaza Bayer Leverkusen Bao 4-2 na Rooney kufunga Bao 2.

Hizo zilikuwa Bao zake za 199 na 200 kwa Man United na kumfanya awe wa 4 katika Listi ya Wafungaji Bora Klabuni hapo.

++++++++++++++++++++++++++

DONDOO MUHIMU:

-Rooney amefunga Bao 10 katika Dabi za Manchester sawa na Wafungaji Bora wa Dabi hii katika Historia, Francis Lee na Joe Hayes, ambao wote wanatoka Man City, na Jumapili akifunga yeye atatwaa Nambari Wani.

++++++++++++++++++++++++++

Kwa Rooney Uwanja wa Etihad humpa mafanikio kwani amefunga Bao 4 katika Mechi 3 za mwisho alizocheza na Man City.

Uso kwa Uso

-Msimu uliopita kwenye Ligi, Man United walishinda Etihad Bao 3-2 na Man City kushinda 2-1 Old Trafford.

-Katika Mechi 10 za mwisho za Ligi walizocheza kati yao, Man United wameshinda 6 na Man City 3.

-Katika Mechi 16 za Ligi Kuu ambazo Man United wamekwenda kucheza Nyumbani kwa Man City wameshinda 9, Man City 5 na Sare 2.

VIKOSI VINATARAJIWA:

MAN CITY [Mfumo: 4-2-3-1]: 

-Hart

- Zabaleta, Kompany, Nastasic, Kolarov

-Toure, Fernandinho

-Navas, Aguero, Nasri

-Dzeko

MAN UNITED [Mfumo: 4-4-2]:

-De Gea

-Smalling, Ferdinand, Vidic, Evra

-Valencia, Carrick, Fellaini, Kagawa

-Rooney, Van Persie

Refa: Howard Webb

++++++++++++++++++++++++++

LIGI KUU ENGLAND

RATIBA:

[Saa za Bongo]

Jumamosi 21 Septemba

14:45 Norwich City v Aston Villa

17:00 Liverpool v Southampton

17:00 Newcastle United v Hull City

17:00 West Bromwich Albion v Sunderland

17:00 West Ham United v Everton

19:30 Chelsea v Fulham

Jumapili 22 Septemba

15:30 Arsenal v Stoke City

15:30 Crystal Palace v Swansea City

18:00 Cardiff City v Tottenham Hotspur

18:00 Manchester City v Manchester United

++++++++++++++++++++++++++

MSIMAMO:
NA

TIMU

P

PTS


1
Liverpool
4
10

2
Arsenal
4
9

3
Tottenham
4
9

4
Man. City
4
7

5
Man. United
4
7

6
Chelsea
4
7

7
Stoke City
4
7

8
Newcastle
4
7

9
Everton
4
6

10
West Ham
4
5

11
Southampton
4
5

12
Cardiff
4
5

13
Swansea
4
4

14
Fulham
4
4

15
Norwich
4
4

16
Hull City
4
4

17
Aston Villa
4
3

18
Crystal Palace
4
3

19
WBA
4
2

20
Sunderland
4
1

No comments:

Post a Comment