Saturday, September 21, 2013

MOURINHO KWA MATA: ‘BADILIKA AU BENCHI!’, MOYES KWA ROONEY: ‘BAKI MCHEZAJI MKUBWA!’

MOYES_v_MOURINHONDIO kwanza UEFA CHAMPIONZ LIGI, UCL, imeanza kwa Klabu kubwa huko England na Ligi Kuu England ndio inaanza kupamba moto lakini Klabu kubwa huko England, Mabingwa Manchester United, na Chelsea, zimepata matokeo tofauti na kuzua mijadala huku Mameneja wao, David Moyes na Jose Mourinho, wakijitokeza na kutoa nadharia zao. 
PATA ZAIDI:

MOURINHO KWA MATA: ‘BADILIKA AU BENCHI!’

Bosi wa Chelsea Jose Mourinho amemwambia Mchezaji wakeJUAN_MATAJuan Mata ni lazima abadilike ikiwa anataka namba Chelsea.
Mata, ambae amekuwa Mchezaji Bora Chelsea kwa Misimu miwili iliyopita, amekuwa hapati namba tangu Jose Mourinho aanze kazi hapo Chelsea mwanzoni mwa Msimu.

Msimu huu amecheza Mechi 3 tu-alitolewa baada ya Dakika 65 na Aston Villa, kuchezeshwa Dakika 57 na Everton na kucheza Dakika 23 Chelsea walipofungwa 2-1 na FC Basel kwenye UCL hivi Juzi.

Mourinho ameweka bayana kuwa Nambari 10 wake ni Oscar na Mata inabidi abadili uchezaji wake ili apate namba.

Mourinho amesema: “Kuna vitu siwezi kuongea na nyinyi. Lakini alicheza na Everton tangu mwanzo na hebu chunguzeni uchezaki wake. Nataka kumjenga Oscar kama Namba 10 wangu. Nataka Wachezaji wengine wawili, kutoka Winga, wakubali hilo na kujifunza vitu ambavyo hawakuwa tayari kujifunza toka mwanzo.  ”

Mourinho alitamka: “Mata alicheza na Basel, si sawa na Ba na Mikel waliokuja kuokoa jahazi, alikuwepo Timu ikiongoza 1-0 na alikuwa na kazi maalum. Ajifunze. Kitu kimoja ni kumchezesha yeye pamoja na Ramires na Oscar, wao kuwabana Wapinzani na Mata kucheza Namba 10 nyuma ya Straika ili asaidie kutoa mchango wa Magoli kwa pasi safi, awajibike kwa sababu ana kipaji.”

Aliongeza: “Kingine ni kubadilika na kufuata uchezaji wetu sasa. Wakati huu, Oscar ndie Namba 10 wangu, na ukiniambia kuwa Oscar sie Mchezaji Bora Chelsea tangu Msimu uanze, nitakupinga!”
Mourinho amekuwa akimchezesha Eden Hazard Winga kushoto, Oscar nyuma ya Straika na kulia, kwenye Mechi na Basel, alianza Willian.

Na Mourinho amesisitiza Oscar na Mata wanaweza kucheza Timu moja lakini anataka Mata, anaetumia Mguu wa kushoto, acheze Winga ya Kulia na pia awajibike kukaba Timu inapopoteza Mpira.

MOYES KWA ROONEY: ‘BAKI MCHEZAJI MKUBWA!’

ROONEY_N_MOYESDavid Moyes amempa changamoto Straika wake Wayne Rooney ahakikishe kuwa yeye ni Mchezaji mkubwa wa Mechi kubwa huku Jumapili wakitarajiwa kusafiri kwenda Etihad kucheza na Mahasimu wao Manchester City kwenye Dabi ya Jiji la Manchester.

Rooney alisakamwa na sakata la kutaka kuhama kufuatia kauli ya Meneja Mstaafu Sir Alex Ferguson Mwezi Mei kuwa Mchezaji huyo anataka kuhama na kisha kuundamwa na kuumia lakini, hivi sasa, kwa Mechi mbili alizoanza Rooney ameonyesha yuko moto na ameshahau sakata hilo lililoleta utata.

Jumamosi iliyopita Rooney alianza Mechi na Crystal Palace na kufunga Bao na Jumanne alicheza Mechi ya UCL na Bayer Leverkusen na kufunga Bao 2.

Hivi Juzi, katika nia ya kusawazisha mambo, Sir Alex Ferguson aliibuka na kuzungumza kwa mara ya kwanza na kumsifia sana Rooney.

Sasa Moyes, ambae ndio anakumbana na Dabi yake ya kwanza kama Meneja wa Man United, amesema anaamini sasa ni wakati muafaka kwa Rooney kuonyesha cheche zake kama mmoja wa Wachezaji Bora Duniani.

Moyes ametamka: “Nadhani mtazamo wa Rooney ni kuwa yeye ni Mchezaji mkubwa wa Mechi kubwa. Anataka kuonyesha hilo kwa kila Mtu. Na Watu wanakuja Mpirani kuona Wachezaji kama yeye wakionyesha tofauti na kubadili Gemu na tunategemea atafanya hivyo. Kitu muhimu ni kuwa abakishe fomu yake. Akiendelea kucheza kama hivi, Magoli yatakuja tu!”

Rooney amefunga Bao 10 katika Dabi za Manchester sawa na Wafungaji Bora, Francis Lee na Joe Hayes, ambao wote wanatoka Man City, na Jumapili akifunga yeye atatwaa Nambari Wani.

Pia, Moyes alisema kwa Sir Alex Ferguson kuibuka na kumsifia Rooney ni jambo jema litakalosaidia sana.
Amesema: “Ukisifiwa na Mtu kama Sir Alex basi kubali. Lakini tukumbuke ni Wayne mwenyewe aliejifikisha hapa. Yeye ndie amefanya kazi ngumu.”

Aliongeza: “Ni Mwaka mkubwa kwake..Rekodi nyingi anaweza kuzipata. Ana Mwaka mkubwa kuelekea Kombe la Dunia.”

No comments:

Post a Comment