Friday, May 10, 2013
KALI YA LEO: "KAMA UNAMPENDA KOCHA WAKO USIMSAJILI CAPTAIN WA ARSENAL"
1: Viera kwenda Juventus mwaka wa pili Capelo kaondoka
2: Thierry Henry kwenda Barca msimu wa pili Frank Rijkaard kaondoka
3: William Gallas kwenda Tottenham Spurs Redknapp kaondoka
4: Cesc Fabregas kwenda Barcelona Pep Guadiola msimu wa pili akaondoka
5: Van Persie kaenda Manchester United - Sir Alex Ferguson huyoooo Je, nani atamchukua Vermerleen?
ED WOODWARD MRITHI WA DAVID GILL NDANI YA MAN UNITED - ALIYE NYUMA YA MAFANIKIO YA KIBIASHARA YA MAN UNITED CHINI YA GLAZERS!
Ni mtaalam wa zamani wa mambo ya
uwekezaji kwenye benki na mtu muhimu nyuma ya uongozi wa familia ya
Glazer, ndio yupo nyuma ya mafanikio ya kibiashara ya Manchester United.
Wakati Ed Woodward, 40, anaweza asiwe na jina kubwa, ameweza kujenga sifa wakati wa miaka yake nane ndani ya Old Trafford.
Na kipindi kijacho cha kiangazi Woodward atachukua nafasi ya ofisa mkuu wa Manchester United David Gill mbaye atastaafu.
Akiwa amehusika kwa kiasi kikubwa katika kuhakikisha familia ya Glazer inainunua klabu hiyo mwaka 2005, Woodward amekuwa mtu muhimu ndani ya klabu hiyo tangu wakati huo.
Akiwa kama msaidizi wa Gill, muingereza huyo amekuwa na jukumu la kuhakikisha mbinu za biashara za United zinakuwa bora, baada ya kuondoka kwa Gill 30 June, ataingia katika majukumu ya kisoka zaidi, yakiwemo masuala ya usajili na uhamisho pamoja majadiliano ya mishahara ya wachezaji.
Woodward anasifika sana kwa kuweza kufanikisha kupatikana kwa dili za mikataba mingi ambayo ilisababisha ongezeko kubwa la faida ndani ya miezi mitatu iliyopita - United wakitangaza faida ya £91 millioni kutoka mwezi January.
Kuanzia 2014, dili lingine kama la Chevrolet litaiwezesha United kulipwa na kampuni hiyo ya magari ya Marekani kiasi cha £51m kwa mwaka kutokana na udhamini wa jezi pekee yake.
Jukumu la kuiongoza United linaweza kuonekana kama kitu ambacho hakikutegemewa kwa mhitimu huyo wa fizikia wa Bristol University, japokuwa Woodward alianza kazi hiyo ya masuala ya uongozi huko PricewaterhouseCoopers akiwa kama mhasibu na mshauri wa masuala ya kodi mwaka 1993.
Mwaka 1999 alihamia JP Morgan, ambapo alifanya kazi kama ofisa mkuu wa masuala ya uwezekezaji katika masuala ya biashara za kimataifa.
Na mahala hapo ndipo alipokutana na Malcom Glazer n kumshauri ainunue Manchester United, na mwaka 2005 aliitwa kuajiriwa na United chini ya Glazers.
Mwanzoni alipewa jukumu la upangaji wa masuala ya fedha, kabla hajapewa jukumu la kuendesha biashara na masuala yote ya media ya Manchester United mwaka 2007 na baadae mwaka jana akawa mkurugenzi.
Woodward alikuwa hana uzoefu wowote wa kufanya kazi kwenye taasisi ya kimichezo kabla hajaja United, lakini alianza kuhudhuria vikao vya wana hisa wa premier league kwa pamoja na Gill mwaka 2012 katika jaribio la kumuongezea uelewa kuhusu siasa za soka.
Na kipindi kijacho cha kiangazi Woodward atachukua nafasi ya ofisa mkuu wa Manchester United David Gill mbaye atastaafu.
Akiwa amehusika kwa kiasi kikubwa katika kuhakikisha familia ya Glazer inainunua klabu hiyo mwaka 2005, Woodward amekuwa mtu muhimu ndani ya klabu hiyo tangu wakati huo.
Akiwa kama msaidizi wa Gill, muingereza huyo amekuwa na jukumu la kuhakikisha mbinu za biashara za United zinakuwa bora, baada ya kuondoka kwa Gill 30 June, ataingia katika majukumu ya kisoka zaidi, yakiwemo masuala ya usajili na uhamisho pamoja majadiliano ya mishahara ya wachezaji.
Woodward anasifika sana kwa kuweza kufanikisha kupatikana kwa dili za mikataba mingi ambayo ilisababisha ongezeko kubwa la faida ndani ya miezi mitatu iliyopita - United wakitangaza faida ya £91 millioni kutoka mwezi January.
Kuanzia 2014, dili lingine kama la Chevrolet litaiwezesha United kulipwa na kampuni hiyo ya magari ya Marekani kiasi cha £51m kwa mwaka kutokana na udhamini wa jezi pekee yake.
Jukumu la kuiongoza United linaweza kuonekana kama kitu ambacho hakikutegemewa kwa mhitimu huyo wa fizikia wa Bristol University, japokuwa Woodward alianza kazi hiyo ya masuala ya uongozi huko PricewaterhouseCoopers akiwa kama mhasibu na mshauri wa masuala ya kodi mwaka 1993.
Mwaka 1999 alihamia JP Morgan, ambapo alifanya kazi kama ofisa mkuu wa masuala ya uwezekezaji katika masuala ya biashara za kimataifa.
Na mahala hapo ndipo alipokutana na Malcom Glazer n kumshauri ainunue Manchester United, na mwaka 2005 aliitwa kuajiriwa na United chini ya Glazers.
Mwanzoni alipewa jukumu la upangaji wa masuala ya fedha, kabla hajapewa jukumu la kuendesha biashara na masuala yote ya media ya Manchester United mwaka 2007 na baadae mwaka jana akawa mkurugenzi.
Woodward alikuwa hana uzoefu wowote wa kufanya kazi kwenye taasisi ya kimichezo kabla hajaja United, lakini alianza kuhudhuria vikao vya wana hisa wa premier league kwa pamoja na Gill mwaka 2012 katika jaribio la kumuongezea uelewa kuhusu siasa za soka.
Jukumu lake jipya litamfanya afanye kazi kwa karibu na Sir Alex Ferguson
na mrithi wake David Moyes katika kuifanya brand ya Manchester United
inafanikiwa kibiashara na kisoka kama ilivyokuwa chini ya David Gill.
BAADA YA KUANDAMWA SANA MASHABIKI WA MAN U - MKE WA ROONEY ASEMA "MUULIZENI ROONEY MWENYEWE SIO MIMI"
Wakati Manchester United ikimtangaza
David Moyes kuwa mrithi wa Sir Alex Ferguson, hatma ya mchezaji Wayne
Rooney ndani ya Old Trafford imekuwa bado ya utata na kupelekea
mashabiki wa klabu hiyo kuwa katika hali ya wasiwasi.
Taarifa mbalimbali zimekuwa zikisema mshambuliaji huyo amepeleka maombi ya kuondoka United kwa mara ya pili ndani ya miaka 3, akisema anahitaji changamoto mpya sehemu nyingine, huku vilabu vya Chelsea, PSG na Bayern Munich vikiwa tayari kutuma ofa kwa ajili ya kumsaini Muingereza huyo.
Kutokana na sintofahamu hiyo kuhusu hatma ya Wayne Rooney ambaye sasa amebadilisha biography yake kwenye mtandao wa Twitter kutoka kuwa "mchezaji wa Manchester United mpaka kuwa NikeUK athlete" - mashabiki wa klabu wamekuwa wakimtumia tweets za vitisho na matusi kuhusu kutaka kuondoka Manchester United wakati huu timu ikiwa kwenye huzuni kubwa kwa kustaafu kwa Fergie.
Kama vile haitoshi baaada ya Wayne Rooney kukaa kimya bila kuwajibu chochote mashabiki ho kwenye Twitter wakamfuata mkewe Coleen Rooney na kuanza kumuuliza kama ni kweli wanataka kuondoka Manchester?
Mwanzoni Coleen alikaa kimya lakini baadae akashindwa kuvumilia na kuwatumia tweet moja mashabiki na kuwaambia kwamba "Mume wangu ana akaunti ya Twitter..... @WayneRooney muulizeni yeye sio mimi".
Taarifa mbalimbali zimekuwa zikisema mshambuliaji huyo amepeleka maombi ya kuondoka United kwa mara ya pili ndani ya miaka 3, akisema anahitaji changamoto mpya sehemu nyingine, huku vilabu vya Chelsea, PSG na Bayern Munich vikiwa tayari kutuma ofa kwa ajili ya kumsaini Muingereza huyo.
Kutokana na sintofahamu hiyo kuhusu hatma ya Wayne Rooney ambaye sasa amebadilisha biography yake kwenye mtandao wa Twitter kutoka kuwa "mchezaji wa Manchester United mpaka kuwa NikeUK athlete" - mashabiki wa klabu wamekuwa wakimtumia tweets za vitisho na matusi kuhusu kutaka kuondoka Manchester United wakati huu timu ikiwa kwenye huzuni kubwa kwa kustaafu kwa Fergie.
Kama vile haitoshi baaada ya Wayne Rooney kukaa kimya bila kuwajibu chochote mashabiki ho kwenye Twitter wakamfuata mkewe Coleen Rooney na kuanza kumuuliza kama ni kweli wanataka kuondoka Manchester?
Mwanzoni Coleen alikaa kimya lakini baadae akashindwa kuvumilia na kuwatumia tweet moja mashabiki na kuwaambia kwamba "Mume wangu ana akaunti ya Twitter..... @WayneRooney muulizeni yeye sio mimi".
MOYES AFUNGUKA, NI WIKI HII TU ALIJUA SAFARI OLD TRAFFORD!
ASEMA OFA YA MAN UNITED HUWEZI KUIKATAA!!
DAVID MOYES amekiri hakuwa anajua kama Sir Alex Ferguson atastaafu Manchester United na yeye kuteuliwa kuwa Meneja huko lakini alipopewa ofa hakusita hata Sekunde moja.
DAVID MOYES amekiri hakuwa anajua kama Sir Alex Ferguson atastaafu Manchester United na yeye kuteuliwa kuwa Meneja huko lakini alipopewa ofa hakusita hata Sekunde moja.
Moyes amesema hatua hii ni kama ile alipotoka Preston North End Mwaka 2002 na kutua Everton.
Ametamka: “Nasikitika kuondoka Klabu
safi kama Everton ambayo imekuwa sehemu ya maisha yangu lakini ukweli
siwezi kuikataa ofa ya Man United!”
Ingawa Mkataba wake na Everton ulikuwa
ukimalizika Juni 30, David Moyes alithibitisha hakuwa na mipango ya
kuhama na alikuwa tayari yeye na Mwenyekiti wa Everton, Bill Kenwright,
walikuwa wameshaandaa mipango ya Msimu ujao.
Moyes pia alimzungumzia Mtu
atakaemrithi, Sir Alex Ferguson, na kutamka: “Hakuna Mtu aliefikiria ipo
Siku Sir Alex Ferguson atastaafu. Tulidhani yeye ni Binadamu wa ajabu.
Yeye ni mfano kwa kila Mtu. Heshima yangu kwake haielezeki. Tumetoka
zama tofauti. Nimekua nikimwona yeye na Jock Stein ni Mashujaa, baadae
nikashindana na Sir Alex. Sina neno lolote ala kumwelezea ambalo
litamtendea haki Sir Alex Ferguson!’
Pia Moyes alizungumzia Mechi yake ya
mwisho akiwa Meneja wa Everton Uwanja wa Nyumbani Goodison Park ambako
Jumapili hii watacheza na Newcastle na kusema anatumaini Mashabiki
watatoa heshima kama ile ya Siku ya kwanza yeye kutua hapo.
Mechi ya mwisho kabisa kwa David Moyes akiwa Meneja wa Everton ni hapo Mei 19 watakapocheza ugenini Stamford Bridge na Chelsea.
BPL: BARCLAYS PREMIER LEAGUE
RATIBA
Jumamosi Mei 11
[Saa 8 Dak 45 Mchana]
Aston Villa v Chelsea
Jumapili Mei 12
[Saa 9 na Nusu Mchana]
Stoke v Tottenham
[Saa 11 Jioni]
Everton v West Ham
Fulham v Liverpool
Norwich v West Brom
QPR v Newcastle
Sunderland v Southampton
[Saa 12 Jioni]
Man United v Swansea
Jumanne Mei 14
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Arsenal v Wigan
[Saa 4 Usiku]
Reading v Man City
Jumapili 19 Mei
MECHI ZA MWISHO ZA LIGI MSIMU HUU
[Saa 12 Jioni]
Chelsea v Everton
Liverpool v QPR
Man City v Norwich
Newcastle v Arsenal
Southampton v Stoke
Swansea v Fulham
Tottenham v Sunderland
West Brom v Man United
West Ham v Reading
Wigan v Aston Villa
MSIMAMO:
FAHAMU: BINGWA TAYARI NI MANCHESTER UNITED!!
NA |
TIMU |
P |
GD |
PTS |
1 |
Man Utd |
36 |
42 |
85 |
2 |
Man City |
36 |
31 |
75 |
3 |
Chelsea |
36 |
34 |
69 |
4 |
Arsenal |
36 |
31 |
67 |
5 |
Tottenham |
36 |
18 |
66 |
6 |
Everton |
36 |
14 |
60 |
7 |
Liverpool |
36 |
25 |
55 |
8 |
West Brom |
36 |
0 |
48 |
9 |
Swansea |
36 |
0 |
46 |
10 |
West Ham |
36 |
-8 |
43 |
11 |
Stoke |
36 |
-10 |
41 |
12 |
Fulham |
36 |
-11 |
40 |
13 |
Aston Villa |
36 |
-21 |
40 |
14 |
Southampton |
36 |
-11 |
39 |
15 |
Sunderland |
36 |
-12 |
38 |
16 |
Norwich |
36 |
-22 |
38 |
17 |
Newcastle |
36 |
-23 |
38 |
18 |
Wigan |
36 |
-23 |
35 |
19 |
Reading |
36 |
-26 |
28 |
20 |
QPR |
36 |
-28 |
25 |
*QPR & READING TAYARI ZIMESHUKA DARAJA!
SHAFFIH DAUDA APEWA SIKU 7 AJIELEZE ALIPATAJE BARUA YA FIFA
KAGERA SUGAR, SHOOTING KUUMANA KAITABA VPL
SIMBA, MGAMBO SHOOTING ZAINGIZA MIL 16
PATA TAARIFA KAMILI:
Release No. 081
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Mei 10, 2013
KAGERA SUGAR, SHOOTING KUUMANA KAITABA VPL
Kagera Sugar inaikaribisha Ruvu Shooting
ya Pwani katika mchezo pekee wa Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) utakaofanyika
kesho (Mei 11 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Kaitba mjini Bukoba.
Ingawa timu zote mbili hazipambani
kutafuta ubingwa ambao tayari umetwaliwa na Yanga wala kukwepa kushuka
daraja, mechi hiyo bado ni muhimu kwao katika mazingira matatu tofauti.
Kagera Sugar inayonolewa na kocha
mkongwe kuliko wote katika VPL, Abdallah Kibaden na ikiwa na pointi 40
yenyewe inasaka moja kati ya nafasi nne za juu ambazo zina zawadi kutoka
mdhamini wa ligi, lakini pia timu zinazoshika nafasi hizo za juu
zinapata tiketi ya kucheza michuano ya BancABC Super 8.
Kwa upande wa Ruvu Shooting ya Kocha
Charles Boniface Mkwasa yenye pointi 31 inasaka moja ya nafasi sita za
juu ambazo ni fursa ya kuingia kwenye Bodi ya Ligi Kuu Tanzania (TPL
Board) ambayo inatarajiwa kuundwa baada ya uchaguzi unaotarajiwa
kufanyika Septemba 28 mwaka huu.
Wagombea nafasi za uenyekiti na makamu
wake ni lazima watoke katika timu zilizoshika nafasi sita la juu katika
VPL msimu uliopita. Uchaguzi wa TPL Board utafanyika siku moja kabla ya
ule wa TFF uliopangwa kufanyika Septemba 29 mwaka huu.
Raundi ya 25 ya ligi hiyo itakamilika
keshokutwa (Mei 12 mwaka huu) kwa mechi kati ya wenyeji Azam na Mgambo
Shooting ya Tanga. Mechi hiyo namba 169 itachezwa katika Uwanja wa Azam
Complex ulioko Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Azam yenye pointi 48 inahitaji moja
zaidi ili kutetea nafasi yake ya umakamu bingwa iliyoutwaa msimu wa
2011/2013 na kupata tiketi ya kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya
Kombe la Shirikisho barani Afrika.
Wakati Azam ikisaka pointi hiyo moja,
Mgambo Shooting inayofundishwa na wachezaji wa zamani wa mabingwa wa
Tanzania Bara mwaka 1988, Mohamed Kampira akisaidiwa na Joseph Lazaro ni
moja ya timu ziko katika hatari ya kurudi Ligi Daraja la Kwanza (FDL)
msimu ujao.
Mgambo Shooting inahitaji pointi moja tu
katika mechi mbili ilizobakiza kukwepa kurudi FDL, ikishindwa kupata
pointi hiyo huku Polisi Morogoro na Toto Africans ya Mwanza zikishinda
mechi zao za mwisho kwa uwiano mzuri wa mabao itakuwa imekwenda na maji.
Mechi ya Azam dhidi ya Mgambo Shooting
itachezeshwa na refa Jacob Adongo kutoka Mara, na atasaidiwa na Abdallah
Rashid wa Pwani na Charles Mbilinyi wa Mwanza. Mwamuzi wa mezani
atakuwa Idd Lila wa Dar es Salaam wakati Kamishna ni Omari Walii wa
Arusha.
SIMBA, MGAMBO SHOOTING ZAINGIZA MIL 16
Mechi namba 149 ya Ligi Kuu ya Vodacom
kati ya Simba na Mgambo Shooting iliyochezwa juzi (Mei 8 mwaka huu)
kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa Simba kushinda
bao 1-0 imeingiza sh. 16,651,000.
Watazamaji 3,006 walikata tiketi
kushuhudia mechi hiyo ambayo viingilio vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000,
sh. 15,000 na sh. 20,000 huku kila klabu ikipata mgawo wa sh. 3,226,125
wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 2,539,983.05.
Mgawo mwingine wa mapato hayo ni
asilimia 15 ya uwanja sh. 1,640,402.54, tiketi sh. 3,175,000, gharama za
mechi sh. 984,241.53, Kamati ya Ligi sh. 984,241.53, Mfuko wa Maendeleo
ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 492,120.76 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa
wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 382,760.60.
TFF YATAKA MAELEZO YA BARUA YA FIFA KWA DAUDA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemtaka Shaffih Dauda ambaye ni mmiliki wa tovuti ya www.shaffihdauda.com kutoa maelezo kuhusiana na barua ya Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) aliyoiweka kwenye mtandao wake huo.
FIFA ambayo ilisimamisha mchakato wa
uchaguzi wa TFF baada ya baadhi ya wagombea kuulalamikia, baadaye ilitoa
maelekezo kuhusu mchakato huo kwa barua ambayo iliituma kwa Rais wa
TFF, Leodegar Lenga.
Rais wa TFF katika mkutano wake na
waandishi wa habari ambao Dauda alihudhuria alibainisha kuwa barua hiyo
ya FIFA hawezi kupewa kila mtu, na kuruhusu waandishi kuisoma kwa Ofisa
Habari wa TFF bila kuondoka nayo.
Wakati Rais Tenga anazungumza na
waandishi wa habari (Mei 2 mwaka huu), nakala ya barua hiyo ya FIFA
ilikuwa kwa viongozi wakuu wa TFF pekee, na viongozi wa Wizara ya
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo. Hivyo TFF imemtaka Dauda kutoa
maelezo ya mahali alipoipata barua hiyo ndani ya siku saba.
Boniface Wambura
Ofisa Habari
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)
FA CUP-FAINALI: WIGAN v MAN CITY
JUMAMOSI MEI 11, SAA 1 NA ROBO USIKU UWANJANI WEMBLEY
WAMEPOKONYWA TAJI lao la Ubingwa wa
England na Manchester United, wametupwa nje hatua ya Makundi ya UEFA
CHAMPIONZ LIGI na sasa wamebakisha FA CUP tu kuokoa Msimu wao, na
pengine kumnusuru Meneja wao Roberto Mancini, Manchester City Jumamosi
watacheza Fainali na Wigan Athletic, Timu ambayo ipo hati hati kushushwa
Daraja.
Hii ni Fainali ya 10 kwa Man City kwenye FA CUP na kwa Wigan ni Fainali ya kwanza tangu Timu yao ianzishwe Mwaka 1932.
WAPI WAMETOKA??
WIGAN:
-Raundi ya 3: Wigan 1 Bournemouth 1 MARUDIANO :Bournemouth 0 Wigan 1
-Raundi ya 4: Macclesfield Town 0 Wigan 1
-Raundi ya 5: Huddersfield Town 1 Wigan 4
-Raundi ya 6: Everton 0 Wigan 3
-NUSU FAINALI [Wembley]: Millwall 0 Wigan 2
MAN CITY:
-Raundi ya 3: Man City 3 Watford 0
-Raundi ya 4: Stoke City 0 Man City 1
-Raundi ya 5: Man City 4 Leeds United 0
-Raundi ya 6: Man City 5 Barnsley 0
-NUSU FAINALI [Wembley]: Man City2 Chelsea 2
Kwa Man City, hii ni Mechi rahisi hasa
kwa kukutana na Wigan Athletic ambayo kwenye Ligi, BPL,Barclays Premier
League, ipo hatarini kushusuhwa Daraja.
Manchester City wanatinga Fainali ya FA
CUP kwa mara ya 10 tangu kuundwa kwa Timu yao na wametwaa Kombe hili
mara 5 katka Miaka ya 1904, 1934, 1956, 1969 na 2011.
Pia, Man United wameshatokea Washindi wa Pili mara 4 katika Kombe hli Miaka ya 1926, 1933, 1955 na 1981.
Man City wakiwa ndio wamechaguliwa kuwa ‘wenyeji’ kwenye Fainali hii, Wigan watalazikimika kuvaa Jezi zao za ugenini Nyeusi.
Hii itakuwa ni Fainali ya 132 ya FA CUP na ya pili kudhaminiwa na Budweiser, Kampuni ya Bia.
Mshindi wa Mechi hii hucheza EUROPA
LIGI kwa Msimu unaofuata lakini kwa vile Man City wameshafuzu UCL, UEFA
CHAMPIONZ LIGI, kwa kutwaa nafasi ya Pili nyuma ya Mabingwa Manchester
United kwenye BPL, Barclays Premier League, Wigan ndio watatwaa nafasi
hii ya kucheza EUROPA LIGI.
MATOKEO KATI YAO MECHI ZAMWISHO:
2012/2013
17 Apr Man City 1 Wigan 0
28 Nov Wigan 0 Man City 2
2011/2012
16 Jan Wigan 0 Man City 1
10 Sep Man City 3 Wigan 0
2010/2011
05 Mar Man City 1 Wigan 1
19 Sep Wigan 0 Man City 2
2009/2010
29 Mar Man City 3 Wigan 0
18 Okt Wigan 1 Man City 1.Thursday, May 9, 2013
RIO FERDINAND, CARRICK WAMKARIBISHA DAVID MOYES MAN UNITED. . .
MWENYEKITI EVERTON KENWRIGHT AHUZUNIKA: “NI MENEJA BORA! MAN UNITED WANA BAHATI!
WAKATI Wachezaji wa Manchester United, Rio Ferdinand na Michael Carrick, wakichekelea na uteuzi wa Meneja mpya David Moyes na kumkaribisha kwa furaha, Mwenyekiti wa Everton, Bill Kenwright, amesikitishwa na kuondoka kwake na kusema Man United wamebahatika sana kumpata.
WAKATI Wachezaji wa Manchester United, Rio Ferdinand na Michael Carrick, wakichekelea na uteuzi wa Meneja mpya David Moyes na kumkaribisha kwa furaha, Mwenyekiti wa Everton, Bill Kenwright, amesikitishwa na kuondoka kwake na kusema Man United wamebahatika sana kumpata.
Jumatano, Sir Alex Ferguson alitangaza
kustaafu kuwa Meneja na leo Man United imemtangaza Mrithi wake kuwa ni
David Moyes, Mtu ambae alipendekezwa na Sir Alex Ferguson mwenyewe.
David Moyes amepewa Mkataba wa Miaka 6 na Man United ambao utaanza rasmi Julai 1.
Moyes, ambae Mkataba wake na Everton
unamalizika Juni 30, ataisimamia Everton katika Mechi zake 2 zilizobakia
za BPL, Barclays Premier League, ambazo watacheza na West Ham na
kumaliza na Chelsea hapo Mei 19 Uwanjani Stamford Bridge.
Rio Ferdinand, ambae amecheza chini ya
Ferguson kwa Miaka 10 huko Old Trafford, amesema: "Ilikuwa ni muhimu kwa
Klabu kufanya uamuzi wa haraka kabla Watu hawajaanza kuleta uvumi.
Hatujawahi kuwa na tatizo nae na Watu wanaomjua wanasema ni Mtu mwema
aliefanya kazi nzuri huko Everton.”
Nae Michael Carrick amesema anachojua
yeye ni kuwa Moyes ni mkweli kwa Wachezaji wake na Mchapa kazi aliefanya
kazi njema Everton.
Mwenyekiti Everton- Bill Kenwright
Mwenyekiti wa Everton Bill Kenwright
amemsifia Meneja wake David Moyes ambae anaondoka na kuanza kazi ya
Umeneja huko Man United kuanzia Julai 1.
Kenwright, ambae ndie alimwingiza Moyes
Goodison Park kutoka Preston North End Mwezi Machi 2002, amesema
amehuzunishwa na kuondoka kwake.
Ametamka: “Huyu ni Meneja Bora na Man
United wana bahati sana kumpata! Everton yote itahuzunika kuagana nae,
ni Meneja Bora! Hatukuweza kumzuia Mkataba wake unakwisha na yeye kaamua
kwenda Man United! Huwezi kumzuia!”
Licha ya kutofanikiwa kuchukua Kombe
lolote akiwa na Everton kwa Miaka yake 11 aliyokuwa hapo kitu pekee na
kikubwa kilichompa umaarufu ni kuiongoza Klabu masikini, isiyokuwa na
Fedha kununua Wachezaji wakubwa, kubakia BPL na kuweza kushindana kiume
na Klabu kubwa na Tajiri.
-ALIANZA kucheza Soka na Celtic
na kumalizia Preston ambako alicheza na Chipukizi David Beckham
aliepelekwa hapo kwa mkopo na Man United kati ya Februari na Machi 1995
-BAADA ya kuifikisha Preston
kwenye Fainali ya Mechi za Mchujo wa Daraja la Kwanza, Moyes akahamia
Everton kama Meneja kumrithi Walter Smith hapo Machi 2002
-ALIMPA Wayne Rooney nafasi ya
kucheza Mechi ya kwanza kwenye Ligi Agosti 2002 na kumuuza Man United
Miaka miwili baadae kwa Pauni Milioni 20.
-ALIIFIKISHA Everton nafasi ya 4 kwenye Ligi Kuu Mwaka 2005 na kucheza UEFA CHAMPIONZ LIGI
-ALIIPELEKA Everton Fainali ya FA CUP Mwaka 2009 walipofungwa 2-1 na Chelsea baada ya kuitoa Man United kwenye Nusu Fainali
Subscribe to:
Posts (Atom)