Klabu ya Tottenham Hotspurs imetangaza rasmi kukubaliana na
Real Madrid katika kumsajili kiungo wa timu hiyo Luka Modric na anasubiriwa
kupimwa afya na klabu hiyo ya LaLiga.
Kutokana na maelezo ya mtandao wa Spurs, yalisema kuwa, “
Makubaliano yameafikiana na yamebakia makubaliano binafsi baina ya mchezajina
klabu hiyo.”
Naye Raisi wa Real Madrid, Florentino Perez Rodriguez
amefurahishwa na kitendo cha kufanikishwa kwa usajili wa mchezaji huyu.
“Mahusiano mazuri kati yetu na Spurs yamepelekea kukubaliana
katika usajili wa Modric. Tunafuraha kumkaribisha Lika Modric na tutaendelea
kufanya kazi na Tottenhammiaka ijayo.” Perez aliuambia mtandao wa Spurs.
“Modric amekuwa mchezaji muhimu kwetu na tulitamani abaki na
sisi kwa muda zaid, lakini tunafuraha kwa luwa Real Madrid, klabu ambayo
tunategemea kushirikiana nayo na kuwa nayo karibu sana katika soka”
Luka aliichezea Tottenham mechi 160, akifunga magoli 17,
baada ya kujiunga nayo akitokea Dinamo Zagreb mwaka 2008.
No comments:
Post a Comment