SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF) limemzuia kiraka Kabange Twite
kuchezea Yanga hadi pale suala lake litakapoamuliwa na Shirikisho la
Soka la Kimataifa (Fifa).
Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF, Saad Kawemba,aliiambia Mwanaspoti
jana Ijumaa kuwa Kabange hatacheza kwenye Ligi Kuu Tanzania Bara kwani
suala lake liko mikononi mwa Fifa baada ya Yanga kushindwa kupata idhini
ya FC Lupopo ya kumsajili mchezaji huyo aliyesaini mkataba wa miaka
miwili Jangwani.
Kamati ya Haki za Wachezaji ya Fifa ndio itatakiwa kumuidhinisha
kwani muda wa mwisho wa kuwasajili wachezaji wa kigeni ulikuwa Desemba
15 ilivyokuwa imepangwa na TFF.
Licha ya kwamba atakuwapo kwenye msafara wa Yanga utakaoondoka kesho
Jumapili alfajiri kwenda kambini Uturuki, Tekinolojia ya Uhamisho wa
Wachezaji kwa Kompyuta (TMS) ndio imetibua mipango ya Kabange kujiunga
na pacha wake Mbuyu Twite, ambaye alijiunga na Yanga mwezi Agosti mwaka
huu.
Kawemba alisema kuwa viongozi wa Yanga walifanya mawasiliano na watu wa Lupopo kwa TMS, lakini hawakupata majibu yoyote.
Yanga waliwasiliana na Lupopo masaa mawili kabla ya dirisha dogo la
usajili wa wachezaji wa kigeni kufungwa Desemba 15, alisema Kawemba.
Hata hivyo walikwama kwani hawakupata majibu yoyote kutoka kwa watu wa Lupopo.
Fifa ilianzisha utaratibu wa uhamisho wa wachezaji kwa njia ya TMS, ambayo husaidia klabu kuwasiliana moja kwa moja
na pia vyama vya soka vya nchi husika vikifuatilia mawasiliano hayo kwa ukaribu.
Lupopo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ndio ilikuwa inammiliki mchezaji huyo kama ilivyokuwa kwa pacha wake, Mbuyu.
Kawemba alisema kufuatia hali hiyo, Yanga wanapaswa kusubiri mawasiliano kutoka kwenye klabu hiyo kwenye TMS.
Alisema, hata hivyo, pale watakapopata majibu ya Lupopo ndio
taratibu zitaanza kushughulikiwa na TFF lakini wenye maamuzi ya mwisho
watakuwa Fifa.
Yanga wakipata mawasiliano na Lupopo watapaswa kurudi kwetu ili tupeleke suala lao Fifa, alisema.
Itabidi tuwaeleza sababu za kuridhisha Fifa kuwa kwanini Yanga
waliingia TMS muda mfupi kabla ya muda wa mwisho wa usajili, pia (Fifa)
watapenda kujua sababu za Lupopo kuchelewa kujibu.
Kawemba alidokeza ikiwa Kamati ya Haki za Wachezaji itaridhika na
maelezo ya pande hizo mbili basi watatoa kibali lakini wasiporidhika
basi watamzuia Kabange kuchezea Yanga.
Aliongeza kuwa Kamati ya Haki na Uhamisho Wachezaji ndio yenye
uamuzi wa mwisho na kuongeza ikiwa Yanga watanyimwa kibali basi
hawatakuwa na ubavu wa kukata rufaa kokote.
Hakuna chombo chenye mamlaka juu ya Kamati ya
Haki na Usajili ya Fifa. Kwa hiyo Yanga wanapaswa kuelewa hilo, aliongeza.
Ninawashauri Yanga wafanye kila njia wawapate Lupopo kwani kadiri watakavyochelewa ndio watakuwa wanajiweka pabaya zaidi.
Hatua hiyo itakuwa pigo kwa Yanga kwani ilikuwa inamtegemea Kabange
angeimarisha kikosi chao kutokana na umahiri wake wa kucheza nafasi
nyingi.
Kama ilivyokuwa Mbuyu, kiraka huyo alikuwa ametolewa kwa mkopo kwenye timu ya APR ya Rwanda na Lupopo.
Lupopo ndio ilikuwa inatakiwa kuidhinisha uhamisho wa nyota huyo kwa
njia ya TMS lakini bahati mbaya utaratibu huo umekuwa ukitumika kwa
nadra nchini Congo kwa kuwa timu zao nyingi ni za ridhaa.
Kama ikishindikana, Yanga itakuwa ina wachezaji wanne tu wa kigeni
baada ya kumwachia kipa Yaw Berko, ambaye amejiunga na Lupopo.
Mwenyekiti wa Kamati ya mashindano na usajili wa Yanga Abdallah
Binkleb aliiambia Mwanaspoti jana akisema: Sisi tulikamilisha kila
kitu, tatizo liko kwao Lupopo na tumeshawaeleza TFF tunasubiri jibu
nadhani kesho (leo Jumamosi) tutapata ufafanuzi zaidi.
SAMSON MFALILA
- MWANASPOTI
Saturday, December 29, 2012
MAN UNITED YAMALIZA 2012 POINTI 7 KILELENI LIGI KUU ENGLAND!!
RATIBA/MATOKEO:
Jumamosi 29 Desemba 2012
Sunderland 1 Tottenham 2
Aston Villa 0 Wigan 3
Fulham 1 Swansea 2
Man United 2 West Brom 0
Norwich 3 Man City 4
Reading 1 West Ham 0
Stoke 3 Southampton 3
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Arsenal v Newcastle
MANCHESTER UNITED 2 WEST BROM 0
Manchester United watauanza Mwaka mpya
2013 wakiwa kileleni mwa Ligi Kuu England wakiwa Pointi 7 mbele baada ya
kuifunga West Bromwich Albion Bao 2-0 Uwanjani Old Trafford.
Bao la kwanza la Man United ni la kujifunga mwenyewe Gareth McAuley akijaribu kuokoa krosi ya Ashley Young.
Bao la Pili kwa Man United lilifungwa
katika Dakika ya 90 na Robin van Persie, alietokea Benchi Kipindi cha
Pili kumbadili Shinji Kagawa aliekuwa akicheza Mechi yake ya kwanza
tangu Oktoba kufuatia kuuguza Goti lake.
VIKOSI:
Man United: De Gea, Smalling, Vidic, Evans, Evra, Carrick, Cleverley, Valencia, Kagawa, Young, Welbeck
Akiba: Lindegaard, Ferdinand, Giggs, Hernandez, van Persie, Scholes, Buttner.
West Brom: Foster, Jones, McAuley, Tamas, Ridgewell, Thorne, Brunt, Rosenberg, Dorrans, Odemwingie, Long
Akiba: Myhill, Morrison, El Ghanassy, Jara Reyes, Lukaku, Dawson, Fortune.
Refa: Jon Moss
STOKE 3 SOUTHAMPTON 3
Bao la Dakika ya 90 la Cameron Jerome limewapa Stoke City, waliokuwa wakicheza Mtu 10, sare ya Bao 3-3 na Southampton.
Southampton ndio walitangulia kufunga kwa Bao la Lambert lakini Stoke wakasawazisha kupitia Kenwyne Jones.
Southampton wakaenda mbele kwa Bao 3-1
kwa mabao ya Jay Rodriguez na lile la kujifunga mwenyewe Andy Wilkinson
kisha Stoke wakafunga Bao la pili kupitia Matthew Upson wakati Stoke
wakicheza Mtu 10 kufuatia Kiungo wao Steven Nzonzi kupewa Kadi Nyekundu.
Ndipo likaja Shuti la Mita 30 lililohakikisha Stoke City wakiendelea na Rekodi yao ya kutofungwa katika Mechi 17.
VIKOSI:
Stoke: Begovic, Shotton, Huth, Upson, Wilkinson, Kightly, Whelan, Nzonzi, Etherington, Walters, Jones
Akiba: Sorensen, Palacios, Owen, Adam, Whitehead, Crouch, Jerome.
Southampton: Kelvin Davis, Hooiveld, Yoshida, Fonte, Shaw, Puncheon, Schneiderlin, Cork, Rodriguez, Do Prado, Lambert
Akiba: Boruc, Steven Davis, Ramirez, Fox, Richardson, Mayuka, De Ridder.
Refa: Mark Clattenburg
READING 1 WEST HAM 0
Leo Reading wamepata ushindi wao wa pili Msimu huo kwa Bao la Dakika ya 5 la Pavel Pogrebnyak.
VIKOSI:
Reading: Federici, Gunter, Mariappa, Pearce, Harte, Leigertwood, Karacan, Kebe, Guthrie, McAnuff, Pogrebnyak
Akiba: Taylor, Le Fondre, Hunt, Morrison, Tabb, Robson-Kanu, Cummings.
West Ham: Jaaskelainen, Tomkins, Collins, Reid, O'Brien, Noble, O'Neil, Taylor, Nolan, Jarvis, Cole
Akiba: Spiegel, Collison, Maiga, Vaz Te, Demel, Diarra, Spence.
Refa: Michael Oliver
ASTON VILLA 0 WIGAN 3
Wigan Athletic leo wamejinasua toka zile
Timu 3 za mkiani na kupanda hadi nafasi ya 16 wakiwa juu ya Aston
Villa, Timu ambayo leo wameichapa 3-0, na kuwashusha hadi nafasi ya 17.
Bao za Wigan zilifungwa na Ivan Ramis, Emmerson Boyce na Arouna Kone.
VIKOSI:
Aston Villa: Guzan, Herd, Clark, Lichaj, Lowton, Ireland, Holman, Bannan, Bennett, Weimann, Benteke
Akiba: Given, El Ahmadi, Albrighton, Westwood, Bowery, Stevens, Carruthers.
Wigan: Al Habsi, Ramis, Caldwell, Figueroa, Boyce, McCarthy, Jones, Beausejour, Kone, Di Santo, Maloney
Akiba: Pollitt, Gomez, McManaman, McArthur, Boselli, Stam, Golobart.
Refa: Kevin Friend
FULHAM 1 SWANSEA 2
Wakiwa kwao Craven Cottage, Fulham
wamefungwa Bao 2-1 na Swansea City waliocheza bila ya Straika wao hatari
Michu na huu ni ushindi wao wa kwanza katika Mechi 5 za Ligi.
Mabao ya Swansea yalifungwa na Graham na De Guzman na la Fulham lilipachikwa na Ruiz.
VIKOSI:
Fulham: Stockdale, Riether, Hangeland, Hughes, Briggs, Dejagah, Sidwell, Karagounis, Frei, Ruiz, Berbatov
Akiba: Etheridge, Kelly, Riise, Senderos, Baird, Richardson, Rodallega.
Swansea: Tremmel, Rangel, Williams, Monk, Tiendalli, de Guzman, Agustien, Dyer, Hernandez, Routledge, Graham
Akiba: Vorm, Bartley, Britton, Shechter, Moore, Ki, Davies.
Refa: Andre Marriner
NORWICH 3 MANCHESTER CITY 4
Wakicheza Mtu 10 Uwanjani Carrow Road
kufuatia Kadi Nyekundu kwa Mchezaji wao Samir Nasri, Mabingwa watetezi
Manchester City walisimama kidete na kuibuka washindi kwa Bao 4-3 dhidi
ya Norwich City.
Man City walitangulia kwa Bao 2 mbele
ndani ya Dakika 4 za kwanza mfungaji akiwa Edin Dzeko lakini Norwich
wakapata Bao moja lililofungwa na Anthony Pilkington.
Licha ya kucheza Mtu 10 kufuatia
kutolewa Nasri, City walipiga Bao la 3 kupitia Sergio Aguero na Russel
Martin akaifungia Norwich Bao la pili na kuifanya Gemu iwe 3-2 lakini
shuti la Dzeko liligonga mwamba na kumbabatiza Kipa Mark Bunn na kuipa
City Bao la 4.
Bao la 3 kwa Norwich lilifungwa na Russell Martin.
VIKOSI:
Norwich: Bunn, Martin, Turner, Bassong, Garrido, Snodgrass, Tettey, Johnson, Pilkington, Hoolahan, Morison
Akiba: Rudd, Howson, Jackson, Elliott Bennett, Barnett, Ryan Bennett, Kane.
Man City: Hart, Zabaleta, Kompany, Nastasic, Clichy, Toure, Barry, Aguero, Silva, Nasri, Dzeko
Akiba: Pantilimon, Lescott, Milner, Sinclair, Javi Garcia, Toure, Tevez.
Refa: Mike Jones
SUNDERLAND 1 TOTTENHAM 2
Tottenham leo wameshinda Mechi yao ya 6
kati ya 8 kwenye Ligi walipotoka nyuma kwa Bao la Nahodha wa Sunderland,
John O’Shea, na kushinda Bao 2-1 kwa Bao za Carlos Cuellar kujifunga
mwenyewe na Winga Aaron Lennon kupiga Bao la pili na la ushindi.
VIKOSI:
Sunderland: Mignolet, Gardner, O'Shea, Cuellar, Kilgallon, Johnson, Larsson, Colback, McClean, Sessegnon, Fletcher
Akiba: Westwood, Campbell, Wickham, McFadden, Vaughan, Ji, Bramble.
Tottenham: Lloris, Walker, Dawson, Caulker, Naughton, Lennon, Sandro, Dembele, Bale, Adebayor, Defoe
Akiba: Friedel, Dempsey, Vertonghen, Huddlestone, Parker, Sigurdsson, Livermore.
Refa: Martin Atkinson
+++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumapili 30 Desemba 2012
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Everton v Chelsea
[SAA 1 Usiku]
QPR v Liverpool
Jumanne 1 Januari 2013
SAA 9 Dak 45 Mchana]
West Brom v Fulham
[SAA 12 Jioni]
Man City v Stoke
Swansea v Aston Villa
Tottenham v Reading
West Ham v Norwich
Wigan v Man United
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Southampton v Arsenal
Jumatano 2 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Chelsea v QPR
Liverpool v Sunderland
[SAA 5 Usiku]
Newcastle v Everton
ARSENAL YAIUA NEWCASTLE 7-3!!
>>WALCOTT APIGA HETITRIKI, ATENGENEZA 2!!
MATOKEO:
MATOKEO:
Jumamosi 29 Desemba 2012
Sunderland 1 Tottenham 2
Aston Villa 0 Wigan 3
Fulham 1 Swansea 2
Man United 2 West Brom 0
Norwich 3 Man City 4
Reading 1 West Ham 0
Stoke 3 Southampton 3
Arsenal 7 Newcastle 3
ARSENAL 7 NEWCASTLE 3
Theo Walcott ameihakikishia Arsenal
kumaliza Mwaka 2012 kwa mguu mzuri alipopiga Hetitriki na kutengeneza
bao mbili zilizowabomoa Newcastle Bao 7-3 Uwanjani Emirates katika Mechi
ya Ligi Kuu England.
++++++++++++++++
MAGOLI:
Arsenal 7
-Walcott 20′, 73′, 90′
-Oxlade-Chamberlain 50′
-Podolski 64′
-Giroud 84′, 87′ .
Newcastle 3
-Ba 43′, 69′
-Marveaux 59
++++++++++++++++
Walcott, ambae mwishoni mwa Msimu huu
Mkataba wake na Arsenal unamalizika, alitangulia kuipa Arsenal Bao la
kuongoza na baada ya hapo ikawa piga ni kupige na Gemu kuwa 3-3 hadi
Dakika 17 za mwisho Arsenal walipocharuka na kubamiza Bao 4.
VIKOSI:
Arsenal: Szczesny, Sagna, Koscielny, Vermaelen, Gibbs, Arteta, Wilshere, Cazorla, Oxlade-Chamberlain, Podolski, Walcott
Akiba: Mannone, Rosicky, Giroud, Ramsey, Djourou, Coquelin, Gervinho.
Newcastle: Krul, Simpson, Coloccini, Perch, Santon, Obertan, Bigirimana, Tiote, Marveaux, Ba, Cisse
Akiba: Harper, Shola Ameobi, Sammy Ameobi, Ferguson, Tavernier, Abeid, Streete.
Refa: Chris Foy
+++++++++++++++++++++++
MSIMAMO-Timu za Juu:
=Tofauti ya Magoli inatajwa kwa Timu zilizofungana Pointi
1 Man United Mechi 20 Pointi 49
2 Man City Mechi 20 Pointi 42
3 Tottenham Mechi 20 Pointi 36
4 Chelsea Mechi 18 Pointi 35
5 Arsenal Mechi 19 Pointi 33 [Tofauti ya Magoli 18]
6 Everton Mechi 19 Pointi 33 [Tofauti ya Magoli 9]
7 WBA Mechi 20 Pointi 33 [Tofauti ya Magoli 3]
8 Stoke Mechi 20 Pointi 29
9 Swansea Mechi 20 Pointi 28
10 Liverpool Mechi 19 Pointi 25
+++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumapili 30 Desemba 2012
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Everton v Chelsea
[SAA 1 Usiku]
QPR v Liverpool
Jumanne 1 Januari 2013
SAA 9 Dak 45 Mchana
West Brom v Fulham
[SAA 12 Jioni]
Man City v Stoke
Swansea v Aston Villa
Tottenham v Reading
West Ham v Norwich
Wigan v Man United
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Southampton v Arsenal
Jumatano 2 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Chelsea v QPR
Liverpool v Sunderland
[SAA 5 Usiku]
Newcastle v Everton
MEIRELES APUNGUZIWA ADHABU YA KUFUNGIWA MECHI 11 MPAKA MECHI 4 - YATHIBITIKA HAKUMTEMEA MATE MWAMUZI!!
Mchezaji wa zamani wa Liverpool na Chelsea kiungo Raul Meireles amepata nafuu ya kupunguziwa adhabu ya kutocheza mechi 11 mpaka kufikia mechi 4.
Shirikisho la soka la Uturuki limesema ilikuwa ni vigumu kwa mchezaji kutema mate kwa kuwa alikuwa anaongea wakati wote wa tukio hilo, hata hivyo bado atakabiliwa na adhabu ya kukosa mechi nne kwa kumtukana mwamuzi.
WENGER AMKANA BA, NEYMAR BARCA BAADA 2014, ANCELOTTI na RONALDO!!
RIPOTI zimebainisha kuwa Arsene Wenger
ameua ile minong’ono kuwa wako njiani kumsajili Straika wa Newcastle,
Demba Ba, huku Meneja wa Paris St Germain Carlo Ancelotti akisisitiza
kuwa hamna nafasi ya wao kumchukua Cristiano Ronaldo na huko Brazil,
Baba Mzazi wa Neymar, amedokeza kuwa Mwanawe atajiunga na Barcelona mara
baada ya kumalizika Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2014
zitakazochezwa huko Brazil.
WENGER na BA
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amefuta
ile dhana ya kuwa wana nia ya kumsajili Straika kutoka Senegal, Demba
Ba, ambae hata Newcastle wenyewe wamenawa mikono kuwa huenda akauzwa.
Lakini Wenger amesema: “Nampenda Ba, lakini hatuwezi kumsaini!”
Demba Ba alijiunga na Newcastle akitokea West Ham Juni Mwaka 2011.
PSG na RONALDO
Kocha wa Paris St Germain Carlo Ancelotti amesisitiza Supastaa wa Real Madrid Cristiano Ronaldo hajiungi na na Timu yake.
Hivi karibuni kumekuwa na uvumi kuwa Ronaldo ataondoka Real na Klabu za Man United na PSG ndizo zinazotajwa kumchukua.
Ancelotti ametamka: “Hamna ukweli kuhusu Ronaldo kuja kwetu. Si tatizo la Pesa lakini je Klabu yake itakubali kuuzwa?”
Vile vile, Ancelotti aligusia kuwa pamoja na Lucas Moura kwenda PSG Mwezi Januari atakuwa na Wachezaji 30 Klabuni hapo.
NEYMAR na BARCA
Kwa mujibu wa Baba Mzazi wa Staa wa
Brazil na Klabu ya Santos Neymar, Mchezaji huyo atajiunga na FC
Barcelona mara baada ya Fainali za Kombe la Dunia zitakazochezwa Nchini
Brazil Mwaka 2014.
Baba huyo amesema mipango hiyo ipo
lakini bado haijakamilika na kufafanua: “Anataka kucheza Ulaya.
Tumebadili kikomo cha Mkataba wake kutoka 2015 na kuwa 2014.
Kwa sasa
atabaki Brazil hadi Kombe la Dunia kwisha! Na kwa sasa ni bora kila Mtu
akae kimya!”
Friday, December 28, 2012
GOODISON PARK KUMKARIBISHA BENITEZ KWA ‘CHUKI!’
>>JUMAPILI: EVERTON v CHELSEA!!!
>>MSIMU HUU, EVERTON HAWAJAFUNGWA NYUMBANI!!
>>CHELSEA WANAPIGWA GOODISON PARK KWA MISIMU MITATU SASA!
Rafael BenÃtez anajua fika kuwa Jumapili
atapokelewa Uwanjani Goodison Park kwa ‘chuki’ kubwa toka kwa Mashabiki
wa Everton wakati Timu yake Chelsea itakapotua hapo kucheza Mechi ya
Ligi Kuu England ya ‘Funga Mwaka 2012’ kwa vile Mashabiki hao
wanakumbuka kebehi ya Meneja huyo kwa kuibatiza Everton ni ‘Klabu Ndogo’
wakati akiwa Meneja wa Mahasimu wao wakubwa Liverpool.
Mwaka 2007 BenÃtez aliibatiza Everton
‘Klabu Ndogo’ na hilo liliwachukiza sana Mashabiki wa Everton wakati huo
na hadi leo hawajaisahau kauli hiyo.
Alipokumbushwa na Mwanahabari, Benitez
alitania: “Una kumbukumbu nzuri. Lakini sasa wanafanya vizuri bila kuwa
na uwezo mkubwa kama Timu nyingine lakini ni wapinzani wagumu! Wako juu,
wanastahili sifa!”
+++++++++++++++++++++++
MSIMAMO-Timu za Juu:
=Tofauti ya Magoli inatajwa kwa Timu zilizofungana Pointi
1 Man United Mechi 19 Pointi 46
2 Man City Mechi 19 Pointi 39
3 Chelsea Mechi 18 Pointi 35
4 Tottenham Mechi 19 Pointi 33 [Tofauti ya Magoli 9]
5 Everton Mechi 19 Pointi 33 [Tofauti ya Magoli 9]
6 WBA Mechi 19 Pointi 33 [Tofauti ya Magoli 5]
7 Arsenal Mechi 18 Pointi 30
8 Stoke Mechi 19 Pointi 28
9 Swansea Mechi 19 Pointi 25 [Tofauti ya Magoli 4]
10 Liverpool Mechi 18 Pointi 25 [Tofauti ya Magoli 2]
+++++++++++++++++++++++
Everton wapo Pointi mbili tu nyuma ya
Timu ya 3 Chelsea na wameonyesha ushindani mkubwa Msimu huu wakiwa
wamepoteza Mechi 2 tu za Ligi na ni moja ya Klabu mbili tu ambazo
hazijafungwa nyumbani Msimu huu, nyingine ikiwa ni Stoke City.
Mbali ya changamoto ya Benitez kutua
Goodison Park huku akiwa anachukiwa Chelsea, kwa Miaka ya hivi karibuni,
wana Rekodi mbovu hapo na wamefungwa kwa Misimu mitatu Uwanjani humo.
Benitez, licha ya yeye kushinda Uwanjani
Goodison Park mara 3 katika Mechi zake za mwisho hapo akiwa na
Liverpool, amekiri: “Everton ni Timu nzuri na itakuwa Mechi ngumu kwetu.
Ni Uwanjani mgumu Goodison Park!”
+++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumamosi 29 Desemba 2012
[SAA 9 Dak 45 Mchana]
Sunderland v Tottenham
[SAA 12 Jioni]
Aston Villa v Wigan
Fulham v Swansea
Man United v West Brom
Norwich v Man City
Reading v West Ham
Stoke v Southampton
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Arsenal v Newcastle
Jumapili 30 Desemba 2012
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Everton v Chelsea
[SAA 1 Usiku]
QPR v Liverpool
Jumanne 1 Januari 2013
SAA 9 Dak 45 Mchana]
West Brom v Fulham
[SAA 12 Jioni]
Man City v Stoke
Swansea v Aston Villa
Tottenham v Reading
West Ham v Norwich
Wigan v Man United
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Southampton v Arsenal
Jumatano 2 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Chelsea v QPR
Liverpool v Sunderland
[SAA 5 Usiku]
Newcastle v Everton
JINA LA ZLATAN LAONGEZWA KATIKA KAMUSI YA SWEDEN!!
2012 - umeendelea kuwa
mwaka mzuri kwa Zlatan Ibrahimovic, baada ya kupata mafanikio ya
uwanjani na kiuchumi sasa jina lake limeongezwa katika kamusi ya
kisweden na taasisi inayoshughulikia lugha nchini Sweden - Neno
'Zlatanera' lenye maana ya Zlatan au 'kutawala' limeongezwa katika
kamusi rasmi ya Sweden.
Hii imekuja kama kumtunuku mchezaji huyo ambaye amekuwa akiletea sifa nchi hiyo ndani na nje ya nchi hiyo kwa miaka takribani 10 sasa.
Hii imekuja kama kumtunuku mchezaji huyo ambaye amekuwa akiletea sifa nchi hiyo ndani na nje ya nchi hiyo kwa miaka takribani 10 sasa.
Neno 'Zlatanera' limetokana na neno la
kifaransa 'zlataner' lenye maana ya kutawala, hivyo wasweden
wakalinyambua na kuongeza herufi 'a' katika 'zlataner'.
FEDHA ZILIZOCHUKULIWA NA TRA KWENYE AKAUNTI YA TFF NI ZA VILABU VYA LIGI KUU - VYATISHIA KUGOMEA LIGI WASIPORUDISHIWA!!
Klabu
14 ambazo timu zao zinashiriki Ligi Kuu ya Vodacom zimesema hazitacheza
hatua ya pili ya Ligi hiyo inayotarajiwa kuanza Januari 26 mwakani hadi
zitakaporejeshewa fedha zao zilizochukuliwa na Mamlaka ya Mapato
Tanzania (TRA) kutoka kwenye moja ya akaunti za Shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania (TFF).
Novemba
23 mwaka huu, TRA kwa uwezo ilionao kisheria iliielekeza benki ya NMB
kuilipa fedha hizo (sh. 157,407,968) kutoka kwenye moja ya akaunti za
TFF ikiwa ni Kodi ya Lipa Kama Unavyopata (PAYE) kutoka kwenye mishahara
ya waliokuwa makocha wa timu za Taifa.
Serikali
ndiyo inayolipa mishahara ya makocha hao moja kwa moja kwenye akaunti
zao, lakini ilikuwa haikati PAYE kutoka kwenye mishahara hiyo, hivyo
malimbikizo kufikia sh. 157,407,968.
TFF
bado inaendelea na mazungumzo na pande husika (Wizara ya Habari,
Vijana, Utamaduni na Michezo kwa upande mmoja na TRA kwa upande
mwingine) ili fedha hizo zirejeshwe kwani zilitolewa na mdhamini wa Ligi
Kuu (kampuni ya Vodacom) kwa ajili ya maandalizi ya timu hizo tayari
kwa mzunguko wa pili wa Ligi hiyo.
OFISA WA CAF KUTUA MWAKANI KUKAGUA VIWANJA
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) litamtuma nchini ofisa wake Abbas
Sendyowa kukagua viwanja na hoteli ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa
utaratibu wa klabu kupata leseni zitakazoziwezesha kushiriki michuano
inayoandaliwa na Shirikisho hilo.
Ofisa
huyo kutoka Uganda atawasili nchini Januari 7 mwakani ambapo
anatarajiwa kukamilisha kazi hiyo Januari 14 mwakani na baadaye kupeleka
ripoti yake CAF.
Utekelezaji
wa kazi yake nchini utahusisha mwakilishi kutoka TFF, mwakilishi kutoka
Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, mameneja wa viwanja
husika na Ofisa Usalama wa TFF.
HAWA NDIO WACHEZAJI WANAOENDA NA YANGA UTURUKI JUMAPILI - NANI KATOSWA??
Mabingwa mara mbili mfululizo wa Kombe la Vilabu Bingwa Afrika
Mashariki al maarufu(Kagame Cup )timu ya Young Africans inatarajia
kuondoka alfajiri ya jumapili kuelekea nchini Uturuki ambako itaweka
kambi ya mazoezi kwa muda wa wiki mbili.
Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Yanga mitaa ya Twiga/Jangwani, Afisa Habari wa klabu ya Yanga Baraka Kizuguto amesema timu itaondoka alfajiri ya jumapili kwa shirika la ndege la Turkish Airline, ambapo itakua na msafara wa watu 34, wachezaji 27 na viongozi 7.
Timu itaondoka majira ya saa 10:30 alfajiri na itafika katika mji wa Instabul majira ya saa 5 kasoro dakika 10, kisha baadae majira ya saa 9 alasiri itaondoka kwenda katika mji wa Antalya uliopo kusini mwa nchi ya Uturuki ambapo itafika saa 10 ndio haswa itakapokuwa kambi ya timu alisema 'Kizuguto'
Kizuguto amesema timu itafikia katika hotel ya Sueno Beach iliyopo pembezoni mwa bahari ya Meditreanian, na itakua ikifanya mazoezi katika viwanja vikubwa viwili vilivyopo katika hotel hiyo na kiwanja kidogo cha nyasi bandia.
Majina ya watakosafiri keshokutwa alfajri ni:
Walinda Mlango: Ally Mustafa 'Barthez', Said Mohamed na Yusuph Abdul
Walinzi wa Pemebeni: Juma Abdul, Shadrack Nsajigwa, Godfrey Taita, Stephano Mwasika na Oscar Joshua
Walinzi wa kati: Mbuyu Twite, Nadir Haroub, Ladisalus Mbogo na Kelvin Yondani
Viungo: Athumani Idd, Frank Domayo, Haruna Niyonzima, Kabange Twite, Nurdin Bakari na Omega Seme
Viungo wa Pembeni: Saimon Msuva, Rehani Kibingu, Nizar Khalfani na David Luhende
Washambuliaji: Didier Kavumbagu, Said Bahanunzi, Jerson Tegete, George Banda na Hamis Kiiza
Viongozi watakaoambatana na timu hiyo ni
Kocha Mkuu: Ernest Brandts,
Kocha msaidizi: Fred Felix Minziro,
Kocha wa makipa: Razaki Siwa,
Daktari wa timu: Dr.Suphian Juma,
Meneja wa timu: Hafidh Saleh,
Afisa wa Habari : Baraka Kizuguto
na kiongozi mkuu wa msafara: Mohamed Nyenge ambae ni mjumbe wa kamati ya utendaji wa klabu ya
Akiongea na waandishi wa habari makao makuu ya klabu ya Yanga mitaa ya Twiga/Jangwani, Afisa Habari wa klabu ya Yanga Baraka Kizuguto amesema timu itaondoka alfajiri ya jumapili kwa shirika la ndege la Turkish Airline, ambapo itakua na msafara wa watu 34, wachezaji 27 na viongozi 7.
Timu itaondoka majira ya saa 10:30 alfajiri na itafika katika mji wa Instabul majira ya saa 5 kasoro dakika 10, kisha baadae majira ya saa 9 alasiri itaondoka kwenda katika mji wa Antalya uliopo kusini mwa nchi ya Uturuki ambapo itafika saa 10 ndio haswa itakapokuwa kambi ya timu alisema 'Kizuguto'
Kizuguto amesema timu itafikia katika hotel ya Sueno Beach iliyopo pembezoni mwa bahari ya Meditreanian, na itakua ikifanya mazoezi katika viwanja vikubwa viwili vilivyopo katika hotel hiyo na kiwanja kidogo cha nyasi bandia.
Majina ya watakosafiri keshokutwa alfajri ni:
Walinda Mlango: Ally Mustafa 'Barthez', Said Mohamed na Yusuph Abdul
Walinzi wa Pemebeni: Juma Abdul, Shadrack Nsajigwa, Godfrey Taita, Stephano Mwasika na Oscar Joshua
Walinzi wa kati: Mbuyu Twite, Nadir Haroub, Ladisalus Mbogo na Kelvin Yondani
Viungo: Athumani Idd, Frank Domayo, Haruna Niyonzima, Kabange Twite, Nurdin Bakari na Omega Seme
Viungo wa Pembeni: Saimon Msuva, Rehani Kibingu, Nizar Khalfani na David Luhende
Washambuliaji: Didier Kavumbagu, Said Bahanunzi, Jerson Tegete, George Banda na Hamis Kiiza
Viongozi watakaoambatana na timu hiyo ni
Kocha Mkuu: Ernest Brandts,
Kocha msaidizi: Fred Felix Minziro,
Kocha wa makipa: Razaki Siwa,
Daktari wa timu: Dr.Suphian Juma,
Meneja wa timu: Hafidh Saleh,
Afisa wa Habari : Baraka Kizuguto
na kiongozi mkuu wa msafara: Mohamed Nyenge ambae ni mjumbe wa kamati ya utendaji wa klabu ya
BPL: NI MOTO KUAGA 2012 WIKIENDI!!!
KLABU ZOTE 20 zitaingia dimbani Jumamosi
na Jumapili kucheza Mechi zao za mwisho za Mwaka 2012 kwenye BPL,
Barclays Premier League, kwa akina sie tunaiita Ligi Kuu England, na
zipo Mechi kadhaa ambazo, bila shaka, zitakuwa tamu na mvuto, na baadhi
ya hizo ni zile za Arsenal v Newcastle, Everton v Chelsea.
Zifuatazo ni Dondoo muhimu kuhusu mitanange hiyo ikiwa pamoja na Hali za Wachezaji wa kila Timu na Marefa:
+++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumamosi 29 Desemba 2012
[SAA 9 Dak 45 Mchana]
Sunderland v Tottenham
[SAA 12 Jioni]
Aston Villa v Wigan
Fulham v Swansea
Man United v West Brom
Norwich v Man City
Reading v West Ham
Stoke v Southampton
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Arsenal v Newcastle
+++++++++++++++++++++++
SUNDERLAND V TOTTENHAM HOTSPUR
Sunderland wataivaa Spurs bila Beki wa
kushoto Danny Rose ambae haruhusiwi kucheza dhidi ya Klabu yake
Tottenham kwa vile yupo hapo Sunderland kwa Mkopo.
Badala ya Danny Rose, huenda Sunderland wakamchezesha Phil Bardsley kwenye nafasi hiyo.
Tottenham wanaweza kuwa nao tena
majeruhi wao waliopona Clint Dempsey na Tom Huddlestone na pia upo
uwezekano wa Wachezaji wao walioumia kwa muda mrefu na sasa kuwa fiti
kuanza Mechi yao ya kwanza na hao ni Benoit Assou-Ekotto na Scott
Parker.
MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Sunderland 1 Man City 0
Aston Villa 0 Tottenham 4
Refa: Martin Atkinson
[Gemu; 15 Kadi za Njano 59 Kadi Nyekundu: 0]
Wasaidizi: P Kirkup & S Burt
Refa wa Akiba: Mike Dean
ARSENAL V NEWCASTLE UNITED
Wachezaji wawili wa Arsenal, Olivier
Giroud na Tomas Rosicky, wameshapona na wanaweza kucheza kwenye Mechi
kama watapangwa lakini Andre Santos na Abou Diaby bado ni majeruhi na
wanatarajiwa kurudi Wiki ijayo.
Newcastle
wana majeruhi kwa Wachezaji wao wanane na hivi karibuni Listi hiyo
imeongezeka na Vurnon Anita (enka) na Jonas Gutierrez (goti).
Kiungo wa Newcastle Cheick Tiote
amemaliza Kifungo chake cha Mechi moja lakini Mike Williamson atatumikia
Kifungo cha Mechi moja baada ya kufikisha Kadi za Njano 5.
MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Man United 4 Newcastle 3
Wigan 0 Arsenal 1
Refa: Chris Foy
[Gemu: 13 Kadi za Njano: 21 Kadi Nyekundu: 0]
Wasaidizi: S Child & H Lennard Refa wa Akiba: Anthony Taylor
NORWICH CITY V MANCHESTER CITY
Norwich watacheza bila ya Beki wao Steven Whittaker ambae ni majeruhi na nafasi yake itachukuliwa na Russell Martin.
Manchester
City wanaweza kuwa nao tena Samir Nasri na Gael Clichy ambao wamepona
maumivu yao lakini watamkosa Mchezaji wao machachari Mario Balotelli
ambae ni mgonjwa.
MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Norwich 0 Chelsea 1
Sunderland 1 Man City 0
Refa: Mike Jones
[Gemu: 12 Kadi za Njano: 44 Kadi Nyekundu: 1]
Wasaidizi: S Ledger & M McDonough
Refa wa Akiba: Craig Pawson
MANCHESTER UNITED V WEST BROMWICH ALBION
Manchester United watakuwa nao tena
Danny Welbeck, ambae amepona ugonjwa, na majeruhi Ashley Young na Phil
Jones waliopona maumivu.
Nae Shinji Kagawa ameshapona Goti lake na anatarajiwa kuanzia Benchi kwa mujibu wa Meneja wao Sir Alex Ferguson.
Majeruhi wa West Brom ni Beki Jonas Olsson, Goran Popov na Kiungo Youssouf Mulumbu.
MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Man United 4 Newcastle 3
QPR 1 West Brom 2
Refa: Jon Moss
[Gemu: 10 Kadi za Njano: 27 Kadi Nyekundu: 1]
Wasaidizi: A Garratt & C Breakspear
Refa wa Akiba: Phil Dowd
READING V WEST HAM UNITED
Meneja wa Reading Brian McDermott
amethibitisha hawana majeruhi na pia upo uwezekano wa Straika wao Jason
Roberts kucheza baada ya kupona maumivu.
Straika
wa West Ham Carlton Cole anaweza kucheza baada ya FA kuifuta Kadi
Nyekundu aliyopewa Wiki iliyopita walipocheza na Everton.
MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Reading 0 Swansea 0
West Ham 1 Everton 2
Refa: Michael Oliver
[Gemu:: 11 Kadi za Njano: 26 Kadi Nyekundu: 1]
Wasaidizi: S Bennett & M Scholes
Refa wa Akiba: Paul Tierney
ASTON VILLA V WIGAN ATHLETIC
Timu hizi zote hazina Listi za majeruhi lakini zinatoka kwenye vipigo vizito mfululizo.
MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Aston Villa 0 Tottenham 4
Everton 2 Wigan 1
Refa: Kevin Friend
[Gemu: 11 Kadi za Njano: 42 Kadi Nyekundu: 2]
Wasaidizi: J Flynn & D England
Refa wa Akiba: Howard Webb
FULHAM V SWANSEA CITY
Fulham hawana majeruhi lakini Swansea
kuna hatihati kuhusu Wachezaji wao Mahamadou Diarra, Mladen Petric na
Straika wao hatari Muchu ambao wana maumivu.
MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Fulham 1 Southampton 1
Reading 0 Swansea 0
Refa: Andre Marriner
[Gemu: 10 Kadi za Njano: 38 Kadi Nyekundu: 0]
Wasaidizi: R West & S Massey
Refa wa Akiba: Neil Swarbrick
STOKE CITY V SOUTHAMPTON
Bosi wa Stoke City Tony Pulis
atalazimika kutafuta Mabeki wengine kwa vile Nahodha wao Ryan Shawcross
na Geoff Cameron wote wapo kwenye Kifungo cha Mechi moja baada
kulimbikiza Kadi za Njano 5 kila mmoja.
Southampton watamkosa Nahodha Adam Lallana ambae ameumia goti.
MATOKEO MECHI WALIZOCHEZA MWISHONI:
Stoke 3 Liverpool 1
Fulham 1 Southampton 1
Refa: Mark Clattenburg
[Gemu: 10 Kadi za Njano: 35 Kadi Nyekundu: 4]
Wasaidizi: S Beck & S Long
Refa wa Akiba: Lee Mason
+++++++++++++++++++++++
MECHI ZIJAZO:
Jumapili 30 Desemba 2012
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Everton v Chelsea
[SAA 1 Usiku]
QPR v Liverpool
Jumanne 1 Januari 2013
SAA 9 Dak 45 Mchana]
West Brom v Fulham
[SAA 12 Jioni]
Man City v Stoke
Swansea v Aston Villa
Tottenham v Reading
West Ham v Norwich
Wigan v Man United
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Southampton v Arsenal
Jumatano 2 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Chelsea v QPR
Liverpool v Sunderland
[SAA 5 Usiku]
Newcastle v Everton
MAMENEJA VITANI! Wenger, Pardew wataka adhabu kwa Fergie!!
>>FA YAWAANDIKIA BARUA REDKNAPP & MANCINI KUJIELEZA!!
WAKATI FA, Chama cha Soka England, kimethibitisha kuwaandikia Barua za kuwataka kujieleza, Mameneja wa Man City na QPR, Roberto Mancini na Harry Redknapp, kufuatia kauli zao baada ya Mechi zao za kulalamika kuhusu Marefa na kudokeza uchezeshaji usio wa haki, Mameneja wa Arsenal, Arsene Wenger, na wa Newcastle, Alan Pardew, wamesema Sir Alex Ferguson alistahili Kadi Nyekundu kwa kubishana na Marefa kwenye Mechi kati ya Manchester United na Newcastle iliyochezwa Boxing Dei.
>>FERGIE AMPANDISHIA PARDEW!!
WAKATI FA, Chama cha Soka England, kimethibitisha kuwaandikia Barua za kuwataka kujieleza, Mameneja wa Man City na QPR, Roberto Mancini na Harry Redknapp, kufuatia kauli zao baada ya Mechi zao za kulalamika kuhusu Marefa na kudokeza uchezeshaji usio wa haki, Mameneja wa Arsenal, Arsene Wenger, na wa Newcastle, Alan Pardew, wamesema Sir Alex Ferguson alistahili Kadi Nyekundu kwa kubishana na Marefa kwenye Mechi kati ya Manchester United na Newcastle iliyochezwa Boxing Dei.
Akijiingiza kwenye mzozo huo, Arsene
Wenger amesema Sir Alex Ferguson alipaswa kuadhibiwa na Refa Mike Dean
kwa kitendo chake cha kabla Kipindi cha Pili kuanza kwenye Mechi kati ya
Manchester United na Newcastle cha kumvaa Refa Mike Dean na
kumlalamikia kisha kumkabili Refa wa Akiba Neil Swarbrick na pia Refa
Msaidizi Jake Collin.
Katika Mechi hiyo ambayo Man United
walishinda Bao 4-3, Ferguson alikuwa amekasirishwa na Refa Mike Dean
kufuta Ofsaidi iliyotolewa ishara na Msaidizi wake Jake Collin na kuamua
ni Bao kwa vile Jonny Evans alijifunga mwenyewe.
Wakati Kipindi cha Pili kinataka kuanza,
Ferguson alimvaa Refa Mike Dean na kumlalamikia kisha akamvaa Refa wa
Akiba Neil Swarbrick na pia Refa Msaidizi Jake Collin.
Lakini FA ilithibitisha jana kuwa Sir
Alex Ferguson hatachukuliwa hatua yeyote kwa vile Refa Mike Dean
hakutaja lolote kwenye Ripoti yake ya Mechi.
Wenger amesema Sheria ni msumeno na Refa Mike Dean alipaswa kumwadhibu Ferguson.
Arsene Wenger ashawahi kukumbana na Kadi
Nyekundu toka kwa Refa Mike Dean Agosti 2009 alipotolewa Uwanjani kwa
kuipiga teke chupa ya maji wakati Arsenal inachapwa 2-1 na Man United
Uwanjani Old Trafford.
WAKATI HUO HUO, Sir
Alex Ferguson amemshambulia Meneja wa Newcastle, Alan Pardew kwa kutamka
kuwa alipaswa kupewa Kadi Nyekundu kwa kubishana na Refa Mike Dean na
Wasaidizi wake wakati Newcastle ilipochapwa 4-3 na Man United Uwanjani
Old Trafford.
Ferguson amejibu mapigo kwa kusema:
“Alan Pardew amejitokeza na kuniponda mimi. Yeye ndio mbaya zaidi kwa
kuvamia Marefa, anadiriki hata kuwasukuma na kisha analeta mzaha kuhusu
hilo! Ameshasahau msaada niliompa!”
Ferguson ameongeza: “Sikufanya kosa!
Sikutoa kashfa yeyote! Nlikuwa nikiongea na Refa tu! Tatizo ni kuwa tupo
Klabu kubwa na mimi ni Meneja wa Klabu kubwa Duniani hivyo kila kitu
kinakuzwa! Sio Newcastle Klabu ndogo iliyo huko Kaskazini Mashariki!”
Pardew aliwahi kufungiwa Mechi mbili na
kudundwa Faini ya £20,000 kwa kumsukuma Refa Msaidizi wakati Newcastle
inaifunga 2-1 Tottenham Hotspur hapo Tarehe 18 Agosti.
HIVI PUNDE TU, FA,
Chama cha Soka England, kimethibitisha kuwaandikia Barua za kuwataka
kujieleza, Mameneja wa Man City na QPR, Roberto Mancini na Harry
Redknapp, kufuatia kauli zao baada ya Mechi zao za kulalamika kuhusu
Marefa na kudokeza uchezeshaji usio wa haki, kitendo ambacho ni kinyume
cha Kanuni za FA.
Mancini, Meneja wa Man City, alilalamika
kuhusu Refa Kevin Friend baada kufungwa 1-0 na Sunderland kwenye Mechi
ya Ligi Kuu England iliyochezwa Desemba 26 kwa Refa huyo kutopiga
Filimbi ya Faulo aliyochezewa Mchezaj wake Pablo Zabaleta na badala yake
kuachia mpira uchezwe na kuzaa Goli la Adam Johnson, Winga wa zamani wa
Man City, lililowaua City 1-0.
Mancini alidai: “Pengine Refa alivimbiwa na Mlo wa Krismasi! Haiwezekani Waamuzi wawili wasione tukio hilo! [Akimaanisha Refa Na Msaidizi wake]”
Nae Harry Redknapp, Bosi wa QPR, yuko
matatani baada ya kuhamaki na maamuzi ya Refa Chris Foy ambayo alidai ni
‘Skandali!’ wakati walipofungwa 2-1 na West Brom na kutupwa mkiani mwa
Ligi Kuu England Siku ya Boxing Dei.
Refa Chris Foy alilikubali Goli la
kujifunga mwenyewe Kipa Robert Green ambae alionekana akibanwa waziwazi
na Mchezaji wa WBA, Marc-Antoine Fortune, na pia aliwayima Penati ya
wazi mwishoni baada ya Beki Liam Ridgewell kuunawa mpira.
Redknapp amewaka: "Ile ni Faulo ya wazi kwa Kipa wetu na ile ni Penati ya wazi! Hii ni kashfa!”
Msimamo wa FA kwa Mameneja ni kwamba
hawatakiwi kuwalaumu Marefa kuhusu maamuzi yao na wakifanya hivyo
wanaandikiwa Barua kutaka maelezo yao na kama hayaridhishi hufunguliwa
Mashitaka.
Thursday, December 27, 2012
KADI NYEKUNDU GIBSON, COLE ZAFUTWA, FERGIE ANUSURIKA…REDKNAPP, MANCINI….!!!
Bosi wa Manchester United Sir Alex
Ferguson hatapata adhabu yeyote toka kwa FA baada ya kumvaa Refa Mike
Dean na Wasaidizi wake lakini Mameneja wa Man City, Roberto Mancini, na
wa QPR, Harry Redknapp, huenda wakaadhibiwa kwa kauli zao na wakati huo
huo Kadi Nyekundu kwa Darron Gibson wa Everton na Carlton Cole wa West
Ham zimefutwa.
Chama cha Soka England, FA,
kimethibitisha kuwa Sir Alex Ferguson, hatapewa adhabu yeyote kwa
kitendo chake cha kabla Kipindi cha Pili kuanza, cha kumvaa Refa Mike
Dean na kumlalamikia kisha kumkabili Refa wa Akiba Neil Swarbrick na pia
Refa Msaidizi Jake Collin, kwa vile Refa Dean hakuzungumza lolote
kuhusu tukio hilo katika Ripoti ya Mechi.
Hata hivyo, Mameneja wa Man City na QPR,
Roberto Mancini na Harry Redknapp, wako matatani kufuatia kauli zao
baada ya Mechi zao za kulalamika kuhusu Marefa na kudokeza uchezeshaji
usio wa haki kitendo ambacho ni kinyume cha Kanuni za FA.
Mancini, Meneja wa Man City, alilalamika
kuhusu Refa Kevin Friend baada kufungwa 1-0 na Sunderland kwenye Mechi
ya Ligi Kuu England iliyochezwa Desemba 26 kwa Refa huyo kutopiga
Filimbi ya Faulo aliyochezewa Mchezaj wake Pablo Zabaleta na badala yake
kuachia mpira uchezwe na kuzaa Goli la Adam Johnson, Winga wa zamani wa
Man City, lililowaua City 1-0.
Mancini alidai: “Pengine Refa alivimbiwa na Mlo wa Krismasi! Haiwezekani Waamuzi wawili wasione tukio hilo! [Akimaanisha Refa Na Msaidizi wake]”
Nae Harry Redknapp, Bosi wa QPR, yuko
matatani baada ya kuhamaki na maamuzi ya Refa Chris Foy ambayo alidai ni
‘Skandali!’ wakati walipofungwa 2-1 na West Brom na kutupwa mkiani mwa
Ligi Kuu England Siku ya Boxing Dei.
Refa Chris Foy alilikubali Goli la
kujifunga mwenyewe Kipa Robert Green ambae alionekana akibanwa waziwazi
na Mchezaji wa WBA, Marc-Antoine Fortune, na pia aliwayima Penati ya
wazi mwishoni baada ya Beki Liam Ridgewell kuunawa mpira.
Redknapp amewaka: "Ile ni Faulo ya wazi kwa Kipa wetu na ile ni Penati ya wazi! Hii ni kashfa!”
Msimamo wa FA kwa Mameneja ni kwamba
hawatakiwi kuwalaumu Marefa kuhusu maamuzi yao na wakifanya hivyo
wanaandikiwa Barua kutaka maelezo yao na kama hayaridhishi hufunguliwa
Mashitaka.
Wakati huo huo, FA imetangaza kuwa Rufaa
za Everton na West Ham kupinga Kadi Nyekundu kwa Wachezaji wao, Darron
Gibson wa Everton na Carlton Cole, zimekubaliwa na Adhabu za kufungiwa
Mechi 3 kila mmoja kwa Wachezaji hao zimefutwa.
Wachezaji hao wote wawili walitolewa
katika Mechi moja na Refa Mark Anthony Uwanjani Upton Park Wikiendi
iliyopita ambako Everton walishinda 2-1 baada ya kutoka nyuma kwa kwa
Bao la Carlton Cole na kutolewa kwa Mfungaji huyo kuliwapa mteremko
kusawazisha na kushinda huku Mchezaji wao Gibson akitolewa Dakika za
majeruhi.
Wachezaji hao wote wawili sasa wako huru kuziwakilisha Klabu zao Mechi za Ligi Wikiendi hii.
KENYA YATOA MAREFA WAWILI KOMBE LA MATAIFA YA AFRIKA - TANZANIA, UGANDA MMHHH!!
Waamuzi wawili wakubwa nchini Kenya wamechaguliwa kwenda nchini Afrika ya Kusini kwenda kuamua mechi ya Africa Cup of Nations (Afcon) zitakazoanza mwezi ujao huko kusini mwa bara la afrika.
Aden Marwa, ambaye ni mwalimu kutoka Nyanza kusini, amechaguliwa pamoja na refa mwingine Sylvester Kirwa, kutoka Eldoret.
Wawili hao wamechaguliwa kuamua mechi za michuano hiyo baada ya kushiriki katika kozi ya CAF ya marefa iliyofanyika huko Egypt mapema mwezi uliopita.
Marefa hao wa pekee kutoka ukanda huu wa Afrika mashariki wataenda South Africa siku ya jumanne tarehe 15, siku nne kabla ya michuano kuanza.
Marwa – ambaye alishiriki katika 2012 AFCON, zilizofanyika nchini Gabon na Equatorial Guinea – amesema kuchaguliwa kwao kwenda AFCON ni ishara nzuri kwa soka la Kenya.
Aden Marwa, ambaye ni mwalimu kutoka Nyanza kusini, amechaguliwa pamoja na refa mwingine Sylvester Kirwa, kutoka Eldoret.
Wawili hao wamechaguliwa kuamua mechi za michuano hiyo baada ya kushiriki katika kozi ya CAF ya marefa iliyofanyika huko Egypt mapema mwezi uliopita.
Marefa hao wa pekee kutoka ukanda huu wa Afrika mashariki wataenda South Africa siku ya jumanne tarehe 15, siku nne kabla ya michuano kuanza.
Marwa – ambaye alishiriki katika 2012 AFCON, zilizofanyika nchini Gabon na Equatorial Guinea – amesema kuchaguliwa kwao kwenda AFCON ni ishara nzuri kwa soka la Kenya.
CHRIS KATONGO ATUNUKIWA NA WANAJESHI WENZAKE ZAMBIA!!
Nahodha wa mabingwa wa Afrika Chris Katongo ametunukiwa na jeshi la Zambia.
Katongo, ambaye ni ofisa wa jeshi la nchi hiyo, alitunukiwa tuzo ya heshima ya jjeshi la Azambia na meja jenerali Toply Lubaya katika sherehe zilizofanyika huko Arakan barracks mwanzoni mwa wiki hii.
Tuzo hii ya heshima imekuja baada ya mshambuliaji huyo wa Zambia kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa BBC African Footballer of the Year award.
Jeshi la nchi hiyo pia lilitoa tuzo na maua kwa wachezaji wengine wa Chipolopolo ambao ni maofisa wa jeshi - Felix Katongo na Nathan Sinkala.
Katongo, ambaye ni ofisa wa jeshi la nchi hiyo, alitunukiwa tuzo ya heshima ya jjeshi la Azambia na meja jenerali Toply Lubaya katika sherehe zilizofanyika huko Arakan barracks mwanzoni mwa wiki hii.
Tuzo hii ya heshima imekuja baada ya mshambuliaji huyo wa Zambia kuchaguliwa kuwa mchezaji bora wa BBC African Footballer of the Year award.
Jeshi la nchi hiyo pia lilitoa tuzo na maua kwa wachezaji wengine wa Chipolopolo ambao ni maofisa wa jeshi - Felix Katongo na Nathan Sinkala.
BRUNO GOMES MBRAZIL ANAYEKUJA OLD TRAFFORD MWAKANI - AIPA UBINGWA TIMU YAKE - ACHUKUA KIATU CHA DHAHABU!!
Mchezaji aliyesajiliwa na Manchester United kutoka Brazil Bruno Gomes ameiongoza klabu yake ya Desportivo Brasil kutwaa ubingwa nchini hiyo wa vijana wenye miaka U17.
Gomes, 16, atajiunga na United kipindi kijacho kiangazi, alifunga hat trick katika fainali ya pili ya kugombea ubingwa huo dhidi MarÃlia, na mwishowe Desportivo wakashinda 6-0.
Mshambuliaji huyo hatari, tayari amekuwa chaguo muhimu katika kikosi cha Brazil cha vijana chini ya umri wa miaka 17, amefunga mabao 27 katika mechi 32 na kubeba kiatu cha dhahabu.
United wana mahusiano rasmi na klabu ya Desportivo Brasil, ambao wachezaji wao wamefunga mabao 88 katika mechi 32 msimu huu.
Inaeleweka kwamba pamoja na Gomes, United wapo katika mazungumzo ya kumsajili winga wa Desportivo aitwaye Welder.
Desportivo pia walishinda ubingwa Milk Cup huko Northern Ireland mwaka huu.
ASILIMIA 82 YA MASHABIKI WA MADRID WANATAKA MOURINHO ATIMULIWE KAZI REAL MADRID !!
Mashabiki wa Real Madrid wameamua. Wanataka Mourinho aondoke Bernabeu.
Kufuatia kupigwa benchi kwa Casillas katika mechi dhidi ya Malagamtandao wa gazeti maarufu nchini Hispania MARCA.com uliuliza "Je inabidi Real Madrid imtimue Mourinho?" na majibu ya takribani wasomaji 100,000 yalikuja yakisema ndio kwa asilimia 82.4%.
Kwa mujibu wa MARCA, mapenzi baina ya washabiki wa Los Blancos na Mourinho yamekwisha kabisa. Madrid wamekuwa na mfululizo wa matokeo mabaya katika kipindi cha hivi karibuni na kusababisha maneno mengi juu ya mustakabli wa kocha Jose Mourinho ndani ya klabu hiyo.
Real Madrid wapo nyuma kwa 16 dhidi ya viongozi wa La Liga Barcelona, na tayari Mourinho ameshasema kwamba ubingwa wa La liga msimu huu hawawezi kushinda tena, na inasemekana kwamba ikiwa atashindwa kuiongoza klabu hiyo kushinda ubingwa wa 10 wa mabingwa wa ulaya basi Mreno huyo atatemeshwa kibarua chake mwishoni mwa msimu.
SIMBA: HUKU ‘GOGORO’ LANUKIA, KOCHA MPYA KUTUA LEO!!
Wakati Mwenyekiti wa Simba, Ismail Aden Rage, akitamka
kuwa Mkutano wa Wanachama uliotishwa na Kundi linalodaiwa kuongozwa na
Mohamed Wandi si halali, zipo taarifa kuwa Kocha mpya wa Klabu hiyo,
Patrick Liewing, kutoka Ufaransa atatua Nchini leo.
Akizungumzia Mkutano huo ulioitishwa na
Kundi la Mohamed Wandi ambalo limeripotiwa kukusanya Saini za Wanachama
698 ili kufanya Mkutano wa Wanachama Jumapili hii kwenye Hoteli ya
Traventine Jijini Dar es Salaam, Rage amesema uchunguzi wa Watu hao 698
umebaini kuwa 490 kati yao si Wanachama hai kwa vile hawajalipa Ada zao
za Uanachama na wengine kati yao ni Marehemu.
Akithibitisha kupokea Barua ya kuitishwa
Mkutano huo wa Dharura wa Wanachama, Rage amesema Kikatiba mwenye
mamlaka ya kuitisha Mkutano wa Dharura wa Wanachama ni Mwenyekiti au
Wanachama hai 600.
Kutokana na hitilafu hizo za Kisheria, Rage amesema Uongozi wake hautautambua Mkutano huo.
Pia, Rage amedai Kundi la Viongozi wa zamani ndio wanaotaka kuitisha Mkutano huo kinyume cha Katiba yao.
Hata hivyo, Mohamed Wandi amekaririwa
akitamka kuwa Mkutano huo hauna nia mbaya ila tu ni kuchambua mwendo
mbovu wa Simba katika mzunguko wa Kwanza wa Ligi Kuu Vodacom ambao
walianza vizuri mno lakini wakamaliza vibaya na kutupwa nafasi ya 3 huku
juu yao wapo Azam FC na vinara ni Mahasimu wao wakubwa, Yanga.
Wakati huo huo, Ismail Aden Rage,
amethibitisha ujio wa Kocha wao mpya, Patrick Liewing, kutoka Ufaransa
ambae atatua Nchini leo.
Rage amesema Kocha huyo, ambae aliwahi
kufundisha Timu za Vijana za Klabu maarufu huko France, Paris Saint
Germain, atakuwa Kocha Mkuu na pia atapewa jukumu la kuendeleza vipaji
vya Vijana.
Rage amesema: “Simba ndio Timu pekee
Nchini yenye mfumo wa kuendeleza Vijana na zipo timu za Vijana chini ya
Miaka 14, 16 17 na 20! Ujio wa Liewing utatusaidia sana kwa sababu ana
uzoefu wa kukuza vipaji!”
Kocha huyo mpya kesho anatarajiwa kukutana na Wachezaji wote kwenye Kambi yao ya Mazoezi huko TCC Chang’ombe, Dar es Salaam.
Liewing, ambae anambadili Kocha kutoka
Serbia Milovan Cirkovic, aliwahi kuwa Kocha wa Asec Mimosa ya Ivory
Coast kati ya Mwaka 2004 na 2009 na kuisaidia kutwaa Makombe kadhaa
Nchini humo pamoja na kuifikisha Nusu Fainali ya CAF CHAMPIONZ LIGI
Mwaka 2009.
Mwaka 2006, Kocha Liewing pamoja na Kocha wa Al Ahly ya Misri waliteuliwa kuwa Makocha Bora Afrika.
FERGIE KULIKWAA RUNGU LA FA? MANCINI AKIRI MATATIZO!!
REDKNAPP AMLAUMU REFA KWA KURUDISHWA MKIANI!!
BENITEZ ASEMA 1-0 NI MUHIMU KAMA 8-0!!
MENEJA
wa Manchester United, Sir Alex Ferguson, anasubiri nini kitamkuta
endapo Refa Mike Dean atamtaja kwenye Ripoti yake ya Mechi ya jana
ambayo Man United waliifunga Newcastle Bao 4-3 baada ya kumkabili Refa
huyo na Wasaidizi wake kabla Kipindi cha Pili kuanza akilalamikia Bao la
pili la Newcastle.
Ferguson alikuwa amekasirishwa na Refa
Mike Dean kufuta Ofsaidi iliyotolewa ishara na Msaidizi wake Jake Collin
na kuamua ni Bao kwa vile Jonny Evans alijifunga mwenyewe.
Wakati Kipindi cha Pili kinataka kuanza,
Ferguson alimvaa Refa Mike Dean na kumlalamikia kisha akamvaa Refa wa
Akiba Neil Swarbrick na pia Refa Msaidizi Jake Collin.
Ikiwa tukio litatajwa kwenye Ripoti ya
Mechi ya Refa Mike Dean basi huenda Sir Alex Ferguson akaadhibiwa FA
lakini kwa vile Refa Dean hakumchukulia hatua yeyote Ferguson huenda
akakwepa adhabu.
Akielezea tukio hilo Ferguson alisema:
“Refa alimfanya Mshika Kibendera abadilishe uamuzi wake wa Ofsaidi.
Alisema ni Goli la kujifunga mwenyewe lakini ukilirudia Goli lile, yule
Mchezaji wa Newcastle alikuwa Ofsaidi na tena alimvuta mkono Evans! Sasa
hilo kama si kuingilia uchezaji ni nini? Ni uamuzi mbovu!”
ROBERTO MANCINI AKIRI MATATIZO MANCHESTER CITY!!
Roberto Mancini amekiri kuwa ana matatizo makubwa mara baada ya jana kuchapwa 1-0 na Sunderland.
Mancini amesema: “Tatizo kubwa Mastraika hawafungi nafasi wanazopata!”
Sasa ni mara ya 3 mfululizo kwa Man City
kufungwa Stadium of Light na Sunderland ambao jana Bao lao pekee
lilifungwa na Winga wa zamani wa Man City, Adam Johnson.
Msimu huu, Man City wamefunga Bao 34 katika Mechi 19 za Ligi Kuu England ikiwa ni Magoli 14 nyuma ya vinara Man United.
Lakini, ingawa Man City sasa wako Pointi
7 nyuma ya Man United, Roberto Mancini amesema wao bado wana nafasi ya
kutetea Taji lao.
Ametamka: “Man United wanafunga Bao
nyingi kupita sisi lakini pia wanafungwa Bao nyingi kupita sisi! Msimu
ni mrefu na ni juu yetu kubadilika!”
HARRY REDKNAPP CRITICISES REFEREE AFTER QPR'S LOSS TO WEST BROM
Bosi wa Queens Park Rangers Harry
Redknapp amekasirishwa na maamuzi ya Refa Chris Foy ambayo amedai ni
‘Skandali!’ wakati jana walipofungwa 2-1 na West Brom na kuwatupa mkiani
mwa Ligi Kuu England.
Refa Chris Foy alilikubali Goli la
kujifunga mwenyewe Kipa Robert Green ambae alionekana akibanwa waziwazi
na Mchezaji wa WBA, Marc-Antoine Fortune, na pia aliwayima Penati ya
wazi mwishoni baada ya Beki Liam Ridgewell kuunawa mpira.
Redknapp amewaka: "Ile ni Faulo ya wazi kwa Kipa wetu na ile ni Penati ya wazi! Hii ni kashfa!”
BENITEZ ASEMA 1-0 NI MUHIMU KAMA 8-0!!
Bosi wa Chelsea Rafael Benitez anaamini
ushindi wa Bao 1-0 dhidi ya Norwich hapo jana ni muhimu kama kile
kipondo cha 8-0 walichowashushia Aston Villa Siku 3 zilizopita.
Ingawa Wadau wengi wa Klabu hiyo
watahisi kimchezo ushindi wa 1-0 ni tofauti na ule wa 8-0, Benitez
ametetea matokeo hayo kwa kusema: “Ni muhimu kuiona Timu ikicheza kwa
bidii na kujilinda kisawasawa! Muhimu ni kuwa hatukufungwa Bao.”
Chelsea sasa wako nafasi ya 3 wakiwa Pointi 4 tu nyuma ya Man City na Mechi moja mkononi.
+++++++++++++++++++++++
MECHI ZIJAZO:
Jumamosi 29 Desemba 2012
[SAA 9 Dak 45 Mchana]
Sunderland v Tottenham
[SAA 12 Jioni]
Aston Villa v Wigan
Fulham v Swansea
Man United v West Brom
Norwich v Man City
Reading v West Ham
Stoke v Southampton
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Arsenal v Newcastle
Jumapili 30 Desemba 2012
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Everton v Chelsea
[SAA 1 Usiku]
QPR v Liverpool
Jumanne 1 Januari 2013
SAA 9 Dak 45 Mchana]
West Brom v Fulham
[SAA 12 Jioni]
Man City v Stoke
Swansea v Aston Villa
Tottenham v Reading
West Ham v Norwich
Wigan v Man United
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Southampton v Arsenal
Jumatano 2 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Chelsea v QPR
Liverpool v Sunderland
[SAA 5 Usiku]
Newcastle v Everton
STOKE WAICHARAZA LIVERPOOL, SPURS YAINYUKA VILLA!
SPURS YAKAMATA NAFASI YA 4, LIVERPOOL NI 10!!
+++++++++++++++++++++++
MATOKEO:
Jumatano 26 Desemba 2012
Everton 2 Wigan 1
Fulham 1 Southampton 1
Man United 4 Newcastle 3
Norwich 0 Chelsea 1
QPR 1 West Brom 2
Reading 0 Swansea 0
Sunderland 1 Man City 2
Aston Villa 4 Tottenham 0
Stoke 3 Liverpool 1
+++++++++++++++++++++++
STOKE 3 LIVERPOOL 1
Stoke City, wakiwa kwao Uwanja wa
Britannia, walizinduka toka kufungwa Bao la Penati la Sekunde 35
iliyofungwa na Nahodha Steven Gerrard kwa kushinda Bao 3-1.
=================
MAGOLI:
Stoke 3
-Walters Dakika ya 5 & 49
-Jones 12
Liverpool 1
-Gerrard Dakika ya 2 [Penati]
=================
Bao mbili za Jon Walters na la Kenwyne
Jones ndio yamewapa Stoke City ushindi wao wa kwanza katika Mechi 4 na
kuendeleza wimbi lao la kutofungwa katika Mechi 9 ikiwa na pamoja ya
kutofungwa Uwanjani kwao tangu Februari.
Kipigo cha Liverpool Uwanjani Britannia
kimeendeleza Rekodi yao ya kutoshinda hapo na pia kuwarudisha hadi
nafasi ya 10 wakiwa Pointi 8 nyuma ya Timu iliyokamata nafasi ya 4.
VIKOSI:
Stoke: Begovic, Cameron, Shawcross, Huth, Wilkinson, Kightly, Nzonzi, Whelan, Etherington, Walters, Jones
Akiba: Sorensen, Adam, Whitehead, Upson, Crouch, Shotton, Jerome.
Liverpool: Reina, Johnson, Skrtel, Agger, Jose Enrique, Gerrard, Lucas, Downing, Shelvey, Suso, Suarez
Akiba: Jones, Cole, Henderson, Coates, Carragher, Allen, Sterling.
Refa: Howard Webb
ASTON VILLA 0 TOTTENHAM 4
Bao 4 za Kipindi cha Pili, ikiwemo
Hetitriki ya Gareth Bale, imewapa ushindi Tottenham wa Bao 4-0 dhidi ya
Aston Villa waliokuwa kwao Villa Park na hiki kimekuwa kipigo chao cha
pili kizito baada ya kutandikwa 8-0 na Chelsea majuzi.
VIKOSI:
Aston Villa: Guzan, Lowton, Herd, Clark, Baker, Bennett, Westwood, El Ahmadi, Delph, Holman, Benteke
Akiba: Given, Ireland, Albrighton, Bowery, Bannan, Lichaj, Carruthers.
Tottenham: Lloris, Walker, Gallas, Vertonghen, Naughton, Lennon, Dembele, Sandro, Bale, Defoe, Adebayor
Akiba: Friedel, Parker, Dawson, Sigurdsson, Livermore, Townsend, Caulker.
Refa: Mark Clattenburg
+++++++++++++++++++++++
MECHI ZIJAZO:
Jumamosi 29 Desemba 2012
[SAA 9 Dak 45 Mchana]
Sunderland v Tottenham
[SAA 12 Jioni]
Aston Villa v Wigan
Fulham v Swansea
Man United v West Brom
Norwich v Man City
Reading v West Ham
Stoke v Southampton
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Arsenal v Newcastle
Jumapili 30 Desemba 2012
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Everton v Chelsea
[SAA 1 Usiku]
QPR v Liverpool
Jumanne 1 Januari 2013
SAA 9 Dak 45 Mchana]
West Brom v Fulham
[SAA 12 Jioni]
Man City v Stoke
Swansea v Aston Villa
Tottenham v Reading
West Ham v Norwich
Wigan v Man United
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Southampton v Arsenal
Jumatano 2 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Chelsea v QPR
Liverpool v Sunderland
[SAA 5 Usiku]
Newcastle v Everton
Wednesday, December 26, 2012
VINARA MAN UNITED 7 MBELE, MABINGWA CITY WACHAPWA!!
CHELSEA WASHINDA, WAINYEMELEA CITY!!
LEO
MABINGWA WATETEZI wa Ligi Kuu England, Manchester City ambao wako
nafasi ya pili, wamechapwa Bao 1-0 na Sunderland huko Stadium of Light,
kwa Bao la Mchezaji wao wa zamani Adam Johnson, na kuwatupa Pointi 7
nyuma ya vinara Manchester United, ambao leo waliifunga Newcastle Bao
4-3 Uwanjani Old Trafford baada ya kuwa nyuma mara 3 na Bao la ushindi
kufungwa Dakika ya 90 na Chicharito huku Chelsea wakiitungua Norwich
City kwa Bao 1-0 na kujizatiti nafasi ya 3 wakiwa Pointi 4 nyuma ya City
huku wakiwa na Mechi 1 mkononi.
+++++++++++++++++++++++
MATOKEO/RATIBA:
Jumatano 26 Desemba 2012
Everton 2 Wigan 1
Fulham 1 Southampton 1
Man United 4 Newcastle 3
Norwich 0 Chelsea 1
QPR 1 West Brom 2
Reading 0 Swansea 0
Sunderland 1 Man City 2
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Aston Villa v Tottenham
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Stoke v Liverpool
+++++++++++++++++++++++
MAN UNITED 4 NEWCASTLE 3
Manchester United leo wameifunga
Newcastle Bao 4-3 Uwanjani Old Trafford baada ya kutoka nyuma mara 3 na
sasa wapo kileleni mwa Ligi Kuu England wakiwa Pointi 7 mbele.
=================
MAGOLI:
Man United 4
-Evans Dakika ya 25
-Evra 58
-Van Persie 71
-Hernandez 90
Newcastle 3
-Perch Dakika ya 4
-Evans 28 [Kajifunga mwenyewe]
-Cisse 68
=================
Bao la ushindi kwa Manchester United
lilifungwa na Javier Hernandez ‘Chicharito’ katika Dakika ya 90 baada ya
pasi murua ya Michael Carrick.
Mechi hii iligubikwa na utata mkubwa
kuhusu Bao la Pili la Newcastle ambalo awali lilikataliwa baada ya Refa
Msaidizi kutoa ishara ya Kibendera kuwa Demba Ba alikuwa ameotea ingawa
Bao hili lilikuwa la kujifunga mwenyewe Evans.
VIKOSI:
Man United: De Gea, Smalling, Ferdinand, Evans, Evra, Valencia, Carrick, Scholes, Giggs, van Persie, Hernandez
Akiba: Lindegaard, Vidic, Cleverley, Fletcher, Buttner, Wootton, Tunnicliffe.
Newcastle: Krul, Simpson, Williamson, Coloccini, Santon, Anita, Perch, Bigirimana, Cisse, Ba, Marveaux
Akiba: Elliot, Shola Ameobi, Obertan, Sammy Ameobi, Ferguson, Tavernier, Campbell.
Refa: Mike Dean
SUNDERLAND 1 MAN CITY 0
Winga wa zamani wa Mabingwa Manchester
City, Adam Johnson, leo aliifungia Sunderland Bao moja, pekee na la
ushindi, dhidi ya Timu yake ya zamani ilipozamishwa Bao 1-0 huko Stadium
of Light na kuwatupa Mabingwa hao Pointi 7 nyuma ya vinara Man United
wakiwa nafasi ya pili.
VIKOSI:
Sunderland: Mignolet, Gardner, Rose, Kilgallon, Cuellar, Larsson, Colback, Johnson, McClean, Sessegnon, Fletcher
Akiba: Bardsley, Campbell, Wickham, McFadden, Vaughan, Bramble, Westwood.
Manchester City: Hart, Kompany, Zabaleta, K Toure, Nastasic, Y Toure, Garcia, Silva, Milner, Aguero, Tevez
Akiba: Pantilimon, Lescott, Rekik, Barry, Razak, Sinclair, Dzeko.
Refa: Kevin Friend
EVERTON 2 WIGAN 1
Everton leo wameendeleza wimbi lao la
kutofungwa katika Mechi 7 za Ligi baada ya Magoli ya Leon Osman na Phil
Jagielka kuwapa ushindi wa 2-1 dhidi ya Wigan Uwanjani Goodison Park.
Bao la Wigan lilifungwa na Arouna Kone.
Bao la pili la Everton lilizalishwa na Nahodha wao Phil Neville ambae leo alikuwa akicheza Mechi yake ya 500 kwenye Ligi.
Ushindi wa leo umewapaisha Everton hadi
nafasi ya 4 wakiwa Pointi 2 tu nyuma ya Chelsea ambao watacheza nao
Uwanjani Goodison Park hapo Jumapili.
VIKOSI:
Everton: Howard, Neville, Jagielka, Distin, Baines, Osman, Hitzlsperger, Gibson, Pienaar, Jelavic, Anichebe
Akiba: Mucha, Heitinga, Oviedo, Naismith, Gueye, Barkley, Vellios.
Wigan: Al Habsi, Boyce, Caldwell, Figueroa, Stam, McCarthy, Jones, McArthur, Beausejour, Maloney, Kone
Akiba: Pollitt, Di Santo, Gomez, McManaman, Boselli, Ramis, Golobart.
Refa: Lee Mason
QPR 1 WEST BROM 2
Ushindi kwa West Brom wa Bao 2-1 umewazamisha QPR hadi mkiani mwa Msimamo wa Ligi Kuu England.
Bao za WBA zilifungwa na Chris Brunt na
la pili ni la kujifunga wenyewe QPR baada Kipa Robert Green kuutumbukiza
mpira wavuni mwenyewe ingawa ilionekana wazi Kipa huyo alikuwa kabanwa
na Marc Antoine-Fortune na halikustahili kuhesabiwa Goli halali.
Bao la QPR lilifungwa na Djibril Cisse.
VIKOSI:
QPR: Green, Da Silva, Ferdinand, Hill, Traore, Mbia, Faurlin, Mackie, Taarabt, Wright-Phillips, Cisse
Akiba: Julio Cesar, Diakite, Derry, Granero, Dyer, Hoilett, Ehmer.
West Brom: Foster, Jones, McAuley, Olsson, Popov, Mulumbu, Morrison, Fortune, Gera, Brunt, Lukaku
Akiba: Myhill, Ridgewell, Rosenberg, Long, Dorrans, Odemwingie, Tamas.
Refa: Chris Foy
NORWICH 0 CHELSEA 1
Bao tamu la Juan Mata limewafikisha
Chelsea, ambao wako nafasi ya 3, kuwa Pointi 4 tu nyuma ya Manchester
City ambao wako nafasi ya pili na kuwapa kipigo cha pili mfululizo
Norwich.
Chelsea wamecheza Mechi moja pungufu.
VIKOSI:
Norwich: Bunn, Martin, Turner, Bassong, Garrido, Snodgrass, Tettey, Johnson, Pilkington, Hoolahan, Holt
Akiba: Rudd, Howson, Jackson, Morison, Elliott Bennett, Barnett, Ryan Bennett.
Chelsea: Cech, Azpilicueta, Ivanovic, Cahill, Cole, Mikel, Luiz, Moses, Oscar, Mata, Torres
Akiba: Turnbull, Lampard, Hazard, Ferreira, Marin, Piazon, Ake.
Refa: Jon Moss
READING 0 SWANSEA 0
Sare ya 0-0 na Swansea City Uwanjani Madejski leo imewanasua Reading toka mkiani kwenye Ligi Kuu England.
Licha ya sare hiyo, Swansea City pia
wamekumbwa na wasiwasi baada ya Straika wao mkuu Michu, ambae ndie
amefungana na Robin van Persie wa Man United kama Wafungaji Bora wa Ligi
wote wakiwa na Goli 13 kila mmoja, kutolewa nje wakati wa Mechi akiwa
anachechemea.
VIKOSI:
Reading: Federici, Gunter, Pearce, Mariappa, Harte, Kebe, Leigertwood, Karacan, McAnuff, Guthrie, Pogrebnyak
Akiba: Taylor, Le Fondre, Hunt, Morrison, Tabb, Robson-Kanu, Cummings.
Swansea: Vorm, Tiendalli, Chico, Williams, Davies, Dyer, Britton, Ki, Moore, Routledge, Michu
Akiba: Tremmel, Bartley, Graham, Monk, Shechter, de Guzman, Agustien.
Refa: Mike Jones
FULHAM 1 SOUTHAMPTON 1
Penati ya Dakika za mwishoni ya Rickie
Lambert imewapa Southampton sare ya 1-1 walipocheza ugenini Uwanjani
Craven Cottage walipocheza na Fulham ambao Bao lao lilifungwa na Dimitar
Berbatov aliesheherekea Bao hilo kwa kuvua Jezi yake na kuonyesha
Tisheti iliyoandikwa: ‘TULIZA BOLI, MUWE MNANIPASIA MIMI MPIRA!’
VIKOSI:
Fulham: Schwarzer, Riether, Hangeland, Senderos, Riise, Dejagah, Sidwell, Baird, Kacaniklic, Berbatov, Rodallega
Akiba: Stockdale, Kelly, Ruiz, Karagounis, Briggs, Hughes, Frei.
Southampton: Kelvin Davis, Clyne, Fonte, Yoshida, Shaw, Schneiderlin, Cork, Steven Davis, Puncheon, Ramirez, Lambert
Akiba: Boruc, Hooiveld, Rodriguez, Ward-Prowse, Do Prado, Richardson, Mayuka.
Refa: Phil Dowd
+++++++++++++++++++++++
MECHI ZIJAZO:
Jumamosi 29 Desemba 2012
[SAA 9 Dak 45 Mchana]
Sunderland v Tottenham
[SAA 12 Jioni]
Aston Villa v Wigan
Fulham v Swansea
Man United v West Brom
Norwich v Man City
Reading v West Ham
Stoke v Southampton
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Arsenal v Newcastle
Jumapili 30 Desemba 2012
[SAA 10 na Nusu Jioni]
Everton v Chelsea
[SAA 1 Usiku]
QPR v Liverpool
Jumanne 1 Januari 2013
SAA 9 Dak 45 Mchana]
West Brom v Fulham
[SAA 12 Jioni]
Man City v Stoke
Swansea v Aston Villa
Tottenham v Reading
West Ham v Norwich
Wigan v Man United
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Southampton v Arsenal
Jumatano 2 Januari 2013
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Chelsea v QPR
Liverpool v Sunderland
[SAA 5 Usiku]
Newcastle v Everton
Subscribe to:
Posts (Atom)