Tuesday, June 4, 2013

EVERTON KULIPIA KUMCHUKUA MARTINEZ, JESUS NAVAZ YUKO CITY!

JOSE MOURINHO: “KURUDI TENA CHELSEA NI UAMUZI RAHISI!”
 
SOMA ZAIDI:
WIGAN_1_CITY_0EVERTON KULIPA FIDIA YA KUMCHUKUA  MARTINEZ KWA WIGAN

Everton wamefikia makubaliano na Wigan ya kuwalipa fidia ikiwa watamchukua Meneja wao Roberto Martinez.
Martinez, Raia wa Spain mwenye Miaka 39, anatarajiwa kumbadili David Moyes ambae anahamia Manchester United kuchukua nafasi ya Sir Alex Ferguson aliestaafu.

Kuondoka kwa Martinez toka Wigan alikodumu kwa Miaka minne kulithibitishwa na Mwenyekiti wa Klabu hiyo Dave Whelan ambae pia alisema yeye na mwenzake wa Everton walishakubaliana kuhusu Martinez.


WASIFU: Roberto Martinez

MIAKA: 39

UCHEZAJI: Real Zaragoza (1993-94), Balaguer (1994-95), Wigan Athletic (1995-2001), Motherwell (2001-02), Walsall (2002-03), Swansea (2003-06), Chester City (2006-07).

MATAJI KAMA MCHEZAJI: Copa del Rey (1994), Football League Third Division (1997), Football League Trophy (1999 & 2006)

UMENEJA: Swansea (2007-09) na Wigan Athletic (2009-13).

MATAJI KAMA MENEJA: Football League One (2008) & FA Cup (2013).

 Inatarajiwa kuhamia kwa Martinez kwenda Everton kunaweza kuthibitishwa katika Masaa 48 yajayo.
Msimu huu Martinez aliiwezesha Wigan kutwaa Kombe la FA CUP walipoifunga Manchester City Bao 1-0 lakini Siku chache baadae wakaporomoka Daraja toka BPL, Barclays Premier League na Msimu ujao watacheza Daraja la chini, Championship.

MAN CITY YAMCHUKUA WINGA WA SEVILLA JESUS NAVAS

Manchester City wamefikia makubaliano na Klabu ya Spain Sevilla ya kumnunua Winga wa Kimataifa wa Spain Jesus Navas.

Navas, mwenye Miaka 27, anategemewa kununuliwa kwa gharama ya Pauni Milioni 17.
Navas yumo kwenye Kikosi cha Spain kitakachocheza Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara huko Brazil kuanzia Juni 15.

Hadi sasa Man City haijatangaza nani Meneja wao mpya baada ya kumtimua Roberto Mancini ingawa wengi wanategemea Manuel Pellegrini, aliekuwa Malaga, ndio atachukua nafasi hiyo.

JOSE MOURINHO: “KURUDI TENA CHELSEA NI UAMUZI RAHISI!” 

Mara baada ya Chelsea kuthibitisha kuwa Jose Mourinho ndie atakuwa Meneja wao mpya, hii ikiwa ni mara ya pili kwa yeye kushika wadhifa huo baada ya kuwa hapo kati ya Miaka 2004 hadi 2007, Mourinho ametamka kuwa uamuzi wa kurudi kwake ulikuwa rahisi.

Mourinho alisema: “Nilimuuliza Bosi [Abramovich] unataka nirudi? Na yeye akaniuliza, unataka kurudi? Baada ya Dakika chache uamuzi ukafanywa!”

Akigusia mipango yake na Chelsea, Mourinho aligusia kuwa nia yake ni kuiboresha Timu lakini si kwa kutumia Mamilioni kuwanunua Wachezaji wapya.

Msimu huu uliopita Chelsea ilimaliza BPL ikiwa Nafasi ya 3 na pia kutwaa Kombe la EUROPA LIGI.

Monday, June 3, 2013

STARS WATUA MARRAKECH!


TAIFA_STARS-FRAMEDJUMAMOSI JUNI 8, MOROCCO v TAIFA STARS [SAA 5 USIKU]

SAMATTA & ULIMWENGU KUJIUNGA NA KIKOSI LEO!!

PATA HABARI KAMILI:

Taifa Stars imewasili hapa Marrakech, Morocco leo- Juni 3 mwaka huu tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya wenyeji Morocco itakayochezwa Jumamosi- Juni 8 mwaka huu.

Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imefikia hoteli ya Pullman ambayo pia Ivory Coast ilifikia ilipokuja kucheza hapa dhidi ya Morocco. Stars imetua na wachezaji 21 huku Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu waliokuwa Maputo, Msumbiji kwenye mechi ya Kombe la Shirikisho na timu yao ya TP Mazembe watawasili kesho- Juni 4 mwaka huu saa 8 mchana.

Mechi kati ya Stars na Morocco itachezwa kuanzia saa 3 usiku kwa saa za hapa wakati nyumbani itakuwa ni saa 5 usiku.

Boniface Wambura

Ofisa Habari

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Marrakech, Morocco


VIDEO & PHOTOS: NEYMAR ATAMBULISHWA NA KUONGEA NA MASHABIKI WA BARCELONA KWA MARA YA KWANZA @CAMP NOU



Neymar Da Silva akiingia rasmi Camp Nou baada ya kufaulu vipimo leo hii na kujiunga na Barcelona kwa mkataba wa miaka mitano.


Arrival: Neymar was unveiled as a Barcelona player at the Nou Camp on Monday
Welcome: The Brazilian has signed a five-year deal with the Catalan club


Juggling: Neymar showed off his skills to the Nou Camp crowd

FC Barcelona's new signing Neymar

RIO FERDINAND: KUFANYIWA MECHI SPESHO KWA UTUMISHI ULIOTUKUKA!

RIO_NA_UBINGWANI OLD TRAFFORD, MAN UNITED v SEVILLA!
MABINGWA Manchester United leo wametangaza kufanyika kwa Mechi maalum ya kutambua Utumishi wa muda mrefu na uliotukuka wa Beki wao Rio Ferdinand.

Mechi hiyo itafanyika Uwanja wa Old Trafford dhidi ya Sevilla ya Spain hapo Agosti 9 ikiwa ni Siku mbili tu kabla ya Man United kucheza Uwanja wa Wembley katika ile Mechi ya kufungua pazia ya Msimu mpya watakapokutana na Wigan Athletics ambao ndio Mabingwa wa FA CUP hapo Agosti 11.

Ferdinand, Miaka 34, Msimu uliokwisha Mwezi Mei alikuwa akitimiza Miaka 11 akiwa na Man United chini ya Meneja aliestaafu hivi karibuni Sir Alex Ferguson na tayari Beki huyo ameongezewa Mwaka mmoja katika Mkataba wake utakaomweka hadi mwisho wa Msimu wa 2013/14.

Mwenyewe Rio Ferdinand amenena: “Hii Klabu ni ya kipekee kwa kila hali, historia yake na msukumo wake huwezi kuamini, unamfanya kila Mtu apiganie kufanikiwa!”

Aliongeza: “Usiku huo utakuwa mkubwa kwangu na utatikisa mawazo yangu! Siamini kama Miaka 10 imepita na nina bahati kuitumikia Man United! Mashabiki wetu ni bora Dunia nzima, wana mapenzi na ninashkuru kwa sapoti yao. Natumai watapata raha Usiku huo!”

Sir Alex Ferguson, ambae alimsaini Ferdinand Mwaka 2002 toka Leeds United, alisema: “Ni kitu muhimu kwa Klabu kuweka Mechi hii spesho kwa Utumishi wake! Yeye ni mmoja wa Mabeki bora Klabu hii imepata kuwa nao! Rio ana kipaji cha asili cha kusoma Mchezo na Mwezi uliokwisha nilitamka kwamba naamini Msimu huu ndio uliokuwa bora katika maisha yake na Man United! Utakuwa Usiku murua kwake na Mashabiki, na pia ni safi kwa kuanza Msimu mpya namna hii!”

Rio Ferdinand ameichezea Man United Mechi 432 na kutwaa Ubingwa wa England mara 6 na Ubingwa wa Ulaya hapo Mwaka 2008.

JOSE MOURINHO RASMI STAMFORD BRIDGE!!

JOSE_MOURINHO-poaNI MENEJA WA 9 HIMAYA YA ABRAMOVICH!!
NI RASMI Jose Mourinho amerudi tena kama Meneja wa Chelsea kwa Mkataba wa Miaka minne.

Jose Mourinho, Miaka 50, anachukua nafasi ya Rafael Benitez ambae alikuwa Meneja wa muda tangu Novemba Mwaka jana na kumaliza Mkataba wake hivi Juzi tu.

Akiwa Chelsea kwa mara ya kwanza na kumalizia hapo Septemba 2007, Mourinho alifanikiwa kutwaa Ubingwa wa Ligi mara mbili mfululizo.

Akiongelea kuhusu ujio huu wa Mourinho, Mtendaji Mkuu wa Chelsea, Ron Gourlay, alitamka: “Alikuwa na bado ni Mtu anaependwa hapa Klabuni na kila Mtu ana hamu ya kufanya nae kazi tena.”

Mourinho alitua Stamford Bridge kwa mara ya kwanza kabla Msimu wa 2004 kuanza ikiwa ni muda mfupi tu baada ya kuiwezesha FC Porto kutwaa UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI.

Akiwa na Chelsea, Mourinho alitwaa FA CUP mbili, Kombe la Ligi mara mbili na Ubingwa mara mbili lakini alishindwa kuchukua UCL.

Mourinho atatambulishwa rasmi kama Meneja mpya wa Chelsea Jumatatu Juni 10.

Akiwa na Inter Milan, Mourinho alitwaa UCL kwa mara ya pili Mwaka 2010 lakini Mwaka huo huo akahamia Real Madrid kumbadili Manuel Pellegrini ambae sasa anasemekana kutaka kujiunga na Manchester City.

Katika Msimu wake wa kwanza wa La Liga, Real Madrid ilimaliza Nafasi ya Pili nyuma ya Barcelona lakini Msimu uliofuatia walinyakua Ubingwa.

Hata hivyo, Msimu huu, hakufanya vizuri na amekuwa na bifu na baadhi ya Wachezaji wake kina Iker Casillas, Sergio Ramos na Pepe na hatimae Barcelona kuipokonya Ubingwa.


MAMENEJA WA CHELSEA CHINI YA ROMAN ABRAMOVICH:

-Claudio Ranieri: Sep 2000 mpaka Mei 2004

-Jose Mourinho: Jun 2004 mpaka Sep 2007

-Avram Grant: Sep 2007 mpaka Mei 2008

-Luiz Felipe Scolari: Jul 2008 mpaka Feb 2009

-Guus Hiddink: Feb 2009 mpaka Mei 2009

-Carlo Ancelotti: Jun 2009 mpaka Mei 2011

-Andre Villas-Boas: Jun 2011 mpaka Machi 2012

-Roberto Di Matteo: Machi 2012 mpaka Nov 2012

-Rafael Benitez: Nov 2012 mpaka Mei 2013

-Jose Mourinho: Juni 2013 -


Mourinho anarudi Chelsea na kuwakuta tena baadhi ya Wachezaji aliokuwa nao mara ya kwanza kina Petr Cech, Ashley Cole, Frank Lampard, John Mikel Obi na John Terry pamoja na Michael Essien ambae alikuwa nae huko Real alikopelekwa kwa Mkopo na Chelsea.

Akizungumza kuhusu Mourinho, Mchezaji mkongwe wa Chelsea, Frank Lampard, alisema: “Ni Meneja Bora! Nimesema hili zaidi ya mara milioni, kiasi cha kuonekana kero kwa Watu, lakini nimebahatika kufanya nae kazi!”

KOMBE LA DUNIA 2014: JAPAN KUWA NCHI YA KWANZA KWENDA BRAZIL?

JAPAN-WC2014KANDA ya Nchi za Asia itamaliza hatua yake ya mwisho ya Mechi za Mchujo kwa Mechi za Makundi yake mawili Mwezi huu Juni na kesho Jumanne Mei 4 Japan inaweza kuwa Nchi ya kwanza Duniani kufuzu kutinga Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2014 huko Nchini Brazil.
 
Bara la Asia litaingiza moja kwa moja Timu 4 kwenye Fainali za Kombe la Dunia, mbili toka kila Kundi la michuano yao, na Timu ya 5 itapatikana baada ya Timu zitazoshika Nafasi za 3 kwenye Makundi kucheza Mechi kati yao na Mshindi kwenda kucheza na Timu kutoka Kanda ya Nchi za Marekani ya Kusini itakayomaliza Nafasi ya 5.

Kesho Jumanne Juni 4, Japan, wanaoongoza Kundi B  wakiwa na Pointi 13, watakuwa Nyumbani kucheza na Australia na wanahistaji sare tu ili watinge Brazil na kuwa Nchi ya kwanza Duniani kufanya hivyo lakini pia hiyo kesho wanaweza kuingia Fainali hata wakifungwa ikiwa tu Iraq, wanaocheza Ugenini, watashindwa kuifunga Oman.

Japan wangeweza kufuzu kwenda Brazil kwenye Mechi za Raundi iliyopita lakini walifungwa 2-1 bila kutegemewa walipocheza Ugenini na Jordan lakini Mechi hii na Australia, itakayochezwa huko Saitama World Cup Stadium ni ngumu kwa vile Australia wana Wachezaji wazoefu na wao wanasaka ushindi ili nao waweze kufuzu.

Matumaini ya Japan yapo kwa Wachezaji wao kina Keisuke Honda, Yuto Nagatomo na Shinji Kagawa huku Australia ikitegemea Kikosi chao chenye Wachezaji wakongwe ambao nusu yao wako kwenye Umri unaozidi Miaka 30.

Katika Mechi yao ya kwanza kwenye Kundi lao Timu hizi zilitoka sare ya Bao 1-1.



RATIBA MECHI ZILIZOBAKI:

Jumanne Juni 4

[Saa ni za Bongo, Kwenye Mabano Matokeo Mechi za Kwanza]

13:30 Japan v Australia [1-1]
13:00 Oman v Iraq [1-1]
16:15 Qatar v Iran [0-0]
 17:30 Lebanon v South Korea [0-3]

Jumanne Juni 11
8:00 Australia v Jordan [1-2]
11:00 South Korea  v Uzbekistan [2-2]
14:30 Iraq v Japan [0-1]
16:30 Iran v Lebanon [0-1]

Jumanne Juni 18
11:00 Australia v Iraq [2-1]
15:00 South Korea v Iran [0-1]
15:00 Uzbekistan v Qatar [1-0]
19:00 Jordan v Oman [1-2]

MSIMAMO:

KUNDI A
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Uzbekistan
6
3
2
1
6
4
2
11
2
South Korea
5
3
1
1
11
5
6
10
3
Iran
5
2
1
2
2
2
0
7
4
Qatar
6
2
1
3
4
7
-3
7
5
Lebanon
6
1
1
4
2
7
-5
4

KUNDI B
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Japan
6
4
1
1
14
4
10
13
2
Jordan
6
2
1
3
6
12
-6
7
3
Australia
5
1
3
1
6
6
0
6
4
Oman
6
1
3
2
6
9
-3
6
5
Iraq
5
1
2
2
4
5
-1
5

KOMBE LA DUNIA 2014: ARGENTINA YAITA WATATU TOKA NYUMBANI, TEVEZ BADO NJE!!

BRAZIL_2014_BESTTANGU KOCHA ALEJANDRO SABELLA ATEULIWE, TEVEZ HAJAIONA ARGENTINA!
 
FERNANDO GAGO, Kiungo wa zamani wa Valencia na AS Roma ambae sasa yuko Klabu ya kwaoARGENTINA_TEAM_JERSEYArgentina, Velez Sarsfield, ni mmoja wa Wachezaji watatu wa Nyumbani walioitwa kwenye Kikosi cha Argentina kwa ajili ya Mechi za Kanda ya Nchi za Marekani ya Kusini ya kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2014 zitakazochezwa huko Brazil lakini Straika wa Manchester City, Carlos Tevez, bado yupo nje baada ya kutoitwa kwa mara nyingine tena.

Pamoja na Gago, Wachezaji wengine wanaocheza ndani ya Argentina ni mwenzake wa Klabu ya Velez Sarsfield, Gino Peruzzi, na Kipa wa Boca Juniors, Agustin Orion.
Kuachwa kwa Carlos Tevez kwenye Timu ya Argentina ni kitu cha kawaida kwa Kocha wa Timu hiyo, Alejandro Sabella, ambaye hajamwita hata mara moja tangu Kocha huyo achukue madaraka Mwaka 2011.
Tevez ameichezea Argentina mara 62 na kufunga Goli 13.

Kwenye Mechi za Kanda ya Nchi za Marekani ya Kusini za kuwania kufuzu Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2014, Argentina, ambao ndio Vinara, Ijumaa watacheza Nyumbani na Colombia na Siku 4 baadae watasafiri kuivaa Ecuador ambayo inashika Nafasi ya Pili.

KIKOSI KAMILI:

MAKIPA: Sergio Romero (Sampdoria), Mariano Andujar (Catania), Agustin Orion (Boca Juniors)

MABEKI: Pablo Zabaleta (Manchester City), Hugo Campagnaro (Napoli), Ezequiel Garay (Benfica), Federico Fernandez (Getafe), Fabricio Coloccini (Newcastle United), Jose Basanta (Monterrey), Marcos Rojo (Sporting Lisbon), Gino Peruzzi (Velez Sarsfield)

VIUNGO: Javier Mascherano (Barcelona), Fernando Gago (Velez Sarsfield), Ever Banega (Valencia), Walter Montillo (Santos), Jose Sosa (Metalist Kharkiv), Augusto Fernandez, (Celta Vigo), Lucas Biglia (Anderlecht), Pablo Guinazu (Libertad), Angel Di Maria (Real Madrid), Erik Lamela (AS Roma)

MAFOWADI: Lionel Messi (Barcelona), Gonzalo Higuain (Real Madrid), Ezequiel Lavezzi (Paris Saint-Germain), Rodrigo Palacio (Inter Milan), Sergio Aguero (Manchester City)

RATIBA

[Saa ni za Bongo, Kwenye Mabano Matokeo Mechi za Kwanza]

Ijumaa Juni 7
22:00 Bolivia v Venezuela [0-1]
00:05 Argentina v Colombia [2-1]

Jumamosi Juni 8
00:10 Paraguay v Chile [0-2]
02:10 Peru v Ecuador [0-2]

Jumanne Juni 11
22:30 Colombia v Peru [1-0]
23:00 Ecuador v Argentina [0-4]

Jumatano Juni 12
00:00   Venezuela v Uruguay [1-1]
00:30 Chile v Bolivia [2-0]

Jumapili Septemba 8
00:00 Colombia v Ecuador [0-1]
00:00 Chile v Venezuela [2-0]
00:00 Paraguay v Bolivia [1-3]
00:00 Peru v Uruguay [2-4]

MSIMAMO: 

NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1

Argentina
11
7
3
1
24
8
16
24
2

Ecuador
10
6
2
2
16
10
6
20
3


Colombia
10
6
1
3
19
7
12
19
4

Chile
11
5
0
6
16
19
-3
15
5

Venezuela
11
4
3
4
9
12
-3
15
6

Uruguay
11
3
4
4
17
21
-4
13
7

Peru
10
3
2
5
11
15
-4
11
8

Bolivia
11
2
3
6
13
20
-7
9

9


Paraguay
11
2
2
7
8
21
-13
8

**FAHAMU: Timu 4 za Juu zitafuzu moja kwa moja kucheza Fainali za Kombe la Dunia 2014 huko Brazil na Timu ya 5 itakwenda kucheza Mechi ya Mchujo na Timu kutoka Kanda ya ASIA kupata Timu 1 ya kuingia Fainali.

Sunday, June 2, 2013

CAF KOMBE LA SHIRIKISHO: TP MAZEMBE YAFUNGWA LAKINI YASONGA!

MBWANA_SAMATTA_IN_TPTIMU 8 ZAINGIA HATUA YA MAKUNDI!
 
JANA Mechi za Marudiano za Raundi ya Mtoano ya Timu 16 za Mashindano ya CAF ya Kombe la Shirikisho zilikamilika na TP Mazembe ya Congo DR, ambayo ina Wachezaji muhimu wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu, ilifungwa Bao 2-1 huko Maputo, Msumbiji na Liga Muculmana lakini ilisonga mbele kwa Jumla ya Mabao 5-2 kwa vile ilishinda katika Mechi ya Kwanza huko Lubumbashi Bao 4-0.

TP Mazembe na Washindi wengine 7 wa Raundi hii wataingizwa kwenye Droo kupanga Makundi mawili ya Timu 4 kila moja.

Timu nyingine 7 zilizosonga ni Entente Setif (Algeria), Stade Malien (Mali), Enugu Rangers (Nigeria), Etoile Sahel (Tunisia), St George (Ethopia), 3 FUS Rabat (Morocco) na 1 CA Bizertin (Tunisia).

Mashindano mengine makubwa ya CAF kwa Klabu ni CHAMPIONZ LIGI na hayo yataanza hatua za Makundi hapo Julai 20 kwa kuwepo Timu 4 kila Kundi na kucheza Ligi ya Nyumbani na Ugenini na Timu 2 za juu toka kila Kundi kuingia Nusu Fainali.

RAUNDI YA MCHUJO YA TIMU 16-MARUDIANO

MATOKEO:

[Kwenye Mabano Jumla ya Magoli kwa Mechi mbili]

Jumamosi Juni 1

2 US Bitam (Gabon) 2 Entente Setif (Algeria) 0 [2-2, Penati 3-5]

Jumapili Juni 2

Liga Muculmana (Mozambique) 2 TP Mazembe (DRC) 1 [2-5]

Lydia Academic (Burundi) 0 Stade Malien (Mali) 1 [0-6]

CS Sfaxien (Tunisia) 0 Enugu Rangers (Nigeria) 0 [0-1]

Etoile Sahel (Tunisia) 2 JSM Bejaia (Algeria) 1 [4-3]

ENPPI (Egypt) 3 St George (Ethopia) 1 [3-3, St George yasonga Goli Ugenini]

FAR Rabat (Morocco) 3 FUS Rabat (Morocco) 3 [3-4]

Ismaily (Egypt) 1 CA Bizertin (Tunisia) 0 [1-3]

KIRAFIKI: BRAZIL 2 ENGLAND 2

RooneyEnglandGERMANY YANYUKWA NA USA!
 
KATIKA Mechi ya ufunguzi rasmi ya Uwanja wa Maracana, jina rasmi Estadio Jornalista Mário Filho, huko Mjini Rio De Janeiro, Wenyeji Brazil walitoka sare ya Bao 2-2 na England hapo jana Usiku.

Brazil walitawala Kipindi chote cha kwanza lakini hawakupata Bao hasa kutokana na kusimama imara kwa Kipa Joe Hart.

MAGOLI:
Brazil 2

-Fred Dakika ya 57

-Paulinho 82

-England 2

- Oxlade-Chamberlain Dakika ya 67

-Rooney 79

Bao zote 4 za Mechi hiyo zilifungwa Kipindi cha Pili na Brazil ndio waliotangulia kufunga kupitia Fred lakini Alex Oxlade-Chamberlain alisawazisha Bao hilo.

Huo ulikuwa ni wakati wa kukumbukwa sana kwani Baba yake Mzazi Alex Oxlade-Chamberlain, Mark Chamberlain, aliekuwa Winga wa Stoke City, aliichezea England mara ya mwisho ilipocheza Maracana Mwaka 1984 na kuifunga Brazil Bao 2-0 katika Mechi ya Kirafiki.

England walitangulia na kuwa Bao 2-1 kwa Bao la Wayne Rooney kwa Shuti la Mita 25 huku zikiwa zimebaki Dakika 11 Mpira kwisha lakini Paulinho aliisawazishia Brazil Dakika 3 tu baadae.

VIKOSI:

Brazil:

12 Julio Cesar
02 Alves
03 Thiago Silva
04 David Luiz
14 Filipe (Marcelo - 46' )
11 Oscar (da Silva Lucas - 56' )
17 Dias (Hernanes - 46' )
18 Paulinho (Bernard - 83' )
09 Fred (Leandro Damiao - 80' )
10 Neymar
19 Hulk Booked (Fernando Martins - 72' )

Akiba:
01 Jefferson
22 Cavalieri
06 Marcelo
15 Dante
16 Araujo Rever
05 Fernando Martins
07 da Silva Lucas
08 Hernanes
13 Jean
20 Bernard
23 Jadson
21 Leandro Damiao

England:
01 Hart
02 Johnson (Oxlade-Chamberlain - 61' )
03 Baines (Cole - 31' )
05 Cahill
06 Jagielka
07 Jones Booked
04 Carrick
08 Lampard
09 Walcott (Rodwell - 84' )
11 Milner
10 Rooney

Akiba:
13 Foster
18 McCarthy
12 Cole
14 Lescott
15 Rodwell
16 Oxlade-Chamberlain
17 Defoe

MATOKEO MECHI NYINGINE ZA KIRAFIKI:

Lesotho 0 South Africa 2

Sudan 0 Tanzania 0

Algeria 2 Burkina Faso 0

Ireland 4 Georgia 0

Ukraine 0 Cameroon 0

United States 4 Germany 3


ADDIS ABABA: TAIFA STARS, SUDAN SARE!

STARS KUONDOKA ETHIOPIA LEO, KUPITIA CAIRO KWENDA MOROCCO!
 
PATA HABARI KAMILI: 

Release No. 094

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Juni 2, 2013

TAIFA_STARS-FRAMEDTAIFA STARS, SUDAN ZATOKA SULUHU
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imetoka sare ya bila kufungana na Sudan (Nile Crodcodile) katika mechi ya kujipima nguvu iliyochezwa leo (Juni 2 mwaka huu) kwenye Uwanja wa Addis Ababa nchini Ethiopia.

Mechi hiyo iliyochezeshwa na mwamuzi Bamlak Tessema wa Ethiopia ilikuwa sehemu ya maandalizi kwa timu zote ambazo wikiendi ijayo zinacheza mechi za mchujo za Kombe la Dunia. Wakati Stars itakuwa ugenini nchini Morocco, Sudan itacheza nyumbani dhidi ya Ghana.

Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager ilicheza vizuri mechi hiyo, hasa kipindi cha pili ambapo ilifanikiwa kutengeneza nafasi kadhaa za kufunga lakini ama washambuliaji walipiga nje au mipira yao kuokolewa na kipa Ehab Abdelfatahh wa Sudan.

Washambualiji wa Stars akina Khamis Mcha, Mrisho Ngasa na Amri Kiemba wakiongozwa na John Bocco walilitia msukosuko mara kwa mara lango la Sudan ambalo lilikuwa chini ya beki wa kati Nadir Eltayeb ambaye alifanya kazi ya ziada dakika ya 72 kuokoa mpira uliokuwa ukielekea wavuni.

Stars katika mechi hiyo iliwakilishwa na Juma Kaseja, Nadir Haroub/Vicent Barnabas, Shomari Kapombe, Kelvin Yondani, Aggrey Morris, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Salum Abubakar, John Bocco/Haruni Chanongo, Amri Kiemba/Khamis Mcha na Simon Msuva/Athuman Idd.

Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Joram Biswaro amewataka wachezaji wa Taifa Stars kuhakikisha wanaipeleka timu hiyo kwenye fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Brazil.

Timu inaondoka kesho alfajiri kwenda Morocco kwa kupitia Cairo, Misri ambapo inatarajia kuwasili Casablanca saa 8 mchana.

Boniface Wambura

Ofisa Habari

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

Addis Ababa

BRAZIL v ENGLAND LEO KUFUNGUA MARACANA!

OXLADE-CHAMBERLAIN KUFUATA NYAYO ZA BABA YAKE!

 BRAZIL KUTUMIA MECHI KWA MATAYARISHO KOMBE LA MABARA!
 
June 2, Saa 4 Usiku Bongo Taimu
 
Estadio Jornalista Mário Filho (Maracanã)
 
Rio de Janeiro

Brazil
 
BRAZIL_SOCCER_FANS BAADA kunusurika kufutwa, Mechi ya Timu za Taifa za Brazil na England itachezwa leo Usiku huko Mjini Rio De Janeiro kwenye Uwanja wa Maracana, ambao Jina lake rasmi ni Estadio Jornalista Mário Filho, ikiwa ni ufunguzi rasmi wa Uwanja huo uliofanyiwa ukarabati mkubwa.
 
Juzi, Jaji mmoja aliamua Mechi hiyo isichezwe baada ya Uwanja huo kutotimiza masharti ya usalama lakini baadae uamuzi huo ukafutwa baada ya Rufaa.

Tangu ufanyiwe ukarabati tayari Mechi moja ya maonyesho imeshachezwa iliyowahusisha Mastaa wa zamani wakati Manguli wa Brazil, Ronaldo na Bebeto, walipoongoza Timu tofauti hapo Aprili 27 na kushuhudiwa na Watazamaji Elfu 25.

Maracana, ambayo iliwahi kupakia Watazamaji hadi 200,000, ilijengwa kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 1950 ambayo Wenyeji Brazil walifungwa kwenye Fainali yake Bao 2-1 na Uruguay waliotwaa Ubingwa wa Dunia.

Kwa mara nyingine tena, Maracana itachezwa Fainali ya Kombe la Dunia hapo Mwaka 2014 wakati Brazil watakapokuwa Wenyeji na Uwanja huo utachukua Washabiki 78,838 wote wakiwa wamekaa Vitini.


MECHI ZA BRAZIL v ENGLAND UWANJA wa MARACANA:

Brazil na England zilikutana mara ya kwanza Uwanja wa Wembley Mwaka 1956.

Mechi 11 zilichezwa Uwanja wa Wembley na nyingine huko Gothenburg, Vina Del Mar, Guadalajara, Los Angeles, Washington, Paris, Shizuoka na Doha.

Zifuatazo ni Mechi zao 5 walizocheza Maracana:

-Mei 13 1959 - Brazil 2 England 0 - Watazamaji: 200,000

-Mei 30 1964 - Brazil 5 England 1 - Watazamaji: 110,000

-Juni 12 1969 - Brazil 2 England 1 - Watazamaji: 125,000

-Juni 8 1977 - Brazil 0 England 0 - Watazamaji: 77,000

-Juni 10 1984 - Brazil 0 England 2 – Watzamaji: 56,126

JUMLA: Brazil 11 England 4 Sare 9


Mara ya mwisho kwa England kucheza Maracana ilikuwa ni Mwaka 1984 walipocheza Mechi ya Kirafiki na kuifunga Brazil Bao 2-0.

Katika Mechi hiyo, mmoja wa Wachezaji alikuwa ni Mark Chamberlain, Baba Mzazi wa Mchezaji wa Arsenal, Alex Oxlade-Chamberlain, ambae leo anatarajiwa kuichezea England na kufuata nyayo za Baba yake.

Hivi Juzi, England, ilicheza Uwanjani Wembley na kutoka sare 1-1 na Republic of Ireland na kupondwa na wengi lakini Meneja wao, Roy Hodgson, ameponda msimamo huo na kudai Timu yake ipo kwenye hali nzuri.

Nao, Brazil, chini ya Meneja Luiz Felipe Scolari, wataitumia Mechi hii kama ya kupasha moto ushiriki wao kwenye Mashindano ya FIFA, Kombe la Mabara, yatakayochezwa Nchini Brazil kuanzia Juni 15 hadi 30.

VIKOSI VINATARAJIWA:

BRAZIL:

Cesar
Alves, Thiago Silva, David Luiz, Marcelo
Fernando, Paulinho
Neymar, Oscar, Moura
Fred

ENGLAND:

Hart
Johnson, Cahill Jagielka, Cole
Carrick, Milner
Oxlade-Camberlain, Lampard, Walcott
Rooney

Refa: W. Roldán‎

MECHI YA MALEJENDARI: MAN UNITED 1 REAL MADRID 2

RUUD VAN NISTELROOY ACHEZEA TIMU ZOTE 2 NA KUFUNGA!

RED_HEART_UNITED LEO huko Old Trafford ilichezwa Mechi ya Kirafiki Maalum iliyoshirikisha Manguli wa Klabu za Manchester United na Real Madrid ili kusaidia Mfuko wa Hisani wa Klabu ya Manchester United uitwao RED HEART UNITED na Real waliibuka kidedea kwa kushinda Bao 2-1. 

Kabla ya Mechi hiyo kuanza, kulikuwa na utangulizi wa Shoo Laivu ya Muziki iliyofanywa na Mastaa JLS na Amelia Lily.

Real ndio walitangulia kupata Bao lililofungwa na Morientes katika Dakika ya 40 kwa shuti la nje ya Boksi lililomshinda Kipa Edwin Van Der Sar.

Man United walisawazisha katika Dakika ya 67 baada ya Andy Cole kumtengenezea Ruud Van Nistelrooy aliefunga kwa Shuti kali.

Van Nistelrooy alianza Mechi hii kwa kuichezea Real Kipindi cha Kwanza na Kipindi cha Pili kuvaa Jezi ya Man United.

Bao la ushindi kwa Real lilifungwa na Ruben De Le Red katika Dakika ya 84 alipomhadaa Kipa Van Der Gouw alieingia kuchukua nafasi ya Edwin Van Der Sar

VIKOSI:

Man United: Van Der Sar, Martin, Irwin, Johnsen, Stam, Blackmore, Scholes, Fortune, Sharpe, Cole, Yorke

Real Madrid: Contreras, Salgado, Helguera, Pavon, Amavisca, Makelele, Hierro, Figo, Zidane, Morientes, Van Nistelrooy

LA LIGA: MOURINHO AAGA KWA USHINDI, SOCIEDAD YATINGA ULAYA, DEPORTIVO YASHUSHWA!

BARCA_HAMASA

Real Sociedad wameipiku Valencia na kutwaa nafasi ya mwisho ya Spain kucheza UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, Msimu ujao walipocheza ugenini na kuifunga Bao 1-0 Deportivo La Coruna kipigo kilichowashusha Daraja huku Jose Mourinho akiaga kwa Timu yake Real Madrid kuifunga Osasuna Bao 4-2 Uwanjani Santiago Bernabeu.
 
Valencia, walikuwa Pointi 2 mbele ya Real Sociedad kabla Mechi za mwisho za La Liga kuchezwa hiyo jana, lakini wakaambua kipigo cha 4-3 toka kwa Sevilla na ushindi wa Sociedad umewatupa nje ya UCL, Valencia.

Timu nyingine zitakazoiwakilisha Spain kwenye UCL Msimu ujao ni Mabingwa FC Barcelona, Timu ya Pili, Real Madrid, na Atletico Madrid iliyomaliza nafasi ya 3.

LA LIGA-MECHI ZA MWISHO ZA MSIMU

MATOKEO:

Real Madrid CF 4 Osasuna 2

FC Barcelona 4 Malaga CF 1 

Celta de Vigo 1 RCD Espanyol 0

Deportivo La Coruna 0 Real Sociedad 1

Real Mallorca 4 Real Valladolid 2

Rayo Vallecano 2 Athletic de Bilbao 2

Sevilla FC 4 Valencia 3

Real Zaragoza 1 Atletico de Madrid 3

Levante 1 Real Betis 1

Granada CF 2 Getafe CF 0



Bao la ushindi kwa Real Sociedad lilifungwa na Antoine Griezmann katika Dakika ya 22 na walimudu kulilinda hata pale walipokuwa Mtu 10 baada ya Mchezaji wao Markel Bergara alipotolewa kwa Kadi Nyekundu katika Dakika ya 84.

Hii ni mara ya kwanza tangu Mwaka 2003 kwa Real Sociedad kumaliza ndani ya 4 Bora.

Sasa Valencia, kwa kumaliza Nafasi ya 5, watacheza EUROPA LIGI Msimu ujao.

Katika vita ya kushuka Daraja iliyokuwa ikizikabili Timu 4, Real Zaragoza na Real Mallorca ziliungana na Deportivo La Coruna kushuka Daraja na Celta Vigo kunusurika baada ya kuifunga Espanyol Bao 1-0 kwa Bao la Natxo Insa.

Huko Santiago Bernabeu, katika Mechi iliyoanza mapema kupita zote, Real Madrid walimuaga Meneja wao Jose Mourinho kwa kuifunga Osasuna Bao 4-2.

Mourinho anaondoka Real baada ya kukaa hapo kwa Miaka mitatu.

Bao za Real Madrid zilifungwa na Gonzalo Higuain, Dakika ya 35, Michael Essien, 38, Karim Benzema, 69, na Jose Maria Callejon, 87.

Bao za Osasuna zilifungwa na Morales Roberto Torres, Dakika ya 52 na Alvaro Cejudo, 63.

Nao Mabingwa Barcelona waliifunga Malaga Bao 4-1 kwa Bao za David Villa, Francesc Fabregas, Martin Montoya na Andres Iniesta.

MSIMAMO:

**BINGWA: Barcelona


NA
TIMU

P
W
D
L
F
A
GD
PTS

1

FC Barcelona
38
32
4
2
115
40
75
100
2

Real Madrid CF
38
26
7
5
103
42
61
85
3

Atletico Madrid
38
23
7
8
65
31
34
76
4

Real Sociedad
38
18
12
8
70
49
21
66
5

Valencia
38
19
8
11
67
54
13
65
6

Malaga CF
38
16
9
13
53
50
3
57
7

Real Betis
38
16
8
14
57
56
1
56
8

Rayo Vallecano
38
16
5
17
50
66
-16
53
9

Sevilla FC
38
14
8
16
58
54
4
50
10

Getafe CF
38
13
8
17
43
57
-14
47
11

Levante
38
12
10
16
40
57
-17
46
12

Athletic Bilbao
38
12
9
17
44
65
-21
45
13

RCD Espanyol
38
11
11
16
43
52
-9
44
14

Real Valladolid
38
11
10
17
49
58
-9
43
15

Granada CF
38
11
9
18
37
54
-17
42
16

Osasuna
38
10
9
19
33
50
-17
39
17

Celta de Vigo
38
10
7
21
37
52
-15
37
18

Real Mallorca
38
9
9
20
43
72
-29
36
19

Deportivo
38
8
11
19
47
70
-23
35
20

Real Zaragoza
38
9
7
22
37
62
-25
34

**KUSHUKA DARAJA: Real Mallorca, Deportivo La Coruna & Real Zaragoza.

BAYERN YATWAA GERMAN DFB POKAL, YAWEKA REKODI!

BAYERN MUNICH 3 STUTTGART 2
BAYERN_MUNICH_LOGO


Mario Gomez alipiga Bao mbili na kuifanya Bayern Munich kuweka Historia ya kuwa Klabu ya kwanza ya Germany kutwaa ‘Trebo’ yaani, Ubingwa wa Nchi, Kombe la Nchi, hili DFB POKAL, na ule Ubingwa wa Ulaya, UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI kwenye Msimu mmoja, walipoifunga VfB Stuttgart 3-2 huko Berlin.

Hiyo ilikuwa Mechi ya mwisho kwa Kocha wa Bayern Jupp Heynckes ambae anastaafu na nafasi yake kuchukuliwa na aliekuwa Kocha wa FC Barcelona Pep Guardiola.

Mbali ya Bao 2 za Mario Gomez, Bao la kwanza la Bayern lilifungwa na Penati ya Thomas Mueller.


HISTORI:

-Bayern ni Timu ya kwanza ya Germany kutwaa Trebo ndani ya Msimu mmoja.

-Bayern inakuwa Klabu ya 7 Barani Ulaya kutwaa Trebo nyingine ni Celtic Mwaka 1967, Ajax 1972, PSV Eindhoven 1988, Manchester United 1999, Barcelona 2009 na Inter Milan hapo 2010.

**FAHAMU:
 Trebo ni kutwaa Ubingwa wa Ligi, Kombe kubwa la Nchi na Kombe la Ubingwa wa Ulaya ndani ya Msimu mmoja

 Bao za Stuttgart zilifungwa na Martin Harnick.

Huu ni ushindi wa 15 katika Mechi 16 walizocheza mwisho Bayern Munich na kipigo chao cha mwisho walikipata Oktoba Mwaka jana.