Klabu ya AC Milan inajaribu kuishawishi Real Madrid iwape
kiungo wao Kaka kwa mkopo kabla ya dirisha la usajili kufungwa ijumaa lakini
mabingwa hao wa LaLiga wanatilia mkazo na kusema kaka siyo wa mkopo bali ni wa
kuuzwa.
“Hali inaonyesha wazi kuwa Real wanataka kumuuza Kaka wakati
sisi tunamtaka mkwa mkopo.” Gilliani aliiambia Sky Sport .
“Kama Real wakabadilisha mawazo nitafanya haraka kumchukua
kwa mkopo”
Kocha wa Real Madrid,Jose Mourinho alimtema Kaka kwenye
kikosi kilichocheza mechi ya alhamisi ya Super cup ikiwa ni mzunguko wa kwanza
na Barcelona pale Nou Camp na mechi ya LaLiga na Getafeakisema kwamba mchezaji
huyu aliyewahi kuwa mchezaji bora wa dunia kwa mwaka wa 2007 kuwa hayupo
kwaenye mipango yake.
Mabingwa hao wa LaLiga wanakamilisha usajili wa kiungo Luca
Modric akitokea Tottenham ambaye amefanya Kaka asiwe kwenye mipango ya Mreno
huyo.
Kaka amekuwa akihusishwa na vyombo vya habari kuwa ataenda
Paris St. German ya Ligue1 Ufaransa, klabu ambayoinanolewa na boss wake wa
zamani pindi anakipiga katika klabu ya Milan Carlo Ancelotti.
No comments:
Post a Comment