Sunday, December 30, 2012

MKONGWE LAMPARD AIPAISHA CHELSEA NAFASI YA 3!!

BPL_LOGOFrank Lampard, Miaka 34, ambae mwishoni mwa Msimu Mkataba wake unamalizika na inadaiwa tayari hana nafasi Klabu hapo, leo alivaa utepe wa Nahodha na kuibeba Chelsea toka Goli 1 nyuma Uwanjani Goodison Park na yeye mwenyewe kupiga Bao mbili na kuwapa ushindi wa Bao 2-1, ukiwa ni ushindi wao wa kwanza kwa Miaka minne Uwanjani hapo.

Hi ilikuwa ni Mechi ya mwisho ya Ligi Kuu England kwa Mwaka 2012 kwa Klabu zote mbili ambazo zitacheza Mechi zao za Ligi zinazofuata hapo Januari 2, Mwaka 2013 kwa Chelsea kuikaribisha QPR Uwanjani Stamford Bridge na Everton kuwa ugenini huko St James Park kuivaa Newcastle.
++++++++++++

MAGOLI:

Everton 1
-Pienaar Dakika ya 2.

Chelsea 2
-Lampard Dakika ya 42 & 72
++++++++++++

Ushindi huu wa leo umeipaisha Chelsea kukamata nafasi ya 3 wakiwa Pointi 4 nyuma ya Timu ya Pili Manchester City huku wao wakiwa na Mechi moja mkononi.
+++++++++++++++++++++++

MSIMAMO-Timu za Juu:

=Tofauti ya Magoli inatajwa kwa Timu zilizofungana Pointi
1 Man United Mechi 20 Pointi 49
2 Man City Mechi 20 Pointi 42
3 Chelsea Mechi 19 Pointi 38
4 Tottenham Mechi 20 Pointi 36
5 Arsenal Mechi 19 Pointi 33 [Tofauti ya Magoli 18]
6 Everton Mechi 20 Pointi 33 [Tofauti ya Magoli 8]
7 WBA Mechi 20 Pointi 33 [Tofauti ya Magoli 3]
8 Stoke Mechi 20 Pointi 29
9 Swansea Mechi 20 Pointi 28
10 Liverpool Mechi 19 Pointi 25 [Tofauti ya Magoli 2]
+++++++++++++++++++++++

Ingawa Everton wamefungwa Mechi hii lakini walitoa upinzani mkubwa na wangeweza hata kushinda kwani Straika wao Nikica Jelavic alipiga posti na kukosa nafasi ya wazi mwishoni.

VIKOSI:

Everton: Howard, Jagielka, Heitinga, Distin, Baines, Naismith, Osman, Hitzlsperger, Pienaar, Anichebe, Jelavic.

Akiba: Mucha, Oviedo, Gueye, Barkley, Vellios, Duffy, Browning.
 
Chelsea: Cech, Azpilicueta, Ivanovic, Cahill, Cole, Ramires, Luiz, Lampard, Mata, Torres, Hazard.

Akiba: Turnbull, Oscar, Moses, Ferreira, Marin, Piazon, Ake.
 
Refa: Howard Webb
+++++++++++++++++++++++

RATIBA MECHI ZIJAZO:  

Jumapili 30 Desemba 2012
[SAA 1 Usiku]
QPR v Liverpool

Jumanne 1 Januari 2013
SAA 9 Dak 45 Mchana]
West Brom v Fulham

[SAA 12 Jioni]
Man City v Stoke
Swansea v Aston Villa
Tottenham v Reading
West Ham v Norwich
Wigan v Man United

[SAA 2 na Nusu Usiku] 
Southampton v Arsenal

Jumatano 2 Januari 2013 

[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Chelsea v QPR
Liverpool v Sunderland

[SAA 5 Usiku]
Newcastle v Everton

No comments:

Post a Comment