NGASSA ni ‘KISIRANI’ BALAA!
Timu
ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, leo imetoa burudani safi na zawadi
safi ya Krismasi na Mwaka mpya kwa Watanzania kwa kuwalaza Mabingwa wa
Afrika Zambia, maarufu kama Chipolopolo, kwa Bao 1-0 kwenye Mechi ya
Kirafiki ya Kimataifa iliyochezwa Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam.
Bao la ushindi lilifungwa na Mrisho Ngassa katika Dakika ya 44 baada ya kupokea krosi safi kutoka kwa Mwinyi Kazimoto.
Kwa ujumla, Taifa Stars, wanaofundishwa na Kim Poulsen, walicheza vizuri sana na uwezo wa kuongeza Mabao mengine ulikuwepo.
Zambia, chini ya Kocha Bora Afrika Herve
Renard, Kipindi cha Pili, waliongeza kasi na Mashambulizi lakini Stars
walisimama imara na kusafisha hatari zote huku Kipa Juma Kaseja akiwa
nguzo imara.
VIKOSI VILIVYOANZA:
TAIFA STARS: Juma
Kaseja, Erasto Nyoni, Shomari Kapombe, Aggrey Morris, Kevin Yondan,
Frank Domayo, Salum Abubakar, Mwinyi Kazimoto, Amri Kiemba, Mrisho
Ngassa, Khamis Mcha
ZAMBIA: Danny Munyao,
Chintu Kampamba, Hichani Himonde, Chisamba Lungu, James Chamanga, Moses
Phiri, Christopher Katongo, Felix Katongo, Nathan Sinkala, Rodrick
Kabwe, Isaac Chansa.
No comments:
Post a Comment