INAAMINIKA, kitu cha kwanza kabisa kwa
Meneja mpya wa Manchester United, David Moyes, ni kuimarisha Idara ya
Kiungo ya Timu hiyo ambayo Miaka nenda rudi ndio dhaifu kupita nyingine
na udhaifu huo unazidi baada ya kustaafu kwa Paul Scholes, kufifia kwa
Anderson, kutotabirika kwa Tom Cleverley na umri kuyoyoma kwa Michael
Carrick lakini ‘wakombozi’ wanatajwa kuwa ni Cesc Fabregas na Thiago
Alcantara wa Barcelona na Kevin Strootman wa PSV.
NANI WANAFAA NA NANI WATAPATIKANA?
Habari za ndani ya Barcelona zinasema
kuwa wao wako tayari kumuuza Cesc Fabregas ikiwa Klabu itafikia Dau la
Pauni Milioni 25 kiwango ambacho Man United wako tayari kulipa lakini
inaelekea Dau hilo linaweza kupanda baada ya Man City kutia mkono na wao
kuonyesha nia ya kumnunua Kiungo huyo mwenye akili ya mpira ambae
alikuwa Nahodha wa Arsenal.
Hata hivyo, Klabu hizo za Jijini
Manchester zinaweza tu kumnasa Fabregas, mwenye Miaka 26, ikiwa tu
Arsenal itatamka kuwa haitaki kumnunua kwa vile Mkataba wake wa kumuuza
kwa Barcelona una kipengele kuwa hawezi kuuzwa Klabu nyingine hadi
Arsenal ithibitishe haitaki kumnunua.
Zipo dalili Arsenal haitaki kumrudisha
Fabregas na kilichobaki ni Klabu ipi ya Manchester itamnasa ingawa
dalili zinaonyesha David Moyes ana nia kubwa ya kumfanya Fabregas kuwa
Mchezaji wake wa kwanza kumsaini ili aungane na mwenzake aliekuwa nae
Arsenal kwa muda mrefu, Robin van Persie.
Wengine wanaotazamwa na Man United
kuimarisha Kiungo ni Mchezaji Chipukizi wa Barcelona, Thiago Alcantara
na Nahodha wa PSV Kevin Strootman.
Wakati Alcantara ni ‘kinda’, Strootman
ni Mchezaji mrefu na mzoefu anaemudu pozisheni zote za Kiungo, iwe
Kiungo Mkabaji au Kiungo Mshambuliaji, kitu kinachomfanya awe na uhakika
wa kupata namba endapo atatua Old Trafford.
Kiungo gani atatua Old Trafford ndio
sakata linalosubiriwa kwa hamu kabla Msimu mpya kuanza hapo Agosti 11
kwa pambano la Fungua Pazia Msimu Mpya la kugombea Ngao ya Jamii kati ya
Mabingwa Man United na Mabingwa wa FA CUP Wigan.
No comments:
Post a Comment