Stoke City na klabu ya Arsenal wamebakia waiktafuta
ushindi wao wa kwanza katika ligi kuu baada ya kutoka sare ya mabao bila ya
kufungana.
Matokea hayo yamezifanya klabu ya Stoke kushika nafasi ya 11
na ile ya Arsenal kushika nafasi ya 12 katika msimamo wa ligi kuu England baada
ya timu zote kucheza mechi mbili.
Washika bunduki hao walipata nafasi nyingi sana lakini
kutokuwepo kwa RVP ambaya amesajiliwa na klabu ya Manchester United,
wakashindwakukwamisha mpira wavuni katika mechi yao ya piliambayo ya kwanza pia
ilikuwa droo.
"Pointi mbili katika mechi mbili za kwanza hazitoshi
kabisa" Kiungo wa Arsenal, Mikel Arteta alikiambia kituo ca televisheni
cha Sky Sports. "Tulihitaji pointi tatu lakini ilikuwa vigumu kwelikupata
hizo pointi tatu." Aliongezea. "Tulikuwa na nafasi nzuri lakini
hatukuzifanyia kazi kama ilivyotakiwa. Tulikuwa na nafasi nzuri ya kuchukua
pointi tatu leo lakini tumepoteza mbili. Ni subira tu kabla ya Olivier Giroud
na Lukas Podolski ambaoni wachezaji wapya kuzoea mfumo wa timu. Alimalizia
Arteta.
Liverpool ambao wapo katika nafasiza chini kwenye msimamo wa
ligi kuu England baada ya kichapo cha mabao 3-0 na West bromwich Albion
wikiendi iliyopita, wanaikaribisha Manchester City katika uwanja wa
anifield baadae.
No comments:
Post a Comment