Mtukutu Joey Barton alitumia akauntiyake ya twitter
kumdhihaki kocha wa QPR Mark Hughes akimwambia kwamba anataka kuihama klabu hiyo
na ke=wenda Olympique Marseille.
Barton 29 yupo katika kifungo cha mechi 12 baada ya kutolewa
nje ya uwanja kwa kufanya vurugu pale
alipomkwatua Sergio Aguero na kwenda kupandishiana na Vicent Kompany.
Kiungo huyo ambaye ana’followers’ 1.68 millioni, alitoa
hisia zake katika twiti 15 akisema, “ Moyowangu tayari upo katika uwanja wa
Marseille.”
Barton ambaye alijiunga na QPR akitokea Newcastle na kocha
aliyepita akimpa unahodha wa klabu hiyo.
“Sikuwahi hata siku moja kuongea maneno mabaya kwa mtu
yoyote. Mimi ni mwanaume. Nataka kuondoka. Nmesema inatosha kwa hapa.”
No comments:
Post a Comment