Samuel Eto’o amekataa nafasi ya kurudi kukipiga katika timu
yake ya taifa ya Cameroon na kusema kwamba timu hiyobado ina utawala mbovu.
Mshambuliaji huyo mwenye miaka 31 aliitwa wiki iliyopita kwa
ajili ya michuano ya African Cup of Nation round ya kwanza katiya Cameroon na
Cape Verde Septemba 8, miezi nane baada ya kusimamishwa baada ya kuwaongoza
wachezaji wenzake kufuatiwa na mgomo kwa sababu ya kutolipwa posho zao.
“Napenda kuwaambia kuwa nimeamua kutokuja kushiriki michuano
hiyona timu yangu ya taifa.” Eto’o aliandika kwenye barua aliyoituma kwa
shirikisho la mpira la Cameroon akiichapisha kwenye mtandao wake (www.samweletoo-officiel.com).
“Mazingira ya timu ya taifa bado yametawaliwa na utawala
mbovu ambao haufai kwa mahitaji ya viwango vya hali ya juu kwenye michezo.”
Aliongezea hivyo mshambuliajihuyo aliyewahi kuwa mchezaji bora wa Afrika mara
nne na akiichezea timu yake ya taifa zaidi ya mara 100.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa klabu ya Inter Milan na
Barcelona, kwa sasa anakipiga katika klabu tajiri kwenye ligi kuu ya Urusi ya Anzi Makhachkala.
Mechi kati ya Cameroon na Cape Verde itaamua nafasi ya
kushiriki fainali za AFCON 2013 huko kwa Madiba, Afrika kusini.
No comments:
Post a Comment