Wakati Barcelona ikishinda ugenini kwa
kuichapa Real Valladolidi Bao 3-1 kwa Bao za Xavi, Lionel Messi na
Tello, Real Madrid walichapwa 3-2 ugenini na Malaga ambao walifunga Bao
zao kupitia Isco na Santa, bao mbili, na Real kufunga kwa Bao za
Sanchez, kujifunga mwenyewe, na Karim Benzema.
Barcelona wamefunga Mwaka wakiwa
kileleni na wana Pointi 40, wakifuatiwa na Atletico Madrid wenye Pointi
40, Real Madrid 33 na Malaga 31.
Huko Italy kwenye Serie A, Inter Milan
walikosa nafasi ya kupunguza pengo lao na Mabingwa Juventus walio
kileleni wakiwa na Pointi 44 baada ya kutoka sare 1-1 na Genoa na
kujikuta wakiporomoka hadi nafasi ya 4.
Nafasi ya 2 imekamatwa na Lazio ambao waliwafunga Sampdoria 1-0 na Fiorentina kushika nafasi ya 3 baada ya kuifunga Palermo 3-0.
MATOKEO:
LA LIGA
Alhamisi Desemba 20
RCD Espanyol 2 Deportivo La Coruna 0
Real Sociedad 2 Sevilla 1
Rayo Vallecano 3 Levante 0
Ijumaa Desemba 21
Valencia 4 Getafe 2
Atletico Madrid 1 Celta Vigo 0
Jumamosi Desemba 22
Real Betis 1 Real Mallorca 2
Real Valladolid 1 FC Barcelona 3
Malaga 3 Real Madrid 2
Osasuna 1 Granada 2
Jumapili Desemba 23
Athletic Bilbao 0 Real Zaragoza 2 [IMECHEZWA JANA USIKU BAADA SAA 6]
**LIGI MAPUMZIKONI HADI JANUARI 6
MSIMAMO-Timu za Juu:
[Kila Timu imecheza Mechi 17]
1 Barcelona Pointi 49
2 Atletico Madrid 40
3 Real Madrid 33
4 Malaga 31
5 Real Betis 28
6 Levante 27
7 Real Sociedad 25
SERIE A
Ijumaa Desemba 21
Pescara 2 Catania 1
Cagliari 1 Juventus 3
Jumamosi Desemba 22
Inter Milan 1 Genoa 1
Atalanta 1 Udinese 1
Bologna 1 Parma 2
Torino FC 2 Chievo Verona 0
Sampdoria 0 SS Lazio 1
Siena 0 Napoli 2
Palermo 0 Fiorentina 3
AS Roma 4 AC Milan 2
**LIGI MAPUMZIKONI HADI JANUARI 6
MSIMAMO-Timu za Juu:
[Kila Timu imecheza Mechi 18]
1 Juventus Pointi 44
2 Lazio 36
3 Fiorentina 35
4 Inter Milan 35
5 Napoli 34
6 AS Roma 32
7 AC Milan 27
8 Parma 26
No comments:
Post a Comment