Saturday, December 22, 2012

Real yaaga Mwaka kwa kichapo, Barca yapaa, Inter yanasa!

BARCA_v_REALLIGI za Spain na Italy hapo jana ziliaga Mwaka 2012 kwa Mechi zao za mwisho na kwenda Vakesheni hadi Januari 6 huku Mabingwa wa Spain, Real Madrid, wakitandikwa kwenye La Liga na kutupwa Pointi 17 nyuma ya vinara Barcelona wakati huko Serie A Inter Milan walijikuta wakishushwa hadi nafasi ya 4 na Mabingwa Juventus kubaki kileleni Pointi 8 mbele.

Wakati Barcelona ikishinda ugenini kwa kuichapa Real Valladolidi Bao 3-1 kwa Bao za Xavi, Lionel Messi na Tello, Real Madrid walichapwa 3-2 ugenini na Malaga ambao walifunga Bao zao kupitia Isco na Santa, bao mbili, na Real kufunga kwa Bao za Sanchez, kujifunga mwenyewe, na Karim Benzema.

Barcelona wamefunga Mwaka wakiwa kileleni na wana Pointi 40, wakifuatiwa na Atletico Madrid wenye Pointi 40, Real Madrid 33 na Malaga 31.

Huko Italy kwenye Serie A, Inter Milan walikosa nafasi ya kupunguza pengo lao na Mabingwa Juventus walio kileleni wakiwa na Pointi 44 baada ya kutoka sare 1-1 na Genoa na kujikuta wakiporomoka hadi nafasi ya 4.

Nafasi ya 2 imekamatwa na Lazio ambao waliwafunga Sampdoria 1-0 na Fiorentina kushika nafasi ya 3 baada ya kuifunga Palermo 3-0.
MATOKEO:

LA LIGA
Alhamisi Desemba 20
RCD Espanyol 2 Deportivo La Coruna 0
Real Sociedad 2 Sevilla 1
Rayo Vallecano 3 Levante 0
Ijumaa Desemba 21
Valencia 4 Getafe 2
Atletico Madrid 1 Celta Vigo 0
Jumamosi Desemba 22
Real Betis 1 Real Mallorca 2
Real Valladolid 1 FC Barcelona 3
Malaga 3 Real Madrid 2
Osasuna 1 Granada 2
Jumapili Desemba 23
Athletic Bilbao 0 Real Zaragoza 2 [IMECHEZWA JANA USIKU BAADA SAA 6]
**LIGI MAPUMZIKONI HADI JANUARI 6

MSIMAMO-Timu za Juu:
[Kila Timu imecheza Mechi 17]
1 Barcelona Pointi 49
2 Atletico Madrid 40
3 Real Madrid 33
4 Malaga 31
5 Real Betis 28
6 Levante 27
7 Real Sociedad 25

SERIE A
Ijumaa Desemba 21
Pescara 2 Catania 1
Cagliari 1 Juventus 3
Jumamosi Desemba 22
Inter Milan 1 Genoa 1
Atalanta 1 Udinese 1
Bologna 1 Parma 2
Torino FC 2 Chievo Verona 0
Sampdoria 0 SS Lazio 1
Siena 0 Napoli 2
Palermo 0 Fiorentina 3
AS Roma 4 AC Milan 2
**LIGI MAPUMZIKONI HADI JANUARI 6

MSIMAMO-Timu za Juu:
[Kila Timu imecheza Mechi 18]
1 Juventus Pointi 44
2 Lazio 36
3 Fiorentina 35
4 Inter Milan 35
5 Napoli 34
6 AS Roma 32
7 AC Milan 27
8 Parma 26

No comments:

Post a Comment