Manager wa Manchester United Sir Alex
Ferguson amewakataza wachezaji wenye umri wa klabu hiyo kuendesha magari
ya kifahari kutoka kwa mdhamini wao mpya Chevrolet.
United hivi
karibuni walisaini mkataba wa mamilioni ya paundi na kampuni hiyo kubwa
ya kutengeneza magari kutoka Marekani, na watakuwa wadhamini wao rasmi
wa jezi kuanzia msimu wa 2014-15.
Kama kuonyesha ishara ya
urafiki mzuri mpya wa kibiashara baina yao na United, Chevrolet kwa
haraka walitoa ofa kwa wachezaji wa kikosi cha kwanza cha United
kuchagua magari ya kifahari wayatakayo na wangepewa bure na vijana wengi
wakaagiza magari aina ya Iconic Corvettes.
Ingawa inasemekana Ferguson akaingilia
kati na kuweka sheria kwamba vijana wa chini ya miaka 23 - haijalishi
wana ukubwa na umuhimu gani kwenye timu - hawatoruhusiwa kutoa oda ya
aina hiyo ya gari la kifahari.
Kwa maana hiyo wachezaji kama Danny
Welbeck, 21, Phili Jones 20, Chris Smalling 22, na Rafael 22, na wengine
kibao hawatoruhusiwa kuendesha magari ya kifahari ya ofa kutoka
Chevrolet aambayo yatakuwa hayajapata baraka kutoka kwa Mzee Fergie.
Uamuzi
huu wa Ferguson unalenga kuhakikisha vijana wake wadogo hawavimbi
vichwa na kujisahau isivyostahili. Pia hii sio mara ya kwanza kwa Fergie
kufanya kitendo kama hiki, miaka miwili iliyopita alitoa katazo kwa
vijana wa timu ya watoto kutovaa viatu vya bei mbaya hasa vya rangi.
No comments:
Post a Comment