BAYERN YATAKA HISTORIA YA TREBO, BRAZIL YAWATIBUA!!
BAADA ya kutwaa Ubingwa wa Bundesliga na UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, Bayern Munich wana nafasi ya kuweka historia hapo Jumamosi ya kuwa Klabu ya kwanza ya Kijerumani kutwaa ‘TREBO’ ikiwa wataifunga VfB Stuttgart kwenye Fainali ya German Cup, maarufu kama German DFB Pokal, lakini azma hiyo imeingia dosari baada ya Brazil kuzuia baadhi ya Wachezaji wao kuichezea Klabu yao.
Mzozo huu umemfanya Mwenyekiti wa Bayern
Munich, Karl-Heinz Rummenigge, apandishe na kudai hilo halikubaliki
baada ya Shirikisho la Soka la Brazil, CBF, kuwazuia Wachezaji wa Bayern
Munich, Kiungo Gustavo na Sentahafu Dante, kutocheza Fainali hiyo na
badala yake kutakiwa kuripoti Kambini Nchini Brazil Siku ya Alhamisi
kuanza maandalizi ya Nchi hiyo kwa ajili ya Mashindano ya FIFA ya Kombe la Mabara yanayoanza kuchezwa Juni 15 Nchini Brazil.
Juni 2, Brazil watacheza Mechi ya Kirafiki na England Uwanja wa Maracana Jijini Rio De Janeiro.
Rummenigge amedai Wachezaji hao wa
Brazil wametishwa kwamba hawatachukuliwa tena kuichezea Brazil
wakichelewa kupiga ripoti Kambini.
Wakati Bayern wanadai huo ni ukatili,
CBF, kupitia Mkurugenzi wao wa Ufundi, Carlos Alberto Parreira, amesema
wao waliwapelekea DFB Barua yenye heshima ya kuelezea msimamo wao.
Hata hivyo Rummenigge
amekiri wenye makosa ni wao wenyewe Germany, hasa Shirikisho la Soka,
DFB, kwa kuipanga Fainali ya German DFB Pokal kuwa Juni 1, tarehe ambayo
ipo kwenye Kalenda ya FIFA ya Mechi za Kimataifa.
No comments:
Post a Comment