Usiku wa kumakia leo Jose Mourinho alikiongoza kikosi chake cha Real Madrid kuwafunga mahasimu wao wakubwa FC Barcelona bao 2-1 kwenye mchezo wa pili wa kogembea kombe la Supercup kwenye uwanja wa Santiago Bernebeu. Kwa matokeo hayo timu hizo zikafunga kwa jumla ya mabao 4-4, lakini kutoka na Madrid kuwa na idadi kubwa ya magoli ya ugenini wakatwaa ubingwa huo wa tatu tangu Mourinho afike Bernebeu.
Kwa maana hiyo baada ya kufanikiwa
kutwaa uchampion huo wa Supercup, Mourinho anaweka historia nyingine
kubwa duniani akiwa ndio kocha pekee kuwahi kutwaa makombe ya ligi na
supercup - (ambalo hukutanisha bingwa wa ligi na bingwa wa kombe la FA
ya nchi husika -au mshindi wa pili wa ligi) katika nchi nne tofauti
zilizo juu kwenye viwango vya FIFA - England alichukua EPL na Community
shield, Ureno walifanya hivyo hivyo, Italia pia na sasa Spain.
No comments:
Post a Comment