Monday, December 24, 2012

Chelsea yarudi Ligi kwa Kishindo cha 8-0, Man United yabanwa!!

FERGIE ATAKA WILLIAMS AFUNGIWE!!!
 BPL_LOGO
Baada ya kushindwa kutwaa Ubingwa wa Dunia huko Japan kwa kufungwa Fainali na Corinthians na jana kujikuta wakiporomoshwa hadi nafasi ya 7, leo Chelsea wamerudi kwa kishindo kwenye Ligi Kuu England na kutwaa tena nafasi yao ya 3 walipoishindilia Aston Villa Bao 8-0 Uwanjani Stamford Bridge na mapema, vinara Manchester United, walitoka sare ya 1-1 na Swansea City huko Liberty Stadium.
DONDOO FUPI za MECHI HIZO:
CHELSEA 8 ASTON VILLA 0
Chelsea leo wakicheza kwao Uwanja wa Stamford Bridge wamerejea kwenye nafasi ya 3 baada ya kuishindilia Aston Villa Bao 8-0.
++++++++++++++++
WAFUNGAJI:
-Torres Dakika ya 3
-Luiz 29
-Ivanovic 34
-Lampard 58
-Ramires 75 & 90
-Oscar 79 (Penati)
-Hazard 83
Aston Villa 0
++++++++++++++++
Mbali ya kufunga Goli hizo 8 Chelsea pia walikosa Penati baada ya Chipukizi toka Brazil, Piazon, kuipiga na Kipa Guzan kuipanchi.
VIKOSI:
Chelsea: Cech, Azpilicueta, Ivanovic, Cahill, Cole, Luiz, Lampard, Moses, Mata, Hazard, Torres
Akiba: Turnbull, Ramires, Oscar, Ferreira, Marin, Piazon, Ake.
Aston Villa: Guzan, Herd, Clark, Baker, Lowton, Bannan, Westwood, Lichaj, Weimann, Holman, Benteke
Akiba: Given, Ireland, El Ahmadi, Albrighton, Delph, Bowery, Bennett.
Refa: Phil Dowd
SWANSEA 1 MAN UNITED 1
Manchester United bado wapo kileleni mwa Ligi Kuu England kwa Pointi 4 mbele ya Mahasimu wao Man City licha ya leo kutoka sare ya Bao 1-1 na Swansea City Uwanjani Liberty.
Man United walitangulia kufunga kwa Bao la kichwa la Patrice Evra kufuatia kona ya Robin van Persie katika Dakika ya 16 lakini Swansea walisawazisha katika Dakika ya 29 kwa Bao la Michu baada ya shuti la Jonathan De Guz kutemwa na Kipa De Gea na kutua kirahisi miguuni mwa Michu.
Kipindi cha Pili Man United walikosa Bao nyingi pamoja na mbili zilizogonga mwamba  lakini tukio ambalo huenda likaleta mjadala ni pale Robin van Persie alipofanyiwa faulo na Refa kupiga Filimbi lakini Beki wa Swansea, Williams, akaupiga mpira kwa nguvu na kumbabatiza kichwani Van Persie wakati akiwa amelala chini na Van Persie akapandwa na jazba na kuanza kuvutana na Williams.
Refa Michael Oliver aliwapa Kadi za Njano Wachezaji wote hao wawili lakini Sir Alex Ferguson ametaka FA ichukue hatua zaidi kwa Williams ambae alidai angeweza kumvunja shingo Van Persie.
VIKOSI:
Swansea: Vorm, Tiendalli, Chico, Williams, Davies, Dyer, Britton, Agustien, de Guzman, Routledge, Michu
Akiba: Tremmel, Graham, Monk, Shechter, Moore, Ki, Richards.
Man United: De Gea, Jones, Evans, Vidic, Evra, Valencia, Carrick, Cleverley, Young, Rooney, van Persie
Akiba: Lindegaard, Giggs, Hernandez, Welbeck, Scholes, Fletcher, Buttner.
Refa: Michael Oliver
+++++++++++++++++++++++
MSIMAMO:
=Tofauti ya Magoli inatajwa kwa Timu zilizofungana Pointi
1 Man United Mechi 18 Pointi 43
2 Man City Mechi 18 Pointi 39
3 Chelsea Mechi 17 Pointi 32
4 Arsenal Mechi 18 Pointi 30 [Tofauti ya Magoli 14]
5 Everton Mechi 18 Pointi 30 [Tofauti ya Magoli 8]
6 Tottenham Mechi 18 Pointi 30 [Tofauti ya Magoli 5]
7 WBA Mechi 18 Pointi 30 [Tofauti ya Magoli 4]
8 Liverpool Mechi 18 Pointi 25 [Tofauti ya Magoli 4]
9 Stoke Mechi 18 Pointi 25 [Tofauti ya Magoli 2]
10 Norwich Mechi 18 Pointi 25 [Tofauti ya Magoli -7]
11 Swansea Mechi 18 Pointi 24
12 West Ham Mechi 18 Pointi 23
13 Fulham Mechi 18 Pointi 20 [Tofauti ya Magoli -5]
14 Newcastle Mechi 18 Pointi 20 [Tofauti ya Magoli -6]
15 Sunderland Mechi 18 Pointi 19
16 Aston Villa Mechi 18 Pointi 18
17 Southampton Mechi 17 Pointi 15 [Tofauti ya Magoli -10]
===============
18 Wigan Mechi 18 Pointi 15 [Tofauti ya Magoli -15]
19 QPR Mechi 18 Pointi 10
20 Reading Mechi 18 Pointi 9
+++++++++++++++++++++++++++
RATIBA:
Jumatano 26 Desemba 2012
[SAA 12 Jioni]
Arsenal v West Ham
Everton v Wigan
Fulham v Southampton
Man United v Newcastle
Norwich v Chelsea
QPR v West Brom
Reading v Swansea
Sunderland v Man City
[SAA 2 na Nusu Usiku]
Aston Villa v Tottenham
[SAA 4 Dak 45 Usiku]
Stoke v Liverpool

No comments:

Post a Comment