Saturday, December 29, 2012

MEIRELES APUNGUZIWA ADHABU YA KUFUNGIWA MECHI 11 MPAKA MECHI 4 - YATHIBITIKA HAKUMTEMEA MATE MWAMUZI!!


Mchezaji wa zamani wa Liverpool na Chelsea kiungo Raul Meireles amepata nafuu ya kupunguziwa adhabu ya kutocheza mechi 11 mpaka kufikia mechi 4.
Mchezaji huyo wa Fenerbahce, 29, alikata rufaa baada ya kuhukumiwa kwa kosa la kumtemea mate mwamuzi kufuatiwa kupewa kadi nyekundu katika mechi ya iliyowakutanaisha mahasimu wao ligi ya Uturuki klabu ya Galatasary.

Shirikisho la soka la Uturuki limesema ilikuwa ni vigumu kwa mchezaji kutema mate kwa kuwa alikuwa anaongea wakati wote wa tukio hilo, hata hivyo bado atakabiliwa na adhabu ya kukosa mechi nne kwa kumtukana mwamuzi.

No comments:

Post a Comment