Falcao, Raia wa Colombia mwenye Miaka 27, amekuwa pia akihusishwa na kuhamia Chelsea na Manchester City.
FALCAO-WASIFU:
-KUZALIWA: 10 Februari 1986
-URAIA: Colombia
-KLABU: River Plate (2005-2009); Porto (2009-2011) & Atletico Madrid (2011-2013)
-ATLETICO MADRID: Mechi 46 Magoli 35
-JE WAJUA? Falcao ndie Mchezaji wa kwanza kwenye UEFA SUPER CUP kupiga
Hetitriki Mwezi Septemba Mwaka jana Atletico Madrid walipoinyuka Chelsea 4-1.
Falcao
amesaini Mkataba wa Miaka mitano na Monaco na usajili huo umelipiwa na
Mmiliki wa Klabu hiyo, Dmitry Rybolovlev, Bilionea kutoka Urusi.
Akitangaza usajili huo, Rybolovlev
alisema: “Ni fahari kubwa kumsaini mmoja wa Wachezaji bora Duniani na
tuna imani ataisaidia Monaco!”
Wakiwa chini ya Kocha Claudio Ranieri,
Msimu huu uliokwisha juzi waliibuka Mabingwa wa Daraja la Pili huko
France na Msimu ujao watacheza Daraja la juu Ligue 1 na hali hiyo
imewafanya waimarishe Kikosi chao na tayari wameshawasajili Wachezaji
wawili hatari toka FC Porto, Joao Moutinho, Miaka 26, na James
Rodriguez, Miaka 21, na pia Beki Mkongwe kutoka Real Madrid, Ricardo
Carvalho, ambae amehamishwa bure baada kumaliza Mkataba wake.
No comments:
Post a Comment