DAVID MOYES amekiri hakuwa anajua kama Sir Alex Ferguson atastaafu Manchester United na yeye kuteuliwa kuwa Meneja huko lakini alipopewa ofa hakusita hata Sekunde moja.
Moyes amesema hatua hii ni kama ile alipotoka Preston North End Mwaka 2002 na kutua Everton.
Ametamka: “Nasikitika kuondoka Klabu
safi kama Everton ambayo imekuwa sehemu ya maisha yangu lakini ukweli
siwezi kuikataa ofa ya Man United!”
Ingawa Mkataba wake na Everton ulikuwa
ukimalizika Juni 30, David Moyes alithibitisha hakuwa na mipango ya
kuhama na alikuwa tayari yeye na Mwenyekiti wa Everton, Bill Kenwright,
walikuwa wameshaandaa mipango ya Msimu ujao.
Moyes pia alimzungumzia Mtu
atakaemrithi, Sir Alex Ferguson, na kutamka: “Hakuna Mtu aliefikiria ipo
Siku Sir Alex Ferguson atastaafu. Tulidhani yeye ni Binadamu wa ajabu.
Yeye ni mfano kwa kila Mtu. Heshima yangu kwake haielezeki. Tumetoka
zama tofauti. Nimekua nikimwona yeye na Jock Stein ni Mashujaa, baadae
nikashindana na Sir Alex. Sina neno lolote ala kumwelezea ambalo
litamtendea haki Sir Alex Ferguson!’
Pia Moyes alizungumzia Mechi yake ya
mwisho akiwa Meneja wa Everton Uwanja wa Nyumbani Goodison Park ambako
Jumapili hii watacheza na Newcastle na kusema anatumaini Mashabiki
watatoa heshima kama ile ya Siku ya kwanza yeye kutua hapo.
Mechi ya mwisho kabisa kwa David Moyes akiwa Meneja wa Everton ni hapo Mei 19 watakapocheza ugenini Stamford Bridge na Chelsea.
BPL: BARCLAYS PREMIER LEAGUE
RATIBA
Jumamosi Mei 11
[Saa 8 Dak 45 Mchana]
Aston Villa v Chelsea
Jumapili Mei 12
[Saa 9 na Nusu Mchana]
Stoke v Tottenham
[Saa 11 Jioni]
Everton v West Ham
Fulham v Liverpool
Norwich v West Brom
QPR v Newcastle
Sunderland v Southampton
[Saa 12 Jioni]
Man United v Swansea
Jumanne Mei 14
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Arsenal v Wigan
[Saa 4 Usiku]
Reading v Man City
Jumapili 19 Mei
MECHI ZA MWISHO ZA LIGI MSIMU HUU
[Saa 12 Jioni]
Chelsea v Everton
Liverpool v QPR
Man City v Norwich
Newcastle v Arsenal
Southampton v Stoke
Swansea v Fulham
Tottenham v Sunderland
West Brom v Man United
West Ham v Reading
Wigan v Aston Villa
MSIMAMO:
FAHAMU: BINGWA TAYARI NI MANCHESTER UNITED!!
NA |
TIMU |
P |
GD |
PTS |
1 |
Man Utd |
36 |
42 |
85 |
2 |
Man City |
36 |
31 |
75 |
3 |
Chelsea |
36 |
34 |
69 |
4 |
Arsenal |
36 |
31 |
67 |
5 |
Tottenham |
36 |
18 |
66 |
6 |
Everton |
36 |
14 |
60 |
7 |
Liverpool |
36 |
25 |
55 |
8 |
West Brom |
36 |
0 |
48 |
9 |
Swansea |
36 |
0 |
46 |
10 |
West Ham |
36 |
-8 |
43 |
11 |
Stoke |
36 |
-10 |
41 |
12 |
Fulham |
36 |
-11 |
40 |
13 |
Aston Villa |
36 |
-21 |
40 |
14 |
Southampton |
36 |
-11 |
39 |
15 |
Sunderland |
36 |
-12 |
38 |
16 |
Norwich |
36 |
-22 |
38 |
17 |
Newcastle |
36 |
-23 |
38 |
18 |
Wigan |
36 |
-23 |
35 |
19 |
Reading |
36 |
-26 |
28 |
20 |
QPR |
36 |
-28 |
25 |
*QPR & READING TAYARI ZIMESHUKA DARAJA!
No comments:
Post a Comment