Friday, May 10, 2013

MOYES AFUNGUKA, NI WIKI HII TU ALIJUA SAFARI OLD TRAFFORD!

ASEMA OFA YA MAN UNITED HUWEZI KUIKATAA!!

MOYES_nFERGIE-NDEFU
DAVID MOYES amekiri hakuwa anajua kama Sir Alex Ferguson atastaafu Manchester United na yeye kuteuliwa kuwa Meneja huko lakini alipopewa ofa hakusita hata Sekunde moja.

Moyes amesema hatua hii ni kama ile alipotoka Preston North End Mwaka 2002 na kutua Everton.

Ametamka: “Nasikitika kuondoka Klabu safi kama Everton ambayo imekuwa sehemu ya maisha yangu lakini ukweli siwezi kuikataa ofa ya Man United!”

Ingawa Mkataba wake na Everton ulikuwa ukimalizika Juni 30, David Moyes alithibitisha hakuwa na mipango ya kuhama na alikuwa tayari yeye na Mwenyekiti wa Everton, Bill Kenwright, walikuwa wameshaandaa mipango ya Msimu ujao.

Moyes pia alimzungumzia Mtu atakaemrithi, Sir Alex Ferguson, na kutamka: “Hakuna Mtu aliefikiria ipo Siku Sir Alex Ferguson atastaafu. Tulidhani yeye ni Binadamu wa ajabu. Yeye ni mfano kwa kila Mtu. Heshima yangu kwake haielezeki. Tumetoka zama tofauti. Nimekua nikimwona yeye na Jock Stein ni Mashujaa, baadae nikashindana na Sir Alex. Sina neno lolote ala kumwelezea ambalo litamtendea haki Sir Alex Ferguson!’

Pia Moyes alizungumzia Mechi yake ya mwisho akiwa Meneja wa Everton Uwanja wa Nyumbani Goodison Park ambako Jumapili hii watacheza na Newcastle na kusema anatumaini Mashabiki watatoa heshima kama ile ya Siku ya kwanza yeye kutua hapo.

Mechi ya mwisho kabisa kwa David Moyes akiwa Meneja wa Everton ni hapo Mei 19 watakapocheza ugenini Stamford Bridge na Chelsea.

BPL: BARCLAYS PREMIER LEAGUE

RATIBA

Jumamosi Mei 11
[Saa 8 Dak 45 Mchana]
Aston Villa v Chelsea

Jumapili Mei 12
[Saa 9 na Nusu Mchana]
Stoke v Tottenham

[Saa 11 Jioni]
Everton v West Ham
Fulham v Liverpool
Norwich v West Brom
QPR v Newcastle
Sunderland v Southampton

[Saa 12 Jioni]
Man United v Swansea

Jumanne Mei 14
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Arsenal v Wigan

[Saa 4 Usiku]
Reading v Man City

Jumapili 19 Mei

MECHI ZA MWISHO ZA LIGI MSIMU HUU 

[Saa 12 Jioni]
Chelsea v Everton
Liverpool v QPR
Man City v Norwich
Newcastle v Arsenal
Southampton v Stoke
Swansea v Fulham
Tottenham v Sunderland
West Brom v Man United
West Ham v Reading
Wigan v Aston Villa


MSIMAMO:

FAHAMU: BINGWA TAYARI NI MANCHESTER UNITED!!

NA
TIMU
P
GD
PTS


1
Man Utd
36
42
85

2
Man City
36
31
75

3
Chelsea
36
34
69

4
Arsenal
36
31
67

5
Tottenham
36
18
66

6
Everton
36
14
60

7
Liverpool
36
25
55

8
West Brom
36
0
48

9
Swansea
36
0
46

10
West Ham
36
-8
43

11
Stoke
36
-10
41

12
Fulham
36
-11
40

13
Aston Villa
36
-21
40

14
Southampton
36
-11
39

15
Sunderland
36
-12
38

16
Norwich
36
-22
38

17
Newcastle
36
-23
38

18
Wigan
36
-23
35

19
Reading
36
-26
28

20
QPR
36
-28
25

*QPR & READING TAYARI ZIMESHUKA DARAJA!

No comments:

Post a Comment