BRAZIL KUTUMIA MECHI KWA MATAYARISHO KOMBE LA MABARA!
June 2, Saa 4 Usiku Bongo Taimu
Estadio Jornalista Mário Filho (Maracanã)
Rio de Janeiro
Brazil
BAADA kunusurika kufutwa, Mechi ya Timu
za Taifa za Brazil na England itachezwa leo Usiku huko Mjini Rio De
Janeiro kwenye Uwanja wa Maracana, ambao Jina lake rasmi ni Estadio
Jornalista Mário Filho, ikiwa ni ufunguzi rasmi wa Uwanja huo
uliofanyiwa ukarabati mkubwa.
Juzi, Jaji mmoja aliamua Mechi hiyo
isichezwe baada ya Uwanja huo kutotimiza masharti ya usalama lakini
baadae uamuzi huo ukafutwa baada ya Rufaa.
Tangu ufanyiwe ukarabati tayari Mechi
moja ya maonyesho imeshachezwa iliyowahusisha Mastaa wa zamani wakati
Manguli wa Brazil, Ronaldo na Bebeto, walipoongoza Timu tofauti hapo
Aprili 27 na kushuhudiwa na Watazamaji Elfu 25.
Maracana, ambayo iliwahi kupakia
Watazamaji hadi 200,000, ilijengwa kwa ajili ya Fainali za Kombe la
Dunia za Mwaka 1950 ambayo Wenyeji Brazil walifungwa kwenye Fainali yake
Bao 2-1 na Uruguay waliotwaa Ubingwa wa Dunia.
Kwa mara nyingine tena, Maracana
itachezwa Fainali ya Kombe la Dunia hapo Mwaka 2014 wakati Brazil
watakapokuwa Wenyeji na Uwanja huo utachukua Washabiki 78,838 wote
wakiwa wamekaa Vitini.
MECHI ZA BRAZIL v ENGLAND UWANJA wa MARACANA:
Brazil na England zilikutana mara ya kwanza Uwanja wa Wembley Mwaka 1956.
Mechi 11 zilichezwa Uwanja wa Wembley na
nyingine huko Gothenburg, Vina Del Mar, Guadalajara, Los Angeles,
Washington, Paris, Shizuoka na Doha.
Zifuatazo ni Mechi zao 5 walizocheza Maracana:
-Mei 13 1959 - Brazil 2 England 0 - Watazamaji: 200,000
-Mei 30 1964 - Brazil 5 England 1 - Watazamaji: 110,000
-Juni 12 1969 - Brazil 2 England 1 - Watazamaji: 125,000
-Juni 8 1977 - Brazil 0 England 0 - Watazamaji: 77,000
-Juni 10 1984 - Brazil 0 England 2 – Watzamaji: 56,126
JUMLA: Brazil 11 England 4 Sare 9
Mara ya mwisho kwa England kucheza Maracana ilikuwa ni Mwaka 1984 walipocheza Mechi ya Kirafiki na kuifunga Brazil Bao 2-0.
Katika Mechi hiyo, mmoja wa Wachezaji
alikuwa ni Mark Chamberlain, Baba Mzazi wa Mchezaji wa Arsenal, Alex
Oxlade-Chamberlain, ambae leo anatarajiwa kuichezea England na kufuata
nyayo za Baba yake.
Hivi Juzi, England, ilicheza Uwanjani
Wembley na kutoka sare 1-1 na Republic of Ireland na kupondwa na wengi
lakini Meneja wao, Roy Hodgson, ameponda msimamo huo na kudai Timu yake
ipo kwenye hali nzuri.
Nao, Brazil, chini ya Meneja Luiz Felipe Scolari, wataitumia Mechi hii kama ya kupasha moto ushiriki wao kwenye Mashindano ya FIFA, Kombe la Mabara, yatakayochezwa Nchini Brazil kuanzia Juni 15 hadi 30.
VIKOSI VINATARAJIWA:
BRAZIL:
Cesar
Alves, Thiago Silva, David Luiz, Marcelo
Fernando, Paulinho
Neymar, Oscar, Moura
Fred
ENGLAND:
Hart
Johnson, Cahill Jagielka, Cole
Carrick, Milner
Oxlade-Camberlain, Lampard, Walcott
Rooney
Refa: W. Roldán
No comments:
Post a Comment