Real Sociedad wameipiku Valencia na kutwaa nafasi ya mwisho ya Spain kucheza UCL, UEFA CHAMPIONZ LIGI, Msimu ujao walipocheza ugenini na kuifunga Bao 1-0 Deportivo La Coruna kipigo kilichowashusha Daraja huku Jose Mourinho akiaga kwa Timu yake Real Madrid kuifunga Osasuna Bao 4-2 Uwanjani Santiago Bernabeu.
Valencia, walikuwa Pointi 2 mbele ya
Real Sociedad kabla Mechi za mwisho za La Liga kuchezwa hiyo jana,
lakini wakaambua kipigo cha 4-3 toka kwa Sevilla na ushindi wa Sociedad
umewatupa nje ya UCL, Valencia.
Timu nyingine zitakazoiwakilisha Spain
kwenye UCL Msimu ujao ni Mabingwa FC Barcelona, Timu ya Pili, Real
Madrid, na Atletico Madrid iliyomaliza nafasi ya 3.
LA LIGA-MECHI ZA MWISHO ZA MSIMU
MATOKEO:
Real Madrid CF 4 Osasuna 2
FC Barcelona 4 Malaga CF 1
Celta de Vigo 1 RCD Espanyol 0
Deportivo La Coruna 0 Real Sociedad 1
Real Mallorca 4 Real Valladolid 2
Rayo Vallecano 2 Athletic de Bilbao 2
Sevilla FC 4 Valencia 3
Real Zaragoza 1 Atletico de Madrid 3
Levante 1 Real Betis 1
Granada CF 2 Getafe CF 0
Bao la ushindi kwa Real Sociedad
lilifungwa na Antoine Griezmann katika Dakika ya 22 na walimudu
kulilinda hata pale walipokuwa Mtu 10 baada ya Mchezaji wao Markel
Bergara alipotolewa kwa Kadi Nyekundu katika Dakika ya 84.
Hii ni mara ya kwanza tangu Mwaka 2003 kwa Real Sociedad kumaliza ndani ya 4 Bora.
Sasa Valencia, kwa kumaliza Nafasi ya 5, watacheza EUROPA LIGI Msimu ujao.
Katika vita ya kushuka Daraja iliyokuwa
ikizikabili Timu 4, Real Zaragoza na Real Mallorca ziliungana na
Deportivo La Coruna kushuka Daraja na Celta Vigo kunusurika baada ya
kuifunga Espanyol Bao 1-0 kwa Bao la Natxo Insa.
Huko Santiago Bernabeu, katika Mechi
iliyoanza mapema kupita zote, Real Madrid walimuaga Meneja wao Jose
Mourinho kwa kuifunga Osasuna Bao 4-2.
Mourinho anaondoka Real baada ya kukaa hapo kwa Miaka mitatu.
Bao za Real Madrid zilifungwa na Gonzalo
Higuain, Dakika ya 35, Michael Essien, 38, Karim Benzema, 69, na Jose
Maria Callejon, 87.
Bao za Osasuna zilifungwa na Morales Roberto Torres, Dakika ya 52 na Alvaro Cejudo, 63.
Nao Mabingwa Barcelona waliifunga Malaga Bao 4-1 kwa Bao za David Villa, Francesc Fabregas, Martin Montoya na Andres Iniesta.
MSIMAMO:
**BINGWA: Barcelona
NA |
TIMU |
P |
W |
D |
L |
F |
A |
GD |
PTS |
1 |
FC Barcelona |
38 |
32 |
4 |
2 |
115 |
40 |
75 |
100 |
2 |
Real Madrid CF |
38 |
26 |
7 |
5 |
103 |
42 |
61 |
85 |
3 |
Atletico Madrid |
38 |
23 |
7 |
8 |
65 |
31 |
34 |
76 |
4 |
Real Sociedad |
38 |
18 |
12 |
8 |
70 |
49 |
21 |
66 |
5 |
Valencia |
38 |
19 |
8 |
11 |
67 |
54 |
13 |
65 |
6 |
Malaga CF |
38 |
16 |
9 |
13 |
53 |
50 |
3 |
57 |
7 |
Real Betis |
38 |
16 |
8 |
14 |
57 |
56 |
1 |
56 |
8 |
Rayo Vallecano |
38 |
16 |
5 |
17 |
50 |
66 |
-16 |
53 |
9 |
Sevilla FC |
38 |
14 |
8 |
16 |
58 |
54 |
4 |
50 |
10 |
Getafe CF |
38 |
13 |
8 |
17 |
43 |
57 |
-14 |
47 |
11 |
Levante |
38 |
12 |
10 |
16 |
40 |
57 |
-17 |
46 |
12 |
Athletic Bilbao |
38 |
12 |
9 |
17 |
44 |
65 |
-21 |
45 |
13 |
RCD Espanyol |
38 |
11 |
11 |
16 |
43 |
52 |
-9 |
44 |
14 |
Real Valladolid |
38 |
11 |
10 |
17 |
49 |
58 |
-9 |
43 |
15 |
Granada CF |
38 |
11 |
9 |
18 |
37 |
54 |
-17 |
42 |
16 |
Osasuna |
38 |
10 |
9 |
19 |
33 |
50 |
-17 |
39 |
17 |
Celta de Vigo |
38 |
10 |
7 |
21 |
37 |
52 |
-15 |
37 |
18 |
Real Mallorca |
38 |
9 |
9 |
20 |
43 |
72 |
-29 |
36 |
19 |
Deportivo |
38 |
8 |
11 |
19 |
47 |
70 |
-23 |
35 |
20 |
Real Zaragoza |
38 |
9 |
7 |
22 |
37 |
62 |
-25 |
34 |
**KUSHUKA DARAJA: Real Mallorca, Deportivo La Coruna & Real Zaragoza.
No comments:
Post a Comment